Askofu Bagonza: Kubambikiwa kiti na Microphone ni hatari kuliko Corona, barakoa na chanjo

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,013
HATARI!!!

KUBAMBIKIWA KITI na MICROPHONE ni Hatari kuliko Corona, Barakoa na Chanjo!

Rais Jakaya Kikwete aliwahi kulijulisha Taifa kuwa kutokana uhasama ndani ya medani za Kisiasa, ilifika wakati "watu walikuwa hawaachiani glasi walipotoka kwenda maliwatoni". Siasa za makundi na uhasama vilitawala na kuondoa kutoaminiana.

Wakati fulani hayati Samuel Sitta akiwa Spika, zilitolewa tuhuma za Mbunge fulani kuonekana akimimina vitu kama unga kwenye baadhi ya viti vya wabunge. Tendo hilo lilizua tafrani bungeni.

Wiki hii Taifa limeshuhudia Mbunge wa CCM ambaye ni Askofu wa Kanisa, akiwa mbele ya Kamati ya Bunge la Wana CCM, akikataa kutumia kiti na microphones vilivyoandaliwa ili aweze kuvitumia wakati anahojiwa na Kamati.

Kitendo hicho si cha kupuuza kwa sababu zifuatazo:

1. Tuhuma za muda mrefu kuhusu kuwekeana sumu, kuuana na kukolimbana, Sasa zinapata msukumo mpya.

2. Aliyeshtuka ni Askofu anayeaminika na watu wengi. Kwa hiyo mashaka yake yanapewa uzito.

3. Ziko tuhuma za watu KUBAMBIKIWA Kesi mbaya kwa sababu za Kisiasa. Kama aliye ndani ya mfumo wa utawala anashtuka, je aliye nje afanye nini?

4. Askofu huyu amekuwa na mashaka juu ya uwepo wa Corona, baadaye akawa na mashaka juu ya chanjo. Sasa anashtukia kiti na microphone. Nini kinafuata?

5. Ikiwa viti na microphones vinaweza kutumiwa kudhuru mtu asiyekubaliana na mfumo wa utawala, je usalama wa wanaosimamia mfumo huo ukoje?

6. Ikiwa jengo la bunge ambalo ni madhabahu ya Taifa letu inahofiwa, je maeneo mengine ya utawala yakoje?

7. Madai ya Askofu kuwa Rais hana tatizo lakini washauri na wasaidizi wake ndio wabaya, yana taswira gani kwa usalama wa Rais? Kumbuka haya yamesemwa na Mbunge na mwana CCM.

8. Mungu anayeweza kumlinda mtu dhidi ya Corona anashindwaje kumlinda mtu na madhara ya kiti na microphone?

Taifa letu linaumwa. Corona ni cha mtoto. Tutafute suluhu nje ya SULUHU. Naendelea kusisitiza, "Kifo cha mbwa huanza kwa kupoteza uwezo wa kunusa hatari".


Askofu Bagonza
 
Nadhani siasa ndivyo zilivyo haijalishi chama ni kipi

Katika kuendelea kuwa mwenyekiti wa kudumu pale Chadema, Mbowe aliwahi kutuonya walioitaka nafasi ya uenyekiti kwamba "SUMU HIONJWI!!"

NA HAKUNA KITU MLIMFANYA☺☺

Imani rohoni, Akili kichwani📍🔨
 
What I like about Bagonza ni his bias

he is very polarized hadi unapata taabu kuelewa dhana ya leadership abs balanced opinion huwa inaisha ukifika daraja gani la wito wake
Binafsi nina hiyo Bias mnoo,
Huwa naamini kila mtu aliyepo kijani hayuko balanced kiakili, lazima atakuwa na mtindio wa akili-Hivyo nitakuwa surprised kukutana na mtu smart kwenye hicho chama.
 
Nadhani siasa ndivyo zilivyo haijalishi chama ni kipi

Katika kuendelea kuwa mwenyekiti wa kudumu pale Chadema, Mbowe aliwahi kutuonya walioitaka nafasi ya uenyekiti kwamba "SUMU HIONJWI!!"

NA HAKUNA KITU MLIMFANYA☺☺
Ule ulikuwa ni usemi tu. Mambo yako CCM.

Mangula alipoumwa kwenye mkutano wa chama tulisikia kuwa aliwekewa sumu.

Kolimba alipoitwa kujieleza, wote tunajua alitokaje.

Membe alipoitwa kwenye kikao cha maadili alikataa maji.
 
Huyu Bagonza naye anaanza kuishiwa kiasi cha kuwa lunatic. Kama anamtetea tapeli Gwajima, ameingia choo ya kike. Si waanzishe chama cha siasa badala ya kujificha nyuma ya majoho na neno la Mungu.
 
Binafsi nina hiyo Bias mnoo,
Huwa naamini kila mtu aliyepo kijani hayuko balanced kiakili,lazima atakuwa na mtindio wa akili-Hivyo nitakuwa surprised kukutana na mtu smart kwenye hicho chama.
Simple generalization that implies laziness in thinking so to speak. Whether CCM are good or bad, there must be all types of people good and bad just like in the opposition. This is a rationalized nuance of things.
 
