Askari Magereza Hii ni Aibu!

Kitendo walichokifanya Asikari kinadhihilisha wazi masikini / mnyonge siku zote hana Haki, kwani hata kama sheria zipo hulenga haki za wenye mabavu. Hivi furushi hili la utumwa kwa wasiojiweza litaisha lini?
 
Naamka asubuhi leo tarehe 19 April nakwenda kujinunulia gazeti langu la Mwananchi gazeti hili limepambwa na picha moja kubwa inayoonyesha askari wawili wakike na watatu wakiume wakiwa wamempiga Tanganyika jeki mama mmoja na chini kuna maandishi yanayosomeka: Mtuhumiwa chini ya ulinzi halafu chini yake kuna maneno yasemayo mwanamke akiwa amedhibitiwa na askari magereza wa mkoa wa Morogoro baada yakudaiwa kufanya fujo! sasa kinachonishangaza ni kuwa kweli askari watano kumshika mwanamke mmoja tu? askari wa bongo wanahitaji mafunzo ya ziada sasa.

Hivi kwani hata kama mtu anakosa ni lazima kumkwida kama walivyofanya hawa askari wetu? kwanza walikuwa wengi, tena hana silaha yoyote, huu ni uoga na kujilinda kusikokuwa na sababu
 
Msiongee msiyoyajua huenda yule mama alikuwa mbishi sana hata kama ningekuwa mm namionyesha kama mm ni kamanda
Pumbavu kabisa
 
Je askari magereza ana mamlaka ya kumuweka mtu chini ya ulinzi? Do they have the power to arrest.

Nadhani hawana mamlaka hayo, huyu mama anaweza kufungua kesi na kupata pochi ya kutakata. Sheria inawapa mamlaka ya delea na wafungwa tuu na si vinginevyo
"Chini ya Ulinzi" ni msemo wa wanajeshi nashangaa polisi na magereza wanautumia bila kuelewa maana yake.
 
Inawezekana mama alikuwa na matatizo makubwa, inawezekana asinge pigwa tanganyika jeki angeweza kuleta madhara kwa raia, usingeanza kuwalaumu askari bila kusoma kwa undani!
 
Back
Top Bottom