Asanteni sana Wabunge wa CCM!

Asanteni sana Wabunge wa CCM!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Najitokeza asubuhi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Wabunge wote wa CCM(wakiwemo pia Mawaziri,Manaibu Mawaziri,Spika,Naibu Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali).Mnafanya kazi ya 'kutukuka'.

Mnauonesha umma wa Tanzania jinsi ulivyofanya makosa kuwachagua kwa wingi wenu katika uchaguzi Mkuu wa 2010 na kupelekea wengine kuteuliwa au kuchaguliwa katika vyeo mlivyonavyo. Mnafanya kazi ya kudharau,kukejeli,kuzomea na kuharibu hoja yoyote ya Mbunge yeyote wa upinzani kwa maslahi hasa ya chama kuliko hata ya watanzania. Mnastahili sifa!

Mpo mnaoongoza kuomba miongozo ya kukandamiza hoja au kauli za wapinzani-hasa Mheshimiwa William Lukuvi,kwa kulinda Serikali na chama. Mnatekeleza kimatendo tulichowachagulia kwacho:ni kuhakikisha kuwa wapinzani hawafurukuti na CCM inatamba iwezavyo Bungeni huku TBC1 na/au Stae TV ikiwaonesha moja kwa moja. Raha ilioje!

Kuongea kwenu ni rahisi sana.Kila mnachosema hasa kinachosambaratisha hoja ya wapinzani hupigiwa meza na makofi mengi kwa kushangilia 'pointi' mnazozungumza. Chama kwanza,wananchi baadaye!

Ipo siku baadhi yenu au wote mtakuwa watazamaji wa Bunge kama sisi-tena si mbali ni 2015. Mtaona jinsi Bunge linavyopaswa kuwa. Msisahau kujikumbusha 'clips' zenu hizi ili mlinganishe na hilo Bunge jipya. Msisahau!

Hivi ni kweli kuwa tumewachagua nyinyi Wabunge kwa mamia kwenda Bungeni kufanya hivi? Mwigulu Nchemba alipoichana hadharani Bajeti Mbadala ya Upinzani iliyowasilishwa na Zitto Z. Kabwe,nyinyi mlishangilia sana. Juzi,Tundu A.M.Lissu aliipinga hoja binafsi ya Hamis Kigwangalla,tena kwa maneno matupu,ikawa nongwa.

Kigwangalla akatafutiwa nafasi ya kujibu mapigo. Muda wake wa kujibu hoja za Wabunge juu ya hoja yake akautumia kumshambulia moja kwa moja Tundu Lissu huku akisindikizwa na makofi na vigeregere.

Ipo siku mtajua kuwa hakuna katika nchi hii mwenye Jimbo wala cheo cha kudumu-si mbali,ni 2015. Mtajua kuwa hata asiye na pesa aweza kuwa Mbunge na kuboresha zaidi hoja zake kuliko nyinyi wenye pesa mnavyofanya. Mtajua kuwa sasa watanzania wanafuatilia kwa makini Wabunge wao na hoja zao. Mtafikia kuzilaumu luninga zinazowaonesha 'live' sasa. Siku inakuja!

Itafikia wakati,tena ni 2015, ambapo watanzania hawatajali fedha,vitisho,uzoefu,propaganda wala nini sijui ila uongozi imara kwa maendeleo ya Taifa hili. Hawatachagua tena wapiga makofi ila wajenga hoja.

Mna heri Wabunge wa CCM kwa kuturahisishia kazi ya kuchagua vyema 2015!
 
Hata wakisoma hii miaka 3 hawaelewi...
We jipange kwa 2015 tu.
 
Mkuu wabarikie sana, na waishi muda mwingi wajionee wenyewe.
 
I hate politics, I hate politicians, I hate.......... I dont know!
 
Wamevimbiwa posho hao 2015 inakuja watakiona cha moto
 
Ccm wanajivunia rushwa ya chumvi, kanga na vikofia vya kijani wakati wa uchaguzi!! Si ajabu kwamba watanzania wakairudisha madarakani tena ccm pamoja na uozo wote huo!!! Bado tuna safari ndefu!!!!!!
 
Sina la kuongeza kaka nadhani kama kweli wabunge wa ccm si mambumbumbu basi wananchi wataamua tu ifikapo 2015.kazi imekua rahisi kwa upumbavu huo ulioonyeshwa jana hatuwezi.nasema hatuwezi.mungu yupo ngoja tuone hapo 2015.
 
R.I.P ccm, tulikupenda lakini mafisadi na shetani wamekupenda zaid.
 
..'Siku yako Ipo MwanaGutu nimekuwekea,
Utapogeuka Upepo Usije Kuliaa...!'



...Aliimba Dada yangu Mmoja wa Tanga kwenye Taarab ya Kweli ya Enzi zile. Namuunga Mkono.
 
Wazungu wanasema hivyo VIOJA wanavyofanya CCM kwa Watanzania IS A BLESSING IN DISGUISE.
Sisi waswahili tunasema kwamba SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA. Hata uwaambie vipi CCM ni sikio la KUFA.

Nitashangaa sana kama CCM itapata MBUNGE hata MOJA Dar es Salaam kutokana na kuzima hii KERO kubwa ya Maji tunayoipata sisi wakaazi wa Dar es salaam. Au Kama CCM itapa MBUNGE hata moja Mtwara kutoka na kutaka kupoka raslimali ya gesi ya Mtwara bila kuwanufaisha wana WanaMtwara.

But gosh, give me a break, Tanzanians have very short memory and CCM knows this very well. 2015 WanaDar es Salaam na Mtwara watakuwa wamesahau haya madhila yote ya CCM, hasa watakapopewa vitenge, kofia, T-shirts, chumvi, sabuni na kusindikizwa na ahadi hewa.

Ukombozi wa kweli wa nchi uko kwenye ELIMU, bila elimu ya URAIA we are doomed. Wana Dar es Salaam ndiyo tunawaangusha Watanzania. Soma historia za nchi mbalimbali chachu za mabadiliko kiini chake huwa ni CAPITAL CITY. Lakini Dar es Salaam Capital City ya Bongo ambapo >90% wako informed na UBAYA WA CCM, sisi ndiyo kwanza tunachagua WABUNGE wa CCM na kumumpatia kura za kishindo mgombea urais wa CCM. Believe me kama Capital City ya Tanzania ingekuwa aidha Mbeya, Arusha au Mwanza, there is no question about that CCM 2015 ingezikwa tena BAHARINI kama Osama Bin Laiden!
 
Iko siku kila ambalo wanafikiri halipo litakuwepo, lile wanalofikiri alitatokea litatokea.
 
Back
Top Bottom