Askari wapiga picha na viongozi wa CCM

Askari wapiga picha na viongozi wa CCM

Hao ni POLICCM kwa hiyo walichokifanya ni sawa tu. Hakuna hatua zozote zitakazo chukuliwa dhidi yao. Wangepiga picha na CDM ungeona viongozi wao wanavyotokwa mapovu mdomoni
Maafande wa doria wakipiga picha na baadhi ya viongozi wa CCM wa kata ya Mji Mpya morogoro.
_MG_3233.JPG


Hii kitu inaruhusiwa jamani??
 
Jamani tunashangaa nini? Hapo wanalinda usalama wa magamba. Akitokea hapo mwandishi wa habari ni risasi tu. Mmesahau ya Mwandishi wa Channel Ten alivyouawa katikati yao. Polisi ni lazima wakasalimiane na Mabwana zao, Magamba.
 
mleta uzi,cku nyingine ukitaka ueleweke vzr jaribu kutoa na maelezo basi,kuwa hapo walikuwa wapi? kwa sababu gani? nk..kuweka picha tu haitoshi,JF ina watu wa aina tofauti tofauti,si kila mtu ataielewa picha hii katika mtazamo ulio nao wewe,vinginevyo ufahamu wako ni mdogo sana kama unadhani hiyo picha inaweza kufananishwa na tukio la yule aliyedaiwa ni JWTZ kwa kutamka kwa mdomo wake yeye mwenyewe kuwa yupo tayari hata kufukuzwa kazi kwa ajili ya CHADEMA,na pia alionyesha ishara ya chama hicho,tofauti na hawa wanaoitwa POLICCM ulioweka picha yao ambayo hata haipo ki ushabiki wa kichama,Rejea picha zote mbili ya JWTZ na hii ya POLICCM naamini utatambua ufahamu wako unapoishia.
 
Tofauti na ile ya kwenu(chadema) ambayo lema alikumbatiana na askari fake wa JWTZ kwa mkao wa kujiandaa kabisa kwa kupiga picha! Hapo wanasalimiana kuwapa habari za kiintelejensia....kuwa kuna mtu kapita kavaa mavazi ya mgambo wakati wanajua hakuwahi kimbia mgambo!
hk /;0pjvbg

wewe ni kumbe ni full kilaza hilo ni pozi la salamu tu??? acheni unafiki na uzandiki samtym muwe mnachuja vya kuongea, askari kashika mkono huku akimtizama mpiga picha kusubiri afotolewe!!! Tunasubiri IGP Said Mwema atatoa agizo gani hapa.
 
huyu anasalimiana na kada wala hajaweka pozi la kishabiki, wa lema aliweka ushabiki zaidi, pia waswahili wa kale walisema Salamu haitii mimba...

Hivi mkuu, ile alama ya V ni alama ya chadema au ushindi?
Kama ni CDM, ina maana akina Che Guavara walikuwa wana chadema kabla hata ya CDM kuasisiwa?
Only in Tanzania!
 
Wachangiaji wengi wanachangi mambo bila kujua sherha za JWTZ asimuhusu askari polisi na za polisi hazimuhusu JWTZ Ingawa kuna mambo yanalingana. Askari hazuiliwi kuwasiliana wanajamii akiwa amevaa/kiraia mfano: mafuliko yametokea askari wameenda kufanya uokozi na viongozi wa kisiasa wako pale wakiwemo wa CDM watasalimiana nao kupeana ushauri wavae sare ama kiraia. Polisi maandamano na mikutano ya vyama vya siasa watakuwepo wakiwa wamevaa sare wanapofanya doria watawasiliana wanajamii bila kujali ni wa chama gani. Watumishi wote wa vyombo vya ulinzi na usalama, binafsi wanaruhusiwa kupiga kura na kuhudhuria mikutano ya kisiasa bila kuvaa sale ila hawaruhusiwi kuwemo kwenye maandamano na nieleweke nimesema binafsi. Pia wakiwa huko hawatakiwi kushabikia, kuhutubia kupiga picha na viomgo/wanachama wa vyama husika. Yule mtu mnaemwita kosa lake kupiga picha kwenye tukio la kisiasa akiwa amevaa sare za jeshi, pili kuonyesha ushabiki kwa kuonye ishara ambayo Cdm wanaitumia. Na baada ya kubainika kuwa sio askari wa JWTZ Kosa lake kwanza kuvaa sare za jeshi kinyume cha sheria inga hapa wengine mtase mbona nchi fulani raia wanavaa hatuongozwi sheria za huko. Kosa lingene kujifanya askari JWTZ kama kweli wanamapinduzi tunataka mabadiriko ya kweli tuache ushabiki tukosoe kila lisilohalali. Na tu coment mada kwa kujua unachochangia majeshi ya sheria zao na kunavitabu vya sheria, wanasheria na mahakama kule hazilingani hizi za kwetu.

