Askofu Gwajima amtetea Lowassa

Askofu Gwajima amtetea Lowassa

Gwajima yuko sahihi. Utagombeaje urais usiwe na hela ? Gwajima big up sana we ni mkweli sana. We unaepinga ukitaka kugombea udiwani unategemea hutakuwa na gharama zozote au mnawaza nini ? Mwacheni Gwajima aseme ukweli
 
Hivi gwajima ndiyo anayetembea na wake za watu kama ndiye kesha laaniwa hata anayozungumza siyo yeye ni shetani aliyemwingia.

Vipi kakugongea mkeo au ? Acha mawazo mabaya wewe . kwani hapo kaongea kosa gani au we ndo mwenye laana ya kutukana watumishi wa Mungu. Acha zako
 
Nshajua ile helcopta kumbe alinunu lowassa ndo kampa gwajima ili wajikosheee
Endeleeni kutumia pesa chafu
Watanzania tumeskut tuu tunausoma mchezoo

Una hakika ? Au unaongea toka kuzimu
 
Hivi gwajima ndiyo anayetembea na wake za watu kama ndiye kesha laaniwa hata anayozungumza siyo yeye ni shetani aliyemwingia.

Ongea Key Points . kachukua wako au ? Au we ndo ulimtafutia mke wa mtu
 
Wewe unaonekana hata gazeti hujasoma au umesimuliwa, pili upate nafasi ya karibu kumfuatilia Askofu Gwajima, nadhani katika Taifa hili kwa sasa ndiye kiongozi wa dini anayeongoza kwa kukemea wezi, mafisadi, wala rushwa na kila aina ya uovu unaofanywa na serikali.. Askofu Gwajima pekee katika pita pita zangu niliwahi kumsikia akiwataja wezi wa mali za umma na kuwataka wajiwajibishe na wakigoma wawajibishwe tena sio tu kwa kuvuliwa nyadhifa zao bali kwa kurudisha mali walizoziibia taifa hili kwa miaka mingi.

Ukisoma gazeti vizuri, mwandishi ameweka wazi maneno mafupi aliyonukuu toka kwa Askofu, na pia ni jambo la wazi lisilopingika kuwa hakuna njia kuelekea urais pasipo kutumia fedha, huitaji elimu ya ngazi ya phD kufahamu jambo hili. Kwani kinachomtesa Kikwete leo hii ni nini? Kulipa fadhila kwa pesa alizotumia kabla ya kuteuliwa na chama, wakati wa kuteuliwa, baada ya kuteuliwa, kabla ya kampeni na wakati wa kampeni. Kuunda mitandao ya ushindi mambo yote haya hugharimu pesa, tatizo linakuja ni kuwa, "Je, Pesa unazotumia ni oesa halali??" Pia, kwa historia ya Askofu Gwajima angeishakuwa kiongozi huyu tena hata Mbunge kutokana na ushawishi wake kwa watu wengi hapa nchini ila kwakua si mtu wa tamaa na ameweka mbele maslahi ya imani na kazi ya Mungu anayoiyofanya... Kipindi yupo Ubungo kiongozi huyu wa dini angegombea Ubunge asingeshindwa kupitia CCM na yawezekana kukataa kwake ndio sababu ya yeye kuondolewa pale Ubungo kwani alikosesha CCM jimbo.

Wacha ukweli usemwe wazi kabisa, Ni Askofu gani au kiongozi gani wa dini alishakemea serikali juu ya ujenzi wa Misikiti/Makanisa katika public service centres zaidi ya Gwajima??
Truth must be told openly, tuache ushabiki wa kishamba... soma gazeti kwa umakini wacha kukurupuka.

Uno vizuro mkui. Hii nchi hawapendi kuona waovu wakikemewa . mwenyewe namfagilia sana Mchungaji Gwajima
 
Nenda kamwambie Gwajima, arudi kwenye mtandao akemee matumizi mabaya ya fedha. Yako matumizi sahihi na matumii maovu. Maandiko yamekataza Rushwa. Fedha ikitumika kwa kununua haki, kupotosha hukumu ama kutengeneza udanganyifu ni dhambi.

Mungu anamtaka Gwajima aseme kweli. Ninaomba mmwambie, (kama kuna mtu ana number yke ya simu ani pm niseme naye sasa hivi) aangalie asijipatie hukumu ya kushindwa kuisema kweli.

Kama hajaelewa wanapozungumza rushwa za lowasa na gharama za kawaida za uchaguzi aulize. Asikimbilie kusema jambo asilolijua.




Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa mara ya kwanza amejitosa kwenye harakati za Urais kwa kutoa kauli za ukosoaji zinazowalenga baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaoutaka Urais.

