feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 6,803
- 12,667
Habari ya asubuhi waungwana.
Ukweli hii tabia ya hawa askari wa barabarani kuchukua rushwa imekithiri sana tena wanachukua wazi wazi na bila kuogopa.Leo asubuhi nimepanda daladala kutoka Rang 3 naelekea vingunguti nikawa nimekaa siti ya mbele kabisa,tumetoka kituo kikuu cha Rang 3 tunafika Kizuiani trafki akasimamisha dereva akafyonya "aah hawa jamaa washaanza asubuhi asubuhi kutaka hela akamwita konda wake jina oya Bonge mpelekee elfu mbili yake tuondoke" na kweli konda akafanya hivyo.
Gari ikaondoka tumefika Sokota ikasimamishwa tena na askari wa kike aliyekuepo pale kiwanda cha maji ya afya.Dereva "oya bonge shuka mwambie tushaunga uko nyuma" konda akaenda lakini akakawia ikabidi dereva nae ashuke akaenda akarudi na hasira "huyu dada njaa sana,sasa kila tukisimamishwa tutakua tunatoa hela" kuna mzee jirani yangu akamuuliza kwani gari inakosa gani? Dereva akajibu "unafikiri mzee gari inakosa yaani hawa trafki gari hata iwe mpya imetoka leo lazima uwape hela ukiwanyima njia utaihama watakavyokuandama kwahiyo imekua kama desturi,ngoja huku tunapoenda utakuta wengine watasimamisha na dau lao ni hilo hilo 2000-3000 kwa asubuhi".
Tulipofika buguruni sheli tukasimamishwa tena na matrafiki wa tatu wawili wanaume na mmoja wa kike kondakta akashuka tena kupeleka elfu 2,kitu cha ajabu wakisimamisha wala hawakagui gari wanazuga wanachukua chao kisha wanaondoka.
Jeshi la polisi usalama barabarani limeoza linahitaji kufumuliwa hii tabia imekithiri sana na sio mara moja kushuhudia,madereva na makonda wa daladala wengi hawana mshahara wanaamka mida mibaya kutafuta pesa lakini trafki badala kufanya kazi kwa ueledi wao wananyanyasa bila huruma wao wana mishahara na viposho lakini tamaa mbele.Na ninyi madereva na makondkta pia acheni unyonge na tabia hii ya kutoa hela hovyo hovyo hata kama huna kosa ni mnafuga ugonjwa,ukiwa na kosa kheri uandikiwe uichangie serikali kuliko kuwapa hao wafuga vigambi.
Ukweli hii tabia ya hawa askari wa barabarani kuchukua rushwa imekithiri sana tena wanachukua wazi wazi na bila kuogopa.Leo asubuhi nimepanda daladala kutoka Rang 3 naelekea vingunguti nikawa nimekaa siti ya mbele kabisa,tumetoka kituo kikuu cha Rang 3 tunafika Kizuiani trafki akasimamisha dereva akafyonya "aah hawa jamaa washaanza asubuhi asubuhi kutaka hela akamwita konda wake jina oya Bonge mpelekee elfu mbili yake tuondoke" na kweli konda akafanya hivyo.
Gari ikaondoka tumefika Sokota ikasimamishwa tena na askari wa kike aliyekuepo pale kiwanda cha maji ya afya.Dereva "oya bonge shuka mwambie tushaunga uko nyuma" konda akaenda lakini akakawia ikabidi dereva nae ashuke akaenda akarudi na hasira "huyu dada njaa sana,sasa kila tukisimamishwa tutakua tunatoa hela" kuna mzee jirani yangu akamuuliza kwani gari inakosa gani? Dereva akajibu "unafikiri mzee gari inakosa yaani hawa trafki gari hata iwe mpya imetoka leo lazima uwape hela ukiwanyima njia utaihama watakavyokuandama kwahiyo imekua kama desturi,ngoja huku tunapoenda utakuta wengine watasimamisha na dau lao ni hilo hilo 2000-3000 kwa asubuhi".
Tulipofika buguruni sheli tukasimamishwa tena na matrafiki wa tatu wawili wanaume na mmoja wa kike kondakta akashuka tena kupeleka elfu 2,kitu cha ajabu wakisimamisha wala hawakagui gari wanazuga wanachukua chao kisha wanaondoka.
Jeshi la polisi usalama barabarani limeoza linahitaji kufumuliwa hii tabia imekithiri sana na sio mara moja kushuhudia,madereva na makonda wa daladala wengi hawana mshahara wanaamka mida mibaya kutafuta pesa lakini trafki badala kufanya kazi kwa ueledi wao wananyanyasa bila huruma wao wana mishahara na viposho lakini tamaa mbele.Na ninyi madereva na makondkta pia acheni unyonge na tabia hii ya kutoa hela hovyo hovyo hata kama huna kosa ni mnafuga ugonjwa,ukiwa na kosa kheri uandikiwe uichangie serikali kuliko kuwapa hao wafuga vigambi.