Asilimia 90 ya wahitimu vyuoni hawajawahi kusoma kitabu chochote cha elimu binafsi, ni professionals tu katika fani walizosomea ila hawajaelimika

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
Hapa sisemei kwamba mtu ana phd / masters / degree ya udaktari, uhandisi, uhasibu, Sheria, masoko, IT. La Hasha !! Hizi taaluma ni kipengere kidogo kwenye elimu, mtu alieelimika huwa kajenga mazoea ya kusoma vitabu nje ya taaluma vyenye maarifa yanayogusia maisha, jamii, kustarabika, kuwa mtu bora, n.k. unaweza kuwa na phd ya Uhandisi lakini kama husomi vitabu nje ya IT utaonekana hujaelimika kawenye mambo ya kawaida kabisa katika maisha nje ya taaluma, Mbaya zaidi kwa hapa kwetu mtu akimaliza shule hata hivyo vitabu vya taaluma havigusi tena labda aende tena chuoni ama iwe ni kwajili ya kufanyia kazi, hii inaonyesha wazi kabisa kusoma vitabu sio kwa kupenda.

Hapa Nchini wasomi wengi sana wanamaliza vyuo hawavijui vitabu muhimu kama how to talk to win friends and influence people, 40 laws of power, The art of war, Rich dad poor dad, n.k.

Hii imepelekea wahitimu wengi nchini kutumia nguvu kubwa kujitambulisha wamesoma vyuoni kwasababu katika hali ya kawaida vitu wanavyofanya na kuongea watu huwa na mashaka hasa hawa ambao wameishia darasa la sabab na form 4 ambao nao wameaminishwa mtu akifika chuoni anakua kaelimika hivyo wanachokiona kwa wahitimu kinatia mashaka.

Dalili za wasomi wetu kutokuelimika ni hizi

Upeo Mdogo wa Maarifa: Watu ambao hawajazoea kusoma vitabu wanaweza kuwa na maarifa kidogo au wamejikita zaidi katika maarifa ya utaalamu wao pekee, Mbongo ukimwambia akupe elimu yeye ataanza kumwaga vitu alivyosomea kwenye taaluma yake, na hapa wengi katika mazungumzo ya kawaida tu ama maisha nje ya taaluma zao huwa wanaumbuka, mtu mara ya mwisho kuongea point hadi ufikirie.

Kutokuwa na Uwezo wa Kujieleza Vyema: Kusoma vitabu kunaweza kuimarisha ustadi wa lugha na uwezo wa kujieleza vizuri kwa facts. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na changamoto katika kuwasiliana kwa ufasaha.

Kutokuwa na Ujuzi wa Kuchambua: Kusoma vitabu kunaweza kukuza uwezo wa kuchambua mawazo na kujenga hoja. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na shida katika kuchanganua mambo kwa undani.

Ugumu wa Kujifunza Vitu Vipya: Kusoma vitabu kunaweza kufundisha jinsi ya kujifunza vitu vipya na kutafsiri habari mpya. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na ugumu katika kujifunza mambo mapya hasa kwa hapa nchini ambako elimu imelenga zaidi kusoma kwa kulazimisha kukariri definitions.

Kutojua Kusoma Kwa Furaha: Watu wanaojifunza kupitia kusoma vitabu mara nyingi hufurahia mchakato huo na wanaweza kuwa na uwezo wa kusoma kwa kujitolea hata nje ya mahitaji ya kitaaluma, Kwa hapa Tanzania mtu mwenye masters unaweza kumpa kitabu anaishia page ya 10 imetoka hio, atatalalamika kitabu kirefu kinamchosha ama atakwambia ashamaliza shule usimchoshe na mavitabu.

Kutokuwa na Mawazo na Mtazamo Mpana: Kusoma vitabu kutoka nyanja mbalimbali kunaweza kuongeza ufahamu na mtazamo mpana. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kukosa ufahamu wa mambo mbalimbali.
 
