Asante sana Ngeleja

Asante sana Ngeleja

Celine Joseph

Member
Joined
Dec 12, 2014
Posts
6
Reaction score
6
NJOMBE, MBINGA ASANTE NGELEJA KWA KUTUTOA GIZANI

Juzi wakati wawakilishi wa gazeti letu walipotembelea maeneo ya Njombe na Mbinga wakihoji kuhusu namna umeme ulivyovifikia vijiji vingi katika maeneo hayo walikutana na maneno mengi sana lakini mengi yalikuwa na maneno ya shukrani kwa aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini mh.Willium Mganga Ngeleja, watu hawa walio wengi kwa idadi walisikika wakisema maneno " ASANTE NGELEJA KWA KUTUJALI, ISINGEKUWA WEWE LEO TUNGEKUWA GIZANI" kauli hii ilinishangaza sana na ilinibidi kuwahoji kwanini hasa wanamtaja Ngeleja kama wakushukuriwa na si Mh.Rais au hata Waziri wa Nishati na Madini wa sasa.

Wakazi hawa wa Njombe na Mbinga walisema kama sio Ngeleja na ubunifu wake leo hii tungekuwa gizani, wakaendelea yaani kama sio umeme wa wakala wa umeme vijijini REA, kitu ambacho Ngeleja alikianzisha kama mkombozi wa sisi watu tuishio vijijini leo tungekuwa gizani na hata nyuma kimaendeleo. " Tunamshukuru sana Ngeleja kwa kuianzisha REA na kuhakikisha sisi huku kijijini tunapata umeme kwa ajili ya maendeleo zaidi".

Wananchi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kusema kuwa viongozi wengi wamekuwa na upendeleo kwa maeneo wanapotoka hasa wanapopata nyadhifa kubwa kama aliyokuwa nayo Ngeleja lakini kwa huyu baba wa watu Ngeleja ni tofauti kabisa yaani ameacha huko kwao usukumani akatukumbuka wahehe na wabena na sisi wangoni pamoja na Wamatengo na hata ndugu