Heshima kwenu wakuuu,
Naandika hapa na maumivu ya moyo makubwa sana mke wangu kipenzi yuko Dar es salaam mimi niko mkoani.
Leo toka mchana mke wangu kanambia simu yake haina charge umeme umekatika lakini kitu cha kushangaza simu zake zote mbili zimezima kwa wakati mmoja toka huo mchana mpaka saizi.
Na kibaya zaidi anaishi Kinondoni kwa Manyanya na kila nikiulizia majirani naambiwa umeme upo toka asubuhi na nimetuma mtu mpaka hapo nyumbani kuna umeme.
Kibaya zaidi nimeingia kwa page yake Fb nimekuta mwanamke anamshambulia mke wangu kuwa aachane na bwana wake.
Iam passing through hell right now na bado simpati mke kwa simu.Maumivu niliyonayo is only God knows.
Pole sana ndugu yangu kwa yalikukuta lakini naomba ukisome kisa hiki kina mafundisho makubwa ndani yake:
Kijana mmoja ambaye alikuwa na mapenzi makubwa sana kwa mkewe kiasi kwamba hata anapokuwa mbalinaye anahisi wanaume wengine wanamtongoza mke wake, siku moja alihisi kusalitiwa na mke wake kipenzi baadaya kuona mabadiliko ya kitabia kutokakwa mke wake huyo.alishindwa kuvumilia ikabidi amwambie mzamzi wake yaani baba yake juu ya tabia ya mkewe, naye baba akamwambia mwanawe asiwe anamfatilia sana mkewe kwani atapata shida sana,kina mama ndivyo walivyo.
Kijana akaona ushauri wa baba hautoshi akaendelea kufanya uchunguzi yaani kumfatilia sana mkewe,akabaini mkewe anaendelea kumsaliti, hali ile ikamfanya kijana akose raha maishani mwake, akawa anapungua mwili siku hadi siku kwa sababu ya kuwaza juu ya mkewe kipenzi. mwisho mzee akaona sasa anaweza kumpoteza kijana wake ikabidi achukue hatua za kunusuru maisha ya mwanawe,akamwambia mwanawe kwamba itabidi aitishe kikao cha familia ili kujadili juu ya jambo hilo, ila akamwambia mwanawe asichangie chochote katika kikao hicho.
Mzee akawaalika ndugu wa pande zote mbili kwa maana ya kikeni na kiumeni , kwa hiyo pale palikuwa na mashangazi,kina dada,mama wadogo na mama mkwe, na ndugu wengine wa kiume toka pande zote,baada ya kukusanyika mzee akawaambia kuwa, yeye amewaita kuzungumzia juu ya hali ya mtoto wake, hali yake inazidi kuwa mbaya siku hadi siku, anaumwa na yeye amejitahidi kumtibia kwa njia za HOSPITAL bila kupata nafuu yoyote.Lakini wamekwenda kwa mganga wa tiba za asili ambaye yeye amegundua tatizo la mtoto wake na ametoa dawa ambazo zina masharti kidogo magumu ndio maana ikabidi aombe ushauri kutoka kwa wanafamilia wote.
Sasa kila mmoja akawa na shauku ya kujua masharti gani waliyopewa na ndipo palipo na fundisho ndugu yangu:mzee akasema hapa tumepewa dawa ambayo kijana wangu anatakiwa kuitumia,lakini masharti ya dawa hii ni kuwa lazima anyweshwe na mwanamke aliyeolewa na ambaye HAJAWAHI KUTOKA NJE YA NDOA YAKE,kwa hiyo yoyote atakayedanganya kuwa yeye hajatoka nje ya ndoa na kasha akampa dawa hii mwanangu wote wawili watapoteza maisha.kwa kweli hapa palikuwa pagumu, kina mama mmoja baada ya mwingine wakaanza kutoka nje, hata mama yake mzazi, mama mkwe wake pamoja na mkewe wote walitoka nje, wanawake wote walishindwa masharti yale.
Baadae mzee akamwita mwanawe akamwambia umejifunza jambo gani katika kikao hiki? mtoto akasema wanawake kutoka nje ya ndoa ni jambo lisiloepukika kwa sababu ni mapungufu waliyoumbiwa, hivyo hupaswi kushindwa kufanya kazi zako kwa sababu hiyo, bali tambua kwamba ni jambo linalowezatokea katika ndoa yako tena kwa asilimia kubwa sana,nawe ndugu yangu kama uko njeya nyumbani kikazi, fanya kazi za watu vizuri, tafuta namna ya kumrekebisha mkeo lakini kama utakuwa na ushahidi wa kutosha juu ya jambo hilo na sio hisia. pole sana ndio Dunia ilivyo.