Muda wa kula bata ni wa kupooza kichwa ili ujipange upya kwa msuli. Hivi unawajua ma lecturers wa vyuo wanavyoandaa mitihani kwa format ya kukomoana? utasoma vitabu vya maarifa binafsi lini?
Huko vyuoni mbona tumesoma vizuri tu, sioni ugumu labda kama umevamia sehemu iliyokuzidi uwezo, vyuo vya Tz vingi malecturer wanarudia maswali yale yale tu ya past papers za miaka tano nyuma, nao wamekaririshwa kutunga hivyo hivyo
 
Huo ndiyo ukweli wenyewe
Hapa Nchini wengi sana wakiwemo hawa maprofes wanamaliza vyuo maishani mwao hawajawahi kusoma kitabu chochote nje ya vile vya kukariri definition na advantages.

Na ndio maana kuna wahitimu wengi sana wanaonekana hawajaelimika kwasababu vitu wanavyofanya na kuongea havina mantiki, mtu unakuta kapata mafanikio kidogo tu anaanza vituko unaona wazi kabisa huyu kasome ujuzi tu ila hajaelimika,

Watu wengi wameelimika katika taaluma zao pekee lakini nje ya hapo hamna kitu

Upeo Mdogo wa Maarifa: Watu ambao hawajazoea kusoma vitabu wanaweza kuwa na maarifa kidogo au wamejikita zaidi katika maarifa ya utaalamu wao pekee.

Kutokuwa na Uwezo wa Kujieleza Vyema: Kusoma vitabu kunaweza kuimarisha ustadi wa lugha na uwezo wa kujieleza vizuri kwa facts. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na changamoto katika kuwasiliana kwa ufasaha.

Kutokuwa na Ujuzi wa Kuchambua: Kusoma vitabu kunaweza kukuza uwezo wa kuchambua mawazo na kujenga hoja. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na shida katika kuchanganua mambo kwa undani.

Ugumu wa Kujifunza Vitu Vipya: Kusoma vitabu kunaweza kufundisha jinsi ya kujifunza vitu vipya na kutafsiri habari mpya. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kuwa na ugumu katika kujifunza mambo mapya hasa kwa hapa nchini ambako elimu imelenga zaidi kusoma kwa kulazimisha kukariri definitions.

Kutojua Kusoma Kwa Furaha: Watu wanaojifunza kupitia kusoma vitabu mara nyingi hufurahia mchakato huo na wanaweza kuwa na uwezo wa kusoma kwa kujitolea hata nje ya mahitaji ya kitaaluma, Kwa hapa Tanzania mtu mwenye masters unaweza kumpa kitabu anaishia page ya 10 imetoka hio, akisoma basi ni kwa sifa ile ili aende hara mitandaoni ajisifie kasoma.

Kutokuwa na Mawazo na Mtazamo Mpana: Kusoma vitabu kutoka nyanja mbalimbali kunaweza kuongeza ufahamu na mtazamo mpana. Watu ambao hawajazoea kusoma wanaweza kukosa ufahamu wa mambo mbalimbali.
 
Hapa Nchini wengi sana wakiwemo hawa maprofes wanamaliza vyuo maishani mwao hawajawahi kusoma kitabu chochote nje ya vile vya kukariri definition na advantages.
Ndugu, una uhakika??? Au hapo kwenye maprofes ulimaanisha nini?? Kama ni Professor waombe radhi.

Sifahamu kiwango chako cha elimu, ila jaribu kwenda UDSM uliza mtu wa shahada ya uzamivu (P.H.D) kwa uchache anatakiwa andae kurasa ngapi (page) halafu awe amepitia rejea ngapi (reference).

Ukimaliza ulizia kwa professor yoyote halafu muulize yeye amechapisha machapisho mangapi huko duniani na ana vitabu vingapi.

Hivi vitu huwezi kufanya bila ya kusoma na kuelewa vitabu kwa undani.Hata ukidanganya vipi bado utakamatwa tu.Nenda UDSM kasome shahada ya uzamivu halafu utuambie mziki wake.

Punguza papara, mhemko na hisia unapotaka kuwasilisha jambo lako.

Penda kujifunza, kujielimisha na kudadisi.
 
Maprof vitabu wanasoma matumbo ndio yana waendesha ila madogo wanao hitimu na vidiploma na videgree uchwara vitabu hawasomi kabisa vichwani empty set.
 