Thank you 🙏🏾 🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾👍🏽
Binafsi nina hiyo Bias mnoo,
Huwa naamini kila mtu aliyepo kijani hayuko balanced kiakili,lazima atakuwa na mtindio wa akili-Hivyo nitakuwa surprised kukutana na mtu smart kwenye hicho chama.
 
Marehemu Horace Kolimba (RIP) anasemekana kuuwawa na CCM ya hayati Mwl Julius K. Nyerere (RIP). Hakika wote walikufa.

Ukiua, utauwawa.
Ukitesa, utateswa.
Ukiiba, utaibiwa.
Ukipora, utaporwa.
Ukitesa, utateswa.
Ukiteka, utatekwa.
Ukidanganya, utadanganywa.
Ukibaka, utabakwa.
Ukilaani, utalaaniwa.
Ukibambikia, utabambikiwa.

Omba Mungu umalizane na dunia bila kuyabeba yote hayo, baada ya kifo. Malipizi huko kusikokuwa na damu na nyama yanatisha.
 
Marehemu Horace Kolimba (RIP) anasemekana kuuwawa na CCM ya hayati Mwl Julius K. Nyerere (RIP). Hakika wote walikufa.

Ukiua, utauwawa.
Ukitesa, utateswa.
Ukiiba, utaibiwa.
Ukipora, utaporwa.
Ukitesa, utateswa.
Ukiteka, utatekwa.
Ukidanganya, utadanganywa.
Ukibaka, utabakwa.
Ukilaani, utalaaniwa.
Ukibambikia, utabambikiwa.

Omba Mungu umalizane na dunia bila kuyabeba yote hayo, baada ya kifo. Malipizi huko kusikokuwa na damu na nyama yanatisha.
Wanaofanya uliyoorodhesha na yasiwatokee hizo antitheses zake. Amin aliua hakuuawa. Yesu hakuua lakini aliuawa. Moi na Kenyatta the first waliibia Kenya sana ila hawakuibiwa pia waliua sana na hawakuuawa. Zuma alibaka hajabakwa bado. Mandela alifungwa hakufunga mtu. nk nk nk
 
Wanaofanya uliyoorodhesha na yasiwatokee hizo antitheses zake. Amin aliua hakuuawa. Yesu hakuua lakini aliuawa. Moi na Kenyatta the first waliibia Kenya sana ila hawakuibiwa pia waliua sana na hawakuuawa. Zuma alibaka hajabakwa bado. Mandela alifungwa hakufunga mtu. nk nk nk
Dunia hii ya mwili wa damu na nyama ni sehemu ndogo tu ya safari. Hayo malipo siyo lazima uyaone kwa macho.
 
7. Madai ya Askofu kuwa Rais hana tatizo lakini washauri na wasaidizi wake ndio wabaya, yana taswira gani kwa usalama wa Rais? Kumbuka haya yamesemwa na Mbunge na mwana CCM.
Hapana, sentensi hii si sawa, wote wana tatizo, Gwajima anamuogopa Rais asishushe amri juu yake. Tatizo ni Samia, weak, extra ordinary weak president,
 
HATARI!!!

KUBAMBIKIWA KITI na MICROPHONE ni Hatari kuliko Corona, Barakoa na Chanjo!

Rais Jakaya Kikwete aliwahi kulijulisha Taifa kuwa kutokana uhasama ndani ya medani za Kisiasa, ilifika wakati "watu walikuwa hawaachiani glasi walipotoka kwenda maliwatoni". Siasa za makundi na uhasama vilitawala na kuondoa kutoaminiana.

Wakati fulani hayati Samuel Sitta akiwa Spika, zilitolewa tuhuma za Mbunge fulani kuonekana akimimina vitu kama unga kwenye baadhi ya viti vya wabunge. Tendo hilo lilizua tafrani bungeni.

Wiki hii Taifa limeshuhudia Mbunge wa CCM ambaye ni Askofu wa Kanisa, akiwa mbele ya Kamati ya Bunge la Wana CCM, akikataa kutumia kiti na microphones vilivyoandaliwa ili aweze kuvitumia wakati anahojiwa na Kamati.

Kitendo hicho si cha kupuuza kwa sababu zifuatazo:

1. Tuhuma za muda mrefu kuhusu kuwekeana sumu, kuuana na kukolimbana, Sasa zinapata msukumo mpya.

2. Aliyeshtuka ni Askofu anayeaminika na watu wengi. Kwa hiyo mashaka yake yanapewa uzito.

3. Ziko tuhuma za watu KUBAMBIKIWA Kesi mbaya kwa sababu za Kisiasa. Kama aliye ndani ya mfumo wa utawala anashtuka, je aliye nje afanye nini?

4. Askofu huyu amekuwa na mashaka juu ya uwepo wa Corona, baadaye akawa na mashaka juu ya chanjo. Sasa anashtukia kiti na microphone. Nini kinafuata?

