Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mpanda Eusebius Nzigirwa amesema katika kusherekea sikukuu ya Christmas siku hiyo inawakumbusha watu thamani na hadhi ya utu wa mwanadamu na kanisa limekuwa likisimama kukemea kwa sauti kubwa wale wanaojaribu kuuchezea utu wa mwanadamu.
Askofu Nzigirwa amesema hayo Disemba 25, 2025 wakati wa mahubiri ya sikukuu ya Christmas Jimbo la Mpanda ambapo amesema inapotokea mwanadamu yeyote anamdharau binadamu mwingine kwa namna yeyote ni kudharau hadhi na thamani ya binadamu
aliyopewa na Mungu kanisa litapaza sauti kupinga.
"adhimisho hili liwafundishe thamani na hadhi ya mwanadamu na ndiyo maana kanisa limekuwa likitoa sauti kubwa kwa vitendo vya udhalilishaji limetoa sauti kubwa linavyopinga uumbaji ulioumbwa na Mungu kwa thamani kubwa anatokea binadamu anauchezea chezea"
Amesema ni muhimu watu kuzingatia uumbaji wa mungu na kuacha vitendo vunavyokiuka maadili na thamani ya uumbaji ikiwemo wanaume kujigeuza tabia za wanawake na wanawake kujigeuza vitendo vya kiume ni kudhalilisha utu na uumbaji wa Mungu.
Amesisitiza kuwaombea watoto walio katika dhiki katika matumbo ya mama zao ili wanapozaliwa wawe na uwezo wa kustahimili kama ilivokuwa kuzaliwa Kwa Yesu kristo.
Source Jambo TV
Askofu Nzigirwa amesema hayo Disemba 25, 2025 wakati wa mahubiri ya sikukuu ya Christmas Jimbo la Mpanda ambapo amesema inapotokea mwanadamu yeyote anamdharau binadamu mwingine kwa namna yeyote ni kudharau hadhi na thamani ya binadamu
aliyopewa na Mungu kanisa litapaza sauti kupinga.
"adhimisho hili liwafundishe thamani na hadhi ya mwanadamu na ndiyo maana kanisa limekuwa likitoa sauti kubwa kwa vitendo vya udhalilishaji limetoa sauti kubwa linavyopinga uumbaji ulioumbwa na Mungu kwa thamani kubwa anatokea binadamu anauchezea chezea"
Amesema ni muhimu watu kuzingatia uumbaji wa mungu na kuacha vitendo vunavyokiuka maadili na thamani ya uumbaji ikiwemo wanaume kujigeuza tabia za wanawake na wanawake kujigeuza vitendo vya kiume ni kudhalilisha utu na uumbaji wa Mungu.
Amesisitiza kuwaombea watoto walio katika dhiki katika matumbo ya mama zao ili wanapozaliwa wawe na uwezo wa kustahimili kama ilivokuwa kuzaliwa Kwa Yesu kristo.
Source Jambo TV