mitale na midimu
JF-Expert Member
- Aug 26, 2015
- 10,420
- 17,701
Kuna mambo manne ambayo Yanapatikana duniani kote kwa asilimia kubwa kabla hata hatujaingiliana (globarization)
1:Watu kuabudu wafu katika desturi zao.
Desturi hii utaikuta utaikuta australia, japan, afrika yote, India,
America Yote, Ulaya, na kila mahala. Hii inaonyesha ufanano huu ambao hauwezi kutokea kwa kuibuka ''Evolve" ni ushahid tosha Kuna siku moja mahali flani watu wote walikuwa wanaishi sehemu moja.
Ibada hizi nyingi, zinapatikana siku hizi hadi katika baadhi ya imani za kikristo,baadhi ya waislam, wabudha.
2; Sikukuu za kumbukumbu za wafu.
Bibilia inasema Safina Ilituama juu ya mlima hararati tarehe ya kumi na saba ya mwezi wa kwanza.
Kwa Kalenda mpya ya kiebrania iliyoanza kuanzia walipotoka misri tarehe hiyo inaanguka mwanzoni mwa mwezi wa tisa.
Tarehe hii au karibu na hii inasherekewa
Peru,kwa wahindu,Mexico, Wakazi wa kaskazini wa visiwa vya pacific, wa australia wa asili, Waajemi na wamisri wa zamani waliisherekea, Mataifa ya kaskazini mwa ulaya, Warumi wa zamani na kwingineko. Baadhi ya wakristo wanasherehe zinazogongana na tarehe hiyohiyo katika kuadhimisha vifo vya watu wao wakidini.
3: uwepo kwa Stori za watu kuokolewa kupitia meli/mtumbwi na aina ya stori zinazoendana na ile ya Nuhu.
uwepo wa stori kuhusu kuwahi kutokea mafuriko na watu kuokolewa kwa njia ya kitu kama mtumbwi upo katika zaidi ya tamaduni 150 duniani kote.
Stori hizi zimekuwepo hata kabla mambo ya imani za kikristo na kiislam kuwepo. Hii ni ushahidi kwamba kuna siku moja watu walikuwa pamoja, wakatawanyika na hiki tunachokiona ni mwangwi wa kile ambacho waliwahi kukiamini wakati wako pamoja. Na mababu wa mababu wao ni wale waliotawanywa pale babeli kwenye mnara.
4: KUABUDU JUA
Ibada za Kuabudu jua,miezi, miandamo ya miezi, nyote na viumbe pia ilianzia huko huko babeli.
Iliaminika wakuu wao wakina Nimrod walikufa walipaa kwenda mwezini, juani na huko angani.
Ibada hii inasura ya kidunia na utaikuta kila kona ya Dunia mfano.
*Misri ya Zamani - Ra, Osiris etc
*Kaanani - Baal, Shamas, Adoni etc
*Syria - Tammuz, Elagabalas
*Umedi na uajemi - Ormuz na Mithra
Wahindi - Mitra
Wagiriki - Apollo, Adonis na Hercules
HISTORIA YA UCHAWI/IBADA YA WAFU/ NA TAMADUNI ZOTE ULIMWENGUNI ZINATURUDISHA PALEPALE BABELI.
Kwa Mujibu wa Vyanzo mbalimbali vya kihistoria,
Vinakubaliana na inachokisema Bibilia kuwa Ustaarabu wa mwanadamu ulianzia pale katika Bonde la SHINARI.
1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.
" Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko...9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote. ''
Mwanzo 11:2,3,9
Wababeli hawa waliambatana na Ibada ya wafu, ndugu zao waliokufa katika Ile Gharika. Lakini Pia waliianzisha sherehe hiyo ya wafu wao siku ambapo Safina Ilitua juu ya mlima hararati.
Hivyo baada ya Kutawanywa sio jambo la ajabu kukuta desturi hizo zikiendelea kila kona. Hapo ndio chanzo cha uchawi wote na tamaduni zote zakijadi duniani hadi huu Kwetu Tanzania.