Ndugu, una uhakika??? Au hapo kwenye maprofes ulimaanisha nini?? Kama ni Professor waombe radhi.

Sifahamu kiwango chako cha elimu, ila jaribu kwenda UDSM uliza mtu wa shahada ya uzamivu (P.H.D) kwa uchache anatakiwa aandae kurasa ngapi (page) halafu awe amepitia rejea ngapi (reference).

Ukimaliza ulizia kwa professor yoyote halafu muulize yeye amechapisha machapisho mangapi huko duniani na ana vitabu vingapi.

Hivi vitu huwezi kufanya bila ya kusoma na kuelewa vitabu kwa undani.Hata ukidanganya vipi bado utakamatwa tu.Nenda UDSM kasome shahada ya uzamivu halafu utuambie mziki wake.

Punguza papara, mhemko na hisia unapotaka kuwasilisha jambo lako.

Penda kujifunza, kujielimisha na kudadisi.
Wengi wana elimu ya taaluma walizosomea tu, ni weupe kwenye elimu nje ya taaluma walizosomea kwasababu hawasomi vitabu,
 
Ni kweli kaka,, ila chanzo unakijua??!
Vitabu havitatui changamoto za Coursework, UE, GPA... Ila pia upatikaji wa vitabu huku mikoani baada ya kuhitimu ni shda...
 
Ndugu, una uhakika??? Au hapo kwenye maprofes ulimaanisha nini?? Kama ni Professor waombe radhi.

Sifahamu kiwango chako cha elimu, ila jaribu kwenda UDSM uliza mtu wa shahada ya uzamivu (P.H.D) kwa uchache anatakiwa andae kurasa ngapi (page) halafu awe amepitia rejea ngapi (reference).

Ukimaliza ulizia kwa professor yoyote halafu muulize yeye amechapisha machapisho mangapi huko duniani na ana vitabu vingapi.

Hivi vitu huwezi kufanya bila ya kusoma na kuelewa vitabu kwa undani.Hata ukidanganya vipi bado utakamatwa tu.Nenda UDSM kasome shahada ya uzamivu halafu utuambie mziki wake.

Punguza papara, mhemko na hisia unapotaka kuwasilisha jambo lako.

Penda kujifunza, kujielimisha na kudadisi.

Hujamuelewa mleta mada,kasema wasomi wengi hawana maarifa nje ya mipaka ya elimu zao.
 
wasomi wengi hawana maarifa nje ya mipaka ya elimu zao.
Unaelewa nini maana ya msemo huu "Elimu ni bahari", wewe hapo unaweza kuimaliza bahari yote kwa kuogelea hata kama unajua kuogelea???


Wewe hapo kwa mfano maarifa uliyokuwa nayo wewe unahisi yanakutosha??? Unahisi utayamaliza maarifa yote ya dunia hii??? Usipoyapata unahisi litakuwa kosa lako au muda, mazingira na mipaka yake????
 
Ndugu, una uhakika??? Au hapo kwenye maprofes ulimaanisha nini?? Kama ni Professor waombe radhi.

Sifahamu kiwango chako cha elimu, ila jaribu kwenda UDSM uliza mtu wa shahada ya uzamivu (P.H.D) kwa uchache anatakiwa andae kurasa ngapi (page) halafu awe amepitia rejea ngapi (reference).

Ukimaliza ulizia kwa professor yoyote halafu muulize yeye amechapisha machapisho mangapi huko duniani na ana vitabu vingapi.

Hivi vitu huwezi kufanya bila ya kusoma na kuelewa vitabu kwa undani.Hata ukidanganya vipi bado utakamatwa tu.Nenda UDSM kasome shahada ya uzamivu halafu utuambie mziki wake.

Punguza papara, mhemko na hisia unapotaka kuwasilisha jambo lako.

Penda kujifunza, kujielimisha na kudadisi.
Huyu bwana, analeta uhuni hapa. Kasimuliwa hadithi za hivyo vijutabu basi anajiona mwamba kwamba kamaliza kila kitu.

Umekosea kuwaweka maprofesa kwenye kundi la wasiojisomea.

Angeliishia ngazi ya undergraduate, angesound right.

Analeta dharau.
 
Back
Top Bottom