Katika mazungumzo yake na RAI, Gwajima alisema kauli zilizotolewa hivi karibuni na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Januari Makamba na Waziri Mkuu wa zamani Cleopa Msuya dhidi ya wanasiasa wenzao zina dhamira ovu ya kupakana matope.

Akizungumzia kauli hizo, Askofu Gwajima alisema wanasiasa wanaodai kuchukizwa na mafisadi na kusema kwamba Watanzania wasiwachague wagombea urais wanaotumia fedha, hawana hoja badala yake wanaendesha vita ya Urais.

"Kwani mtu yeyote mwenye akili timamu anajua kwamba bila fedha huwezi kujenga mtandao wa Urais, ili ufanikiwe unahitaji kutumia fedha kujenga mtandao, kwa mfano unahitaji usaidizi wa watu wa Rukwa, Mwanza n.k; lazima uwe na watu huko Rukwa na Mwanza na lazima utoe fedha ili watu hao waweze kusafiri, kula na kulala."

"Bila fedha huwezi kuwaza suala la Urais, maneno yao yanalenga kupotosha watu kwamba wako watu fulani wasiotumia fedha, huku wakijua ukweli kwamba kila mtu anatumia fedha, kwa mfano fomu ya kuwania Urais ni shilingi milioni tano, sasa wao hizo fedha watakuwa wamezipata wapi? Kiujumla, hatua kubwa kama ya Urais inahitaji fedha," alisema.

SOURCE: GAZETI LA RAI ALHAMISI JANUARI 8-14, 2015
 
Yaani watu hawajui ukweli shida ya watu wanasoma bila kuelewa ni wazi kweli huwezi kugombea urais bila fedha coz lzm ziitajike kwenye kampeni gwajima alikuwa right jamani
 
Pesa siyo dhambi ila matumizi mabaya kwa ajili ya uovu ndiyo dhambi. Mtu unaweza kuwa na pesa lakini ukaitumia kwa mambo yanayokubalika katika jamii kama vile kuisaidia jamii. Vile vile mtu mwingine anaweza kutumia fedha hiyohiyo kwa ajili ya uhalifu na kutimiza makusudio ya ubaya. Mtumishi yuko sawa maana huwezi kuacha kutumia pesa katika harakati za kuusaka urais. Wanachokifanya sasa hawa wawania nafasi hiyo nyeti ni kuchafuana ili kukipata kiti. Cha msingi wananchi wanatakiwa kujua ni yupi anayefaa regardless matumizi yake ya pesa.
 
Wakati mwingine hata watoto wa darasa huenda wakawa humu ndani Jamii forum, naomba Moderator muongeze Jukwaa la Watoto kwa ajili ya kudiscus habari za kitoto na kijinga ambazo kimsingi hazina mantiki.

Kusema mtu anaweza kuwa Rais bila pesa ni Ujinga uliopitiliza... Juzi tu tumemsikia Nyalandu naye katangaza nia na vyanzo vinasema Marekani inamuunga mkono, kumuunga mkono maana yake ni nini hapa?? Kuna usaidizi mkubwa wa kifedha, ushauri na mengine mengi kwahiyo hakuna madaraka yanayopatikana pasioo mtu kuwa na fedha. Urais sio kama enzi zile za kina Daudi unapakwa mafuta na Mtume Samwel na kutawala kama ilivyokua kwa Sauli wa Israel au mifumo mingine ya kulithishana madaraka.

Urais ni hatamu ya juu katika nchi anayejipanga sana na zaidi ya wengine ana nafasi kubwa ya kushinda kama mambo yote yatakua sawa (if all things remain constant).

Namuunga Mkono Askofu Gwajima katika suala hili kwa asilimia 100% na pia hakuna mahali amesema anatetea wezi au wala rushwa ni siasa za kwenye magazeti kwani unapokaribia uchaguzi makundi mengi hujitokeza kuwapinga wengine isitoshe hata muandishi wa habari hii akawa yupo kambi nyingine au pinzani na Lowasa na akawa anakerwa na ukaribu wa Lowasa na Gwajima.

Mbona Dr. Slaa alienda kwa Gwajima na akaombewa?? Na akatabiriwa mazuri... kwanini msiongelee hayo?? Hili ni jambo la kitoto sana limeletwa mtoa hoja asiyejua anachokifanya au amekurupuka.
 
Gwajima tapeli kama matapeli wengine tu naye ni miongoni mwa watu waliogawiwa hela na mafisadi lakini zitamtokea puani.

