Askofu Anthony Mayalla is no more


Thank you man. Angalau Mwanakijiji ana vi detail detail kwenye taarifa zake sometimes, unapata ka biography ka marehemu kujua what kinda man we are dealing with here. Poleni wafiwa, wakatoliki na Watanzania sote.
 
Asante Lunyungu kwa post hii. Masanilo alishatoka na breaking news yake dakika 42 kabla ya post yako. Nashauri umuombe mod aiunganishe ili tuendelee na eulogy moja for this great man
RIP Bishop Mayalla.


Mayala is our hero kanda ya Ziwa
Fika Parokia za Komuge, Zanaki, Mugumu,Tarime ,Sirari , Mwisenge , Fika kule Nyamiongo, Makoko Seminary , Kiagata , utajua kwamba Mayala alitumia muda wake kuwatumia Watanzania na kuleta maendeleo
 
Unafiki gani aliokufanyia? Weka wazi watu tujue.
RIP askofu Mayalla, utakumbukwa daima hapa chuoni bugando.

Mkuu Yo Yo ana agenda zake za siri au hajui analolisema au anasema tu ili kukuza wachangiaji

RIP Mayalla
 
Yo Yo kweli watu wamefiwa wewe unawabeza! Great thinkers ni watu wenye mitazamo ya ndani zaidi ya hisia. Humfahamu huyu marehemu, huelekei hata kuwafahamu hao maaskofu, au kwa lugha nyingine huna ushahidi wa huo unafiki, sidhani kama utakuwa nao (evidence ni jinsi unavyoandika). Kwa nini kama inakukera wenzio kumkumbuka mtu wao wanaomheshimu usiende kwenye thread nyingine. Hivi MOD hawezi akawazuia watu kama hawa humu ndani?
 
Inna lillah wa inna ilayhi rajiun
We All Belong to God and To Him We Shall Return.’

Poleni wafiwa na wakatoliki wote kwa ujumla!

 
sina la kusema maana huyu baba askofu kanisaidia sana, wakati niko pale sengerema seminari.pumzika baba

naomba chanzo cha kifo chake jamani
 
Jamani wenzetu wakatoliki wa jimbo la Mwanza poleni sana kwa msiba huu.
Mungu awatie nguvu katika wakati huu mgumu.
 
From Cananews:


Upumzike kwa amani Askofu Mayala
 
RIP Bishop Antony Mayala

We All Belong to God and To Him We Shall Return
 
Hizi ni habari za kusikitisha sana hasa sisi ambaye tulikuwa nae karibu na ametulea vizuri sana kipindi chote tulichokuwa pale Seminary ya Nyegezi,kwa habari nilizopata toka kwenye source iliyokuwa karibu ni kwamba Mhashamu Baba Askofu alikumbwa na low pressure na alifikishiwa ICU pale hospitali ya rufaa ya Bugando majira ya mchana ambapo mauti yalimkumba.R.I.P....Amen
 
R.I.P Baba Mayala nitakukumbuka kwa ushauri wako ulionipa pindi nipo pale Makoko Seminary baba. Machozi yangu yatafutwa na Mungu. Enzi za uhamisho wa Baberi baada ya Seminary yetu Makoko kufungwa ulinisaidia kwa mengi sana.
 
Last edited:
ASKOFU mkuu wa jimbo kuu la Mwanza, kanisa Katoliki Mhashamu Anthony Petro Mayalla (69) amefariki dunia leo mchana kutokana na maradhi ya moyo baada ya kuugua ghafla akiwa ofisini kwake.Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mkurungenzi wa mawasiliano wa baraza la Maaskofu (TEC) kanisa katoliki, Padri Revocatus.Makonge Askofu huyo amefariki baada ya madaktari wa Hospitali ya rufaa ya Bugando kuhangaika kumpatia matibabu bila ya mafanikio.

Alisema kuwa marehemu aliamuka salama leo na kuendelea na shughuli zake za kila siku ofisini kwake mpaka majira ya saa 4:00 asubuhi ambapo alizidiwa ghafla na kukimbizwa Hospitali ya rufaa ya Bugando.Habari kutoka katika ofisi ya aksofu huyo, zimeeleza kuwa alipatwa na maradhi hayo wakati akiwa katika maandalizi ya ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Vatican ambaye alikuwa akitarajiwa kufanya ziara jimboni kwake Oktoba 5 mwaka huu kwa ajili ya kufungua ujenzi wa hospitali ya watoto.“Baada ya kufikisha hospitalini hapo madaktari waliahangaika kuokoa maisha yake lakini nahati mbaya lifariki dunia majira ya saa 8;30 mchana,” alieleza Padri Revocatus Makonge.

Askofu Mayalla alizaliwa Aprili 23 mwaka 1940 katika katika kijiji cha Nera wilayani Kwimba na kupata elimu yake ya msingi katika wilaya hiyo na masomo ya sekondari.Askofu Mayalla alikuwa amehitimu shahada ya kwanza ya elimu aliyopita katika chuo kikuu cha Loyola huko Chicago Marekani mwaka 1973 hadi mwaka 1975.
Imetolewa na mwandishi wa habari hapa Mwanza.
 
We thank the Lord for the life of this good servant of His. He has run the good race, he has completed the journey. Now he has gone to the house of the Father. Our prayers accompany him there.
 

Kwa hiyo wewe ni Baba Padre?

RIP Bishop Antony Mayala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…