5. Ikiwa viti na microphones vinaweza kutumiwa kudhuru mtu asiyekubaliana na mfumo wa utawala, je usalama wa wanaosimamia mfumo huo ukoje?

6. Ikiwa jengo la bunge ambalo ni madhabahu ya Taifa letu inahofiwa, je maeneo mengine ya utawala yakoje?

7. Madai ya Askofu kuwa Rais hana tatizo lakini washauri na wasaidizi wake ndio wabaya, yana taswira gani kwa usalama wa Rais? Kumbuka haya yamesemwa na Mbunge na mwana CCM.

8. Mungu anayeweza kumlinda mtu dhidi ya Corona anashindwaje kumlinda mtu na madhara ya kiti na microphone?

Taifa letu linaumwa. Corona ni cha mtoto. Tutafute suluhu nje ya SULUHU. Naendelea kusisitiza, "Kifo cha mbwa huanza kwa kupoteza uwezo wa kunusa hatari".

Askofu Bagonza
Askofu wa Taifa kasema, Sasa tuyaishi na kuyatendea kazi maangalizo haya, kwa ajili ya ustawi wetu na taifa letu
 
HATARI!!!

KUBAMBIKIWA KITI na MICROPHONE ni Hatari kuliko Corona, Barakoa na Chanjo!

Rais Jakaya Kikwete aliwahi kulijulisha Taifa kuwa kutokana uhasama ndani ya medani za Kisiasa, ilifika wakati "watu walikuwa hawaachiani glasi walipotoka kwenda maliwatoni". Siasa za makundi na uhasama vilitawala na kuondoa kutoaminiana.

Wakati fulani hayati Samuel Sitta akiwa Spika, zilitolewa tuhuma za Mbunge fulani kuonekana akimimina vitu kama unga kwenye baadhi ya viti vya wabunge. Tendo hilo lilizua tafrani bungeni.

Wiki hii Taifa limeshuhudia Mbunge wa CCM ambaye ni Askofu wa Kanisa, akiwa mbele ya Kamati ya Bunge la Wana CCM, akikataa kutumia kiti na microphones vilivyoandaliwa ili aweze kuvitumia wakati anahojiwa na Kamati.

Kitendo hicho si cha kupuuza kwa sababu zifuatazo:

1. Tuhuma za muda mrefu kuhusu kuwekeana sumu, kuuana na kukolimbana, Sasa zinapata msukumo mpya.

2. Aliyeshtuka ni Askofu anayeaminika na watu wengi. Kwa hiyo mashaka yake yanapewa uzito.

3. Ziko tuhuma za watu KUBAMBIKIWA Kesi mbaya kwa sababu za Kisiasa. Kama aliye ndani ya mfumo wa utawala anashtuka, je aliye nje afanye nini?

4. Askofu huyu amekuwa na mashaka juu ya uwepo wa Corona, baadaye akawa na mashaka juu ya chanjo. Sasa anashtukia kiti na microphone. Nini kinafuata?

5. Ikiwa viti na microphones vinaweza kutumiwa kudhuru mtu asiyekubaliana na mfumo wa utawala, je usalama wa wanaosimamia mfumo huo ukoje?

6. Ikiwa jengo la bunge ambalo ni madhabahu ya Taifa letu inahofiwa, je maeneo mengine ya utawala yakoje?

7. Madai ya Askofu kuwa Rais hana tatizo lakini washauri na wasaidizi wake ndio wabaya, yana taswira gani kwa usalama wa Rais? Kumbuka haya yamesemwa na Mbunge na mwana CCM.

8. Mungu anayeweza kumlinda mtu dhidi ya Corona anashindwaje kumlinda mtu na madhara ya kiti na microphone?

Taifa letu linaumwa. Corona ni cha mtoto. Tutafute suluhu nje ya SULUHU. Naendelea kusisitiza, "Kifo cha mbwa huanza kwa kupoteza uwezo wa kunusa hatari".


Askofu Bagonza
Walíanza na kuthibiti upinzani ndani na nje ya bunge na wamehamia kwa wenyewe kwa wenyewe , tusubirie tuone mwisho wake!
 
Huyo Askofu ana ugonjwa wa kushtuka, Corona ikamshtua, chanjo ikamshtua, kuitwa na kamati ya bunge akashtuka mpaka akaomba na vidonge atulize pressure.
 
Huyu Bagonza naye anaanza kuishiwa kiasi cha kuwa lunatic. Kama anamtetea tapeli Gwajima, ameingia choo ya kike. Si waanzishe chama cha siasa badala ya kujificha nyuma ya majoho na neno la Mungu.

NIMEMWALIKA MUNGU HAPA ANAKUSIKIA, ANDIKA GWAJIMA ANAKOSA GANI LA KATIKA HILI. WEWE ULITAKAJE? AMEKUTAPELI NINI? NA KATIKA HOJA ZAKE ALOZISHITAHTAIKWA NAZO WEWE UNAELEWA NINI? USITUKANE BALI JIBU HOJA LA SIVYO NYAMAZA.
 
Back
Top Bottom