Umetapeliwa nini ? Tatizo hii nchi mshazoea kuburuzwa wakijitokeza watu wanaosema ukweli mnawaona matapeli. Acha zako ungekuwa wewe unagombea serikali za mitaa ungefanya bure ? Acha upumbavu kuongea mambo yasokuwa na msingi. Nyie ndo wachafuzi wa nchi hii Maana siku zote MTU akisema kweli eti fisadi. Pyuuuuuuuuuu
 
Katika watu niliowai kuwasikia ktk makanisa na cd zao za mahubiri niliwai kumsikia gwajima yaani mm na ubishi wangu nilimuekewa sn hususan palw anapo waweka wazi wezi wa nchi hii pia gwajima huyuhuyu aliwai kuwavua nguo na kuwaacha freemansons wa Tanzania uchi kabisa pia ni huyu jamaa aliwai kusema Tanzania lzm itakuwa vzr kiuchumi kama haitoshi aliwaalika viongozi wapande zote ccm na chadema huyu jamaa hapendelei mi nahisi wanamchafua ccm maama ni kiboko yao..ni maoni yangu hayo wadau...
 
Kusema ukweli kama wachungaji wote wangekuwa kama huyo jamaa sijui tanzania ingekuaje anaumbua kweli
 
Ninawaza tu hapa kwa sauti! Inaelekea kwamba CCM imebadilika sana nyakati hizi za Kikwete!!?? Hivi kazi ya kujenga mtandao ni ya mtu binafsi, au ni ya Chama? Hivi mgombea Urais kutoka Chama Cha Mapinduzi, ni mgombea binafsi, au ni mgombea wa Chama? Je, Mwinyi na Mkapa waliijenga binafsi mitandao yao, au ni Chama Cha Mapinduzi kilichowajengea mitandao yao? Je, Mwinyi na Mkapa, ni nani aliyewalipia ada za fomu zao?
Sasa endelea kuwaza ukishapata jibu ndo utajua analofanya EL ni sahihi ama si sahihi,japo mimi nimefikia hitimisho kwamba ni hilo la pili..
 
Wewe unaonekana hata gazeti hujasoma au umesimuliwa, pili upate nafasi ya karibu kumfuatilia Askofu Gwajima, nadhani katika Taifa hili kwa sasa ndiye kiongozi wa dini anayeongoza kwa kukemea wezi, mafisadi, wala rushwa na kila aina ya uovu unaofanywa na serikali.. Askofu Gwajima pekee katika pita pita zangu niliwahi kumsikia akiwataja wezi wa mali za umma na kuwataka wajiwajibishe na wakigoma wawajibishwe tena sio tu kwa kuvuliwa nyadhifa zao bali kwa kurudisha mali walizoziibia taifa hili kwa miaka mingi.

Ukisoma gazeti vizuri, mwandishi ameweka wazi maneno mafupi aliyonukuu toka kwa Askofu, na pia ni jambo la wazi lisilopingika kuwa hakuna njia kuelekea urais pasipo kutumia fedha, huitaji elimu ya ngazi ya phD kufahamu jambo hili. Kwani kinachomtesa Kikwete leo hii ni nini? Kulipa fadhila kwa pesa alizotumia kabla ya kuteuliwa na chama, wakati wa kuteuliwa, baada ya kuteuliwa, kabla ya kampeni na wakati wa kampeni. Kuunda mitandao ya ushindi mambo yote haya hugharimu pesa, tatizo linakuja ni kuwa, "Je, Pesa unazotumia ni oesa halali??" Pia, kwa historia ya Askofu Gwajima angeishakuwa kiongozi huyu tena hata Mbunge kutokana na ushawishi wake kwa watu wengi hapa nchini ila kwakua si mtu wa tamaa na ameweka mbele maslahi ya imani na kazi ya Mungu anayoiyofanya... Kipindi yupo Ubungo kiongozi huyu wa dini angegombea Ubunge asingeshindwa kupitia CCM na yawezekana kukataa kwake ndio sababu ya yeye kuondolewa pale Ubungo kwani alikosesha CCM jimbo.

Wacha ukweli usemwe wazi kabisa, Ni Askofu gani au kiongozi gani wa dini alishakemea serikali juu ya ujenzi wa Misikiti/Makanisa katika public service centres zaidi ya Gwajima??
Truth must be told openly, tuache ushabiki wa kishamba... soma gazeti kwa umakini wacha kukurupuka.

Waambie kabisa hawajui hawa mwana bwatuka tu
 
Sijui kashamwacha yule mwimbaji wa nyimbo za Injili.Halafu kuna ile scandal ya kuzaa na mke wa mtu Dr fulani sijui kesi imemalizika au imechinjiwa baharini.

Juzi alipomsema CAG mlikesha kumtetea leo kamsema msiempenda Kawa mbaya, vigeu geu
 
Nampenda Askofu Gwajima kwa sababu ni msema kweli, na huu ni ukweli usiopingika Membe ni mnafiki na amesema unafiki suala la kua hatumii pesa ni uongo uliopitiliza kwani nani asiyewajua makada wa CCM wanaompigia debe, je wafanya kazi bure? Kazi anayoifanya Makonda kumtukana Lowasa hadharani unafikiri ni kazi anayoifanya kwa utashi wake binafsi?? Lazima ukweli usemwe...

