Ng'wanapagi
JF-Expert Member
- Sep 18, 2013
- 9,125
- 8,627
Niliamua kukaa siku mbili bila kibali cha Makonda Dar es Salaam. Nilifanya vile kwani nilikokuwa nimezamia nilikutana na Wabongo kibao wengine wakaniomba nifikishe zawadi ana kwa ana kwa ndugu zao pia niliona bora nipite mitaa ya narung'ombe kwani ndiyo mitaa nilipoanza kiduka cha vifaa vya umeme mzigo wa kwanza nilichukulia mitaa hiyo. Siku ya kwanza ya mapumziko niliamua kuwatafuta marafiki zangu wa FB walioko Dar na nilikutana na wawili na nashukru walikuwa wadada wema na wanaojiheshimu. Baadae niliamua kukabidhi dhawadi nilizopewa huko ng'ambo ndipo kati ya hao watu aliniambia nimsubiri Sinza. Nilisubiri baadae niliamua kwenda kwenye ofisi za ACACIA kumuona ngosha mwezangu ambaye aliniomba nisikose kumuona kabla ya kwenda Usukumani. Nilionana nae ofisini kwake karibia na sheli ya mafuta iitwayo Victoria na baadae nikarudi Sinza na kumsubiri mwenyeji wangu nimkabidhi zawadi zake then nisonge Mwanza. Basi nikiwa hapo nikamuuliza dreva tax ni wapi tapata chakula kizuri hasa ugali, akaniambia ni hapo Sinza Makaburini sehemu inaitwa Fast Food. walikuja polisi watatu na kati ya hao mmoja nilimfahamu kwani alikuwa mpakani Mtukula na nilimfahamu kipindi naenda kufuata vipodozi Kampala ndipo nikawaambia waagize chakula nilipe!! Jamani bill ilipoletwa nilitamani kupitia mlango wa chooni. Niliuliza pembeni mbali na hao maafande ili wasisikie kulikoni hii bill imekuwa kubwa hivi wakati chakula nichakawaida tu(80,000/=)? Wakanijibu ni bei ya kuku mzima wa kienyeji na vingine!! Ukweli ni kwamba walileta kuku nusu na nikawauliza kama kuku ni yote leteni hapa firigisi mhudumu akasema firigisi huwa zinabaki machinjioni!! Kweli kupatwa si kwa jua tu hata kwa binadamu pia.