Asilimia 67 ya watanzania wanatumia ARVs

Asilimia 67 ya watanzania wanatumia ARVs

Oya unaleta za wapi hizo? Asilimia 67 sio mchezo ujue, yaani katika watu wanne mmoja anao? Acha zako
Hesabu ni janga! Mmoja kati ya wanne ni 25%. 67% ni wawili kati ya watatu.....
 
Hizi takwimu sio za kweli kabisa, ujue 67% ni zaidi ya nusu ya raia wa Tanzania, kwa hiyo unataka kusema Tanzania ni Sodoma na Gomorah hatujafikia huko bhana ungesema 6.7% labda kidogo ningekuelewa, maana hata mimi niko miongoni mwa 67% mbona situmii ARV
 
Hizi takwimu sio za kweli kabisa, ujue 67% ni zaidi ya nusu ya raia wa Tanzania, kwa hiyo unataka kusema Tanzania ni Sodoma na Gomorah hatujafikia huko bhana ungesema 6.7% labda kidogo ningekuelewa, maana hata mimi niko miongoni mwa 67% mbona situmii ARV
Ni 67 % ya watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI ndiyo wanatumia dawa.
 
Waandishi wa habari kanjanja wanaandika vichwa vya habari kuuza gazeti bila kujali madhara yake.
Hawa hawa wakifungiwa humu humu kuna watu watawatetea.
 
Mwandishi wa habari hii hakutaka hata kutumia akili ya darasa la saba.

Prevalence ya ukimwi inatakiwa akokotoe kutoka watu 1.4 million aloyoandika wana maambukizi ya ukimwi.

Labda kama hiyo 67% ni idadi ya waathirika wanaotumia ARV.

Tumuombe Dr Abas atoe press kumuomba mwandishi akanushe uzushi wake la sivyo achukulie hatua kuandika habari ya uongo.

Hakuna nchi duniani wanaoumwa ukimwi wakafika 67% na haitatokea.
Magazeti kama haya hayafai hata kuchungulia. HIV prevalence rate sasa ni 5.8 percent
 
na sisi tukirudi TZ hyo asilimia itapungua eeh!! mimi situmii wala sina.
 
Waandishi wa kitz makajanja sana.

Gazeti kama hilo likipewa likizo ya miaka miwili kuna watu humu watalalamika kweli.

Hivi kweli 67% ya watz ni waathirika!!!!! Aisee huu ni uongo mchana wa saa 14:50
 
7b24db432f260ffb11ec55aeb48abcce.jpg
Upotoshaji wa kiwango cha juu.yaani ilivyo kaa hapa inavuta kununua gazeti hili sana.sijui mhariri alikuwa ameshalala
 
Back
Top Bottom