Unapoona akina Membe wamekaa kimya wanajifanya wasafi yawezekana wao ndio wakawa wanafanya makubwa zaidi hata ya Lowasa kwa kuwa wako kimya na hatujui wanawaza nini???

Membe anatoa ahadi za uongozi katika serikali kwa makada wanaombeba nani asiyejua jambo hilo.??

Askofu Gwajima, endelea kusema ukweli, na ndio siri ya ukweli duniani kote, ukweli huumiza lakini ndio dawa ya maendeleo na mafanikio.

Waandishi wa habari lazima wajifunze kutofautisha kuandikia hisia na mapenzi yao na kuandikia uhalisia wa mambo juu ya kile kinachoendelea.
Songa mbele Askofu Gwajima na uendelee kuusema zaidi ukweli ili tuujue ukweli wa wezi hawa wanaojifanya wasafi na kuwanyooshea wengine vidole.
 
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa mara ya kwanza amejitosa kwenye harakati za Urais kwa kutoa kauli za ukosoaji zinazowalenga baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaoutaka Urais.

Katika mazungumzo yake na RAI, Gwajima alisema kauli zilizotolewa hivi karibuni na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Januari Makamba na Waziri Mkuu wa zamani Cleopa Msuya dhidi ya wanasiasa wenzao zina dhamira ovu ya kupakana matope.

Akizungumzia kauli hizo, Askofu Gwajima alisema wanasiasa wanaodai kuchukizwa na mafisadi na kusema kwamba Watanzania wasiwachague wagombea urais wanaotumia fedha, hawana hoja badala yake wanaendesha vita ya Urais.

"Kwani mtu yeyote mwenye akili timamu anajua kwamba bila fedha huwezi kujenga mtandao wa Urais, ili ufanikiwe unahitaji kutumia fedha kujenga mtandao, kwa mfano unahitaji usaidizi wa watu wa Rukwa, Mwanza n.k; lazima uwe na watu huko Rukwa na Mwanza na lazima utoe fedha ili watu hao waweze kusafiri, kula na kulala."

"Bila fedha huwezi kuwaza suala la Urais, maneno yao yanalenga kupotosha watu kwamba wako watu fulani wasiotumia fedha, huku wakijua ukweli kwamba kila mtu anatumia fedha, kwa mfano fomu ya kuwania Urais ni shilingi milioni tano, sasa wao hizo fedha watakuwa wamezipata wapi? Kiujumla, hatua kubwa kama ya Urais inahitaji fedha," alisema.

SOURCE: GAZETI LA RAI ALHAMISI JANUARI 8-14, 2015

Askofu wa kujipa mwenyewe kama kakobe. Eti askofu. Uaskofu si kitu cha kujibandika tu mwenyewe. Kalala kaamka anaanzisha kanisa na kuwa mkuu. Tuyaache hayo. Fisadi yeyote hafai kuwa Kiongozi mahali popote na ktk nafasi yoyote ya uongozi. Kwa mantiki hiyo fisadi yeyote na wafuasi wake katika uchaguzi wa Oktoba 2015 wasichaguliwe ili nchi yetu ipate viongozi safi watakaotuongoza ktk maendeleo, amani na utulivu.
 
Askofu wa kujipa mwenyewe kama kakobe. Eti askofu. Uaskofu si kitu cha kujibandika tu mwenyewe. Kalala kaamka anaanzisha kanisa na kuwa mkuu. Tuyaache hayo. Fisadi yeyote hafai kuwa Kiongozi mahali popote na ktk nafasi yoyote ya uongozi. Kwa mantiki hiyo fisadi yeyote na wafuasi wake katika uchaguzi wa Oktoba 2015 wasichaguliwe ili nchi yetu ipate viongozi safi watakaotuongoza ktk maendeleo, amani na utulivu.

Naomba nitofautiane na wewe katika mistari yako miwili ya mwanzo. Kulingana na Biblia, Askofu siyo hadhi tu ya kupewa, ni kazi (1TIMOTHEO 3:1). Ni kazi gani? Ni Mwangalizi wa Makanisa kadha yaliyo chini ya uangalizi wake (2WAKORINTHO 11:28). Kakobe ni Mwangalizi wa Makanisa zaidi ya elfu moja nchi nzima yaliyo chini ya uangalizi wake, na Gwajima naye pia ana Makanisa yaliyo chini ya uangalizi wake, hivyo wana sifa ya kuitwa Maaskofu hata kama desturi za dini yako ni tofauti! Hata hivyo umenifurahisha uliposema,"TUYAACHE HAYO". Hapo sawa, tuzungumzie tu alichokisema Gwajima kama kina mantiki au la!
 
sasa mbona sijaona jina la lowassa hapo
 
Back
Top Bottom