Ustaarabu wa Dunia Ulianzia babeli kwa wakaldayo, Ukaenda Misri, wagiriki wakautoa misri na kuuingiza Ulaya. Warumi wakauchukua kutoka kwa Wagiriki. Na ustaarabu huo mwingii ukatapakaa tena dunia hii ya kisasa kutokea ulaya. Lakin kabla miaka mingi iliyopita Siku ambayo wanadamu walitawanywa na kuchafuliwa Lugha dunia nzima baada ya gharika walizisambaza katika asili na tamaduni zote duniani.
Miungu Ya Babeli ambayo ilikuwa na Utatu wao Mtakatifu yaani BABA,MAMA, na Mwana (Nimrod, semiramis na Tammuz) Imetapakaa dunia nzima kwa majina tofauti tofauti. Na miungu hii yote iliwahi kuwa watu halisi siku za nyuma kabla hawajafanywa miungu.
Mfano, Mwanahistoria Prutaech anasema makuhani wa kimisri waliwafundisha kuwa hao miungu yaani Osiris, Horus na Volcan walikuwa watu halisi huko nyuma.
Alexander The great aliwahi kumuandikia barua mama yake mzazi akimwambia miungu yao Saturn, Jupiter, Juno, wote walikuwa watu halisi kama alivyoambiwa na kuhani mkuu wa miungu ya kimisri Leo alipokuwa akifundishwa siri za miungu. Miungu hii inauwezo wa Kutokea watu na kuwapa maelekezo ya Kiungu.
Mwisho;
Hakuna jipya chini ya jua. Miungu na taratibu nyingi za kipagani dunia ya sasa bila kujali ni ya kisasa kiasi au imeingizwa kwenye dini kwa kificho kiasi gani chanzo chake ni Babeli, Zikaingia Misri, na Kuingizwa Ulaya na Wagiriki kisha kusambaa dunia yote ya kisasa. Ila dunia ya Kale ilisambaa kupitia Machafuko ya Lugha pale mnara.
Hii ndiyo sababu Kitabu cha UFunuo kwa mafumbo kinaifananisha hali ya dunia ya siku za mwisho na Babeli ile ya zamani na upagani wake.
Anawaita wanadamu Wote watoke katika mifumo ya kiibada inayoelekezwa kwa wafu, Jua, miezi, Ushetani na kila aina ya mfumo wa maisha usiompendeza.
Ufunuo 18:1Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.
2 Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;
3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.
1:Watu kuabudu wafu katika desturi zao.
Desturi hii utaikuta utaikuta australia, japan, afrika yote, India,
America Yote, Ulaya, na kila mahala. Hii inaonyesha ufanano huu ambao hauwezi kutokea kwa kuibuka ''Evolve" ni ushahid tosha Kuna siku moja mahali flani watu wote walikuwa wanaishi sehemu moja.
Ibada hizi nyingi, zinapatikana siku hizi hadi katika baadhi ya imani za kikristo,baadhi ya waislam, wabudha.
2; Sikukuu za kumbukumbu za wafu.
Bibilia inasema Safina Ilituama juu ya mlima hararati tarehe ya kumi na saba ya mwezi wa kwanza.
Kwa Kalenda mpya ya kiebrania iliyoanza kuanzia walipotoka misri tarehe hiyo inaanguka mwanzoni mwa mwezi wa tisa.
Tarehe hii au karibu na hii inasherekewa
Peru,kwa wahindu,Mexico, Wakazi wa kaskazini wa visiwa vya pacific, wa australia wa asili, Waajemi na wamisri wa zamani waliisherekea, Mataifa ya kaskazini mwa ulaya, Warumi wa zamani na kwingineko. Baadhi ya wakristo wanasherehe zinazogongana na tarehe hiyohiyo katika kuadhimisha vifo vya watu wao wakidini.
3: uwepo kwa Stori za watu kuokolewa kupitia meli/mtumbwi na aina ya stori zinazoendana na ile ya Nuhu.
uwepo wa stori kuhusu kuwahi kutokea mafuriko na watu kuokolewa kwa njia ya kitu kama mtumbwi upo katika zaidi ya tamaduni 150 duniani kote.
Stori hizi zimekuwepo hata kabla mambo ya imani za kikristo na kiislam kuwepo. Hii ni ushahidi kwamba kuna siku moja watu walikuwa pamoja, wakatawanyika na hiki tunachokiona ni mwangwi wa kile ambacho waliwahi kukiamini wakati wako pamoja. Na mababu wa mababu wao ni wale waliotawanywa pale babeli kwenye mnara.
