johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 84,035
- 142,134
Askofu Prof Gamanywa wa BCIC amesema mwaka 2017 alifanya Utafiti kuhusu kauli ya " Kila aibarikiye Israel atabarikiwa na ailaaniye atalaaniwa" na akagundua Kauli Hiyo inaishi kiuhalisia
Askofu Prof Gamanywa amesema kwanza aliyachukua Mataifa 10 yenye Uchumi bora duniani na kuangalia Uhusiano wao na Israel ambayo ni Marekani, China, Japan, German, UK, France, India, Italy, Brazil na Canada
Alichogundua ni kwamba nchi hizo zote zina mahusiano mema na Israel ambapo kwa mfano 70% ya Wawekezaji wa Marekani ni Wayahudi, China ina Viwanda zaidi ya 1000 vya Wayahudi, India ni mnunuzi mkuu wa Silaha za Israel (50%), Ujerumani inaongoza kwa kuuza bidhaa za Israel barani Ulaya nk...nk
Hizo zote ni Baraka Nchi hizo tajiri duniani zinapata kwa sababu ya kuibariki Israel
Askofu Gamanywa amesema Tanzania ilianza kuharibikiwa baada ya kuvunja Uhusiano na Israel Ndio Vita ya Kagera, Njaa, Umaskini, Utapeli vikatuandama hadi pale Rais wa awamu ya 5 aliporejesha Uhusiano na Israel Ndio tukaingia kwenye Uchumi wa Kati ikiwa ni Baraka za kuibariki Israel
Baba askofu amesema Usipoibariki Israel utalaaniwa tu na hiyo haina Mbadala
Source: WAPO TV
Askofu Prof Gamanywa amesema kwanza aliyachukua Mataifa 10 yenye Uchumi bora duniani na kuangalia Uhusiano wao na Israel ambayo ni Marekani, China, Japan, German, UK, France, India, Italy, Brazil na Canada
Alichogundua ni kwamba nchi hizo zote zina mahusiano mema na Israel ambapo kwa mfano 70% ya Wawekezaji wa Marekani ni Wayahudi, China ina Viwanda zaidi ya 1000 vya Wayahudi, India ni mnunuzi mkuu wa Silaha za Israel (50%), Ujerumani inaongoza kwa kuuza bidhaa za Israel barani Ulaya nk...nk
Hizo zote ni Baraka Nchi hizo tajiri duniani zinapata kwa sababu ya kuibariki Israel
Askofu Gamanywa amesema Tanzania ilianza kuharibikiwa baada ya kuvunja Uhusiano na Israel Ndio Vita ya Kagera, Njaa, Umaskini, Utapeli vikatuandama hadi pale Rais wa awamu ya 5 aliporejesha Uhusiano na Israel Ndio tukaingia kwenye Uchumi wa Kati ikiwa ni Baraka za kuibariki Israel
Baba askofu amesema Usipoibariki Israel utalaaniwa tu na hiyo haina Mbadala
Source: WAPO TV