Mkuu, unge-edit kidogo ili upate kueleweka vizuri.
Yawezekana wewe ni mwanajeshi, lakini sheria ya vyama vya siasa haitamki aina ya jeshi la TZ bali askari wote kwa ujumla wake hawaruhusiwi kushabikia chama chochote cha siasa full-stop.

Na kwamba ati V ni alama ya CDM ni utoto. V ni alama inayotumika duniani kote kumaanisha ushindi na ambayo CDM nao wanaitumia pia.
 
Technix za kuua vyama vingi hiyo, Nyerere kafa nani atarudisha Tena . Ila nimekubali wabongo hawachoki, L
na ndo kwanza wanaunda vingine vi3 vipya. Hata wakileta Kama ya Mwangosi hawaogopi?!!!!! Yule soja wa arusha akiona hii pict. lazima aandamane
 
Wachangiaji wengi wanachangi mambo bila kujua sheria za JWTZ asimuhusu askari polisi na za polisi hazimuhusu JWTZ Ingawa kuna mambo yanalingana. Askari hazuiliwi kuwasiliana wanajamii akiwa amevaa kijesh/kiraia mfano: mafuliko yametokea sehemu falani ya nchi, askari wameenda kufanya uokozi na viongozi wa kisiasa wako pale wakiwemo wa CDM hawakatazwi kuwasiliana nao kusalimiana na hata kwa kupeana mikono kupeana ushauri wavae sare ama kiraia. Polisi wanatakiwa kuwepo kwenye maandamano na mikutano ya vyama vya siasa wakiwa wamevaa sare na baadhi kiraia. wanapofanya doria watawasiliana wanajamii bila kujali ni wa chama gani ilimradi kwenye mkusanyi wa kisiasa. Watumishi wote wa vyombo vya ulinzi na usalama, binafsi wanaruhusiwa kupiga kura na kuhudhuria mikutano ya kisiasa bila kuvaa sale ila hawaruhusiwi kuwemo kwenye maandamano, na nieleweke nimesema binafsi. Pia wakiwa huko hawatakiwi kushabikia, kuhutubia kupiga picha na viongozi/wanachama wa vyama husika. Sasa tukifananisha yule mtu mnaemwita mwanajeshi wa lema yeye kosa lake kupiga picha kwenye tukio la kisiasa akiwa amevaa sare za jeshi, pili kuonyesha ushabiki kwa kuonye ishara ambayo Cdm wanaitumia. Na baada ya kubainika kuwa sio askari wa JWTZ Kosa lake kwanza kuvaa sare za jeshi kinyume cha sheria ingawa hapa wengine mtasema mbona nchi fulani raia wanavaa sare za jeshi hatuongozwi sheria za huko. Kosa lingene kujifanya askari JWTZ kama kweli wanamapinduzi tunataka mabadiriko ya kweli tuache ushabiki tukosoe kila lisilohalali kutendwa viongozi wenu wa vyama, na wanaojiita watetezi haki za binaadam wanayajua haya ndo maana wako kimya.
 
Wanawashukuru walikuwa wanawalindia madem zao
 
Mkuu, unge-edit kidogo ili upate kueleweka vizuri.
Yawezekana wewe ni mwanajeshi, lakini sheria ya vyama vya siasa haitamki aina ya jeshi la TZ bali askari wote kwa ujumla wake hawaruhusiwi kushabikia chama chochote cha siasa full-stop.

Na kwamba ati V ni alama ya CDM ni utoto. V ni alama inayotumika duniani kote kumaanisha ushindi na ambayo CDM nao wanaitumia pia.
nime editi mkuu. Kasome coment ya kwenye mada mama Saluma kikwete alipofananisha kupewe heshima kama rais utasema mi nafanyia kazi ofisi ya mkuu wilaya/mkoa mi naamini yule nikirudi kwenye mada jamaetu aliekula mvua nne hajaonewa amejitakia mwenye aidha kwa kutojua ama kwa makusudi, ndo maana unaona hakuna kiongozi, wa chama chochote cha kisiasa wala wanaharakati au wanasheria wanaonyesha kupinga hukumu ile au kuonyesha niakumkatia rufaa. Ili kumtetea, Ukweli ndo huo ingawa hamtaki ndo maana mmebaki kufananisha matukio tu.
 
Maafande wa doria wakipiga picha na baadhi ya viongozi wa CCM wa kata ya Mji Mpya morogoro.
_MG_3233.JPG


Hii kitu inaruhusiwa jamani??

hapa walikuwa wanasalimiana wewe ndo ukawapiga picha acha kupotosha sema utawapata wasiofikiria
 
Uchochezi tu huu, hapa haionyeshi kuwa wanapiga picha, walikuwa wanasalimiana tu
 
Hii mada tunatoka povu bure hii habari ni ya kutengenezwa ukweli wa habari hii nenda kwenye mada inayosomeka. Barua ya wazi kwa m/kiti chadema mbowe zimewekwa picha kama hii na maelezo yake. Mi naona hii nchi wanasiasa mmeja uongo tuu.
 
Back
Top Bottom