BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
CORONA BADO IPO DUNIANI
Kufuatia taharuki inayotokana na vifo kadhaa mwishoni na mwanzoni mwa mwaka hapa Karagwe, watu wengi wamekuwa wanapiga simu kwangu na kwa uongozi wa hospitali teule ya Nyakahanga kuulizia kulikoni? Jibu hili litoshe kusaidia kujibu maswali hayo:
1. Corona BADO iko duniani. Tanzania ni sehemu ya dunia. Malizia sehemu inayobaki. Maswali yaliyobaki waulizeni wenye dhamana na masuala ya Afya ngazi ya Mkoa na Wilaya.
2. Tanzania si makao makuu ya Mungu. Yeye ni wa wakati wote na wa mahali pote. Mahali alipo, Corona yaweza kuwapo pia. Wenye dhambi na watakatifu wote wanaugua na kufa. Makutano yetu ni ufufuko.
3. Uhai tulio nao si mali ya serikali wala ya dini yoyote. Tuna wajibu wa kuulinda. Tuchukue tahadhari zote bila kusubiri maagizo ya serikali au ya dini. Nawa mikono, tumia barakoa, jiepushe na mikusanyiko, nyungu haizuiwi na tiba mbadala nyingine hazizuiwi. Ramli ni marufuku hospitalini.
4. Kama si lazima usiende hospitalini kutembea. Kama si lazima tibiwa nyumbani kwako. Kama si lazima usizushe kuwa una ugonjwa ambao haujathibitishwa kwa vipimo.
5. Tunapakana na nchi zilizojitangaza kuwa zina maambukizi makubwa ya Corona. Majirani wema huzaa watoto wanaofanana kwa sababu ya kuhusiana vizuri. Hii ni vita, ujirani uchukue viwango vipya.
6. Idadi ya wagonjwa wenye matatizo ya kupumua imeongezeka ndani ya muda mfupi. Yawezekana ni uchovu wa mwisho wa mwaka! Idadi ya mitungi ya Oksijeni tuliyo nayo ni ndogo. Wasamaria wema wanakaribishwa kusaidia mitungi zaidi. Siasa safi ni kujitolea mitungi zaidi ili wenye shida ya kupumua wasaidiwe. Karibuni.
Kwa nia njema na kwa mapenzi makubwa kwa watu nilioagizwa kuwachunga na kuwalisha.
Kufuatia taharuki inayotokana na vifo kadhaa mwishoni na mwanzoni mwa mwaka hapa Karagwe, watu wengi wamekuwa wanapiga simu kwangu na kwa uongozi wa hospitali teule ya Nyakahanga kuulizia kulikoni? Jibu hili litoshe kusaidia kujibu maswali hayo:
1. Corona BADO iko duniani. Tanzania ni sehemu ya dunia. Malizia sehemu inayobaki. Maswali yaliyobaki waulizeni wenye dhamana na masuala ya Afya ngazi ya Mkoa na Wilaya.
2. Tanzania si makao makuu ya Mungu. Yeye ni wa wakati wote na wa mahali pote. Mahali alipo, Corona yaweza kuwapo pia. Wenye dhambi na watakatifu wote wanaugua na kufa. Makutano yetu ni ufufuko.
3. Uhai tulio nao si mali ya serikali wala ya dini yoyote. Tuna wajibu wa kuulinda. Tuchukue tahadhari zote bila kusubiri maagizo ya serikali au ya dini. Nawa mikono, tumia barakoa, jiepushe na mikusanyiko, nyungu haizuiwi na tiba mbadala nyingine hazizuiwi. Ramli ni marufuku hospitalini.
4. Kama si lazima usiende hospitalini kutembea. Kama si lazima tibiwa nyumbani kwako. Kama si lazima usizushe kuwa una ugonjwa ambao haujathibitishwa kwa vipimo.
5. Tunapakana na nchi zilizojitangaza kuwa zina maambukizi makubwa ya Corona. Majirani wema huzaa watoto wanaofanana kwa sababu ya kuhusiana vizuri. Hii ni vita, ujirani uchukue viwango vipya.
6. Idadi ya wagonjwa wenye matatizo ya kupumua imeongezeka ndani ya muda mfupi. Yawezekana ni uchovu wa mwisho wa mwaka! Idadi ya mitungi ya Oksijeni tuliyo nayo ni ndogo. Wasamaria wema wanakaribishwa kusaidia mitungi zaidi. Siasa safi ni kujitolea mitungi zaidi ili wenye shida ya kupumua wasaidiwe. Karibuni.
Kwa nia njema na kwa mapenzi makubwa kwa watu nilioagizwa kuwachunga na kuwalisha.