4: KUABUDU JUA
Ibada za Kuabudu jua,miezi, miandamo ya miezi, nyote na viumbe pia ilianzia huko huko babeli.
Iliaminika wakuu wao wakina Nimrod walikufa walipaa kwenda mwezini, juani na huko angani.
Ibada hii inasura ya kidunia na utaikuta kila kona ya Dunia mfano.
*Misri ya Zamani - Ra, Osiris etc
*Kaanani - Baal, Shamas, Adoni etc
*Syria - Tammuz, Elagabalas
*Umedi na uajemi - Ormuz na Mithra
Wahindi - Mitra
Wagiriki - Apollo, Adonis na Hercules
HISTORIA YA UCHAWI/IBADA YA WAFU/ NA TAMADUNI ZOTE ULIMWENGUNI ZINATURUDISHA PALEPALE BABELI.
Kwa Mujibu wa Vyanzo mbalimbali vya kihistoria,
Vinakubaliana na inachokisema Bibilia kuwa Ustaarabu wa mwanadamu ulianzia pale katika Bonde la SHINARI.
1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.
" Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko...9 Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote. ''
Mwanzo 11:2,3,9
Wababeli hawa waliambatana na Ibada ya wafu, ndugu zao waliokufa katika Ile Gharika. Lakini Pia waliianzisha sherehe hiyo ya wafu wao siku ambapo Safina Ilitua juu ya mlima hararati.
Hivyo baada ya Kutawanywa sio jambo la ajabu kukuta desturi hizo zikiendelea kila kona. Hapo ndio chanzo cha uchawi wote na tamaduni zote zakijadi duniani hadi huu Kwetu Tanzania.
Ustaarabu wa Dunia Ulianzia babeli kwa wakaldayo, Ukaenda Misri, wagiriki wakautoa misri na kuuingiza Ulaya. Warumi wakauchukua kutoka kwa Wagiriki. Na ustaarabu huo mwingii ukatapakaa tena dunia hii ya kisasa kutokea ulaya. Lakin kabla miaka mingi iliyopita Siku ambayo wanadamu walitawanywa na kuchafuliwa Lugha dunia nzima baada ya gharika walizisambaza katika asili na tamaduni zote duniani.
Miungu Ya Babeli ambayo ilikuwa na Utatu wao Mtakatifu yaani BABA,MAMA, na Mwana (Nimrod, semiramis na Tammuz) Imetapakaa dunia nzima kwa majina tofauti tofauti. Na miungu hii yote iliwahi kuwa watu halisi siku za nyuma kabla hawajafanywa miungu.
Mfano, Mwanahistoria Prutaech anasema makuhani wa kimisri waliwafundisha kuwa hao miungu yaani Osiris, Horus na Volcan walikuwa watu halisi huko nyuma.
Alexander The great aliwahi kumuandikia barua mama yake mzazi akimwambia miungu yao Saturn, Jupiter, Juno, wote walikuwa watu halisi kama alivyoambiwa na kuhani mkuu wa miungu ya kimisri Leo alipokuwa akifundishwa siri za miungu. Miungu hii inauwezo wa Kutokea watu na kuwapa maelekezo ya Kiungu.
Mwisho;
Hakuna jipya chini ya jua. Miungu na taratibu nyingi za kipagani dunia ya sasa bila kujali ni ya kisasa kiasi au imeingizwa kwenye dini kwa kificho kiasi gani chanzo chake ni Babeli, Zikaingia Misri, na Kuingizwa Ulaya na Wagiriki kisha kusambaa dunia yote ya kisasa. Ila dunia ya Kale ilisambaa kupitia Machafuko ya Lugha pale mnara.
Hii ndiyo sababu Kitabu cha UFunuo kwa mafumbo kinaifananisha hali ya dunia ya siku za mwisho na Babeli ile ya zamani na upagani wake.
Anawaita wanadamu Wote watoke katika mifumo ya kiibada inayoelekezwa kwa wafu, Jua, miezi, Ushetani na kila aina ya mfumo wa maisha usiompendeza.
Ufunuo 18:1Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.
2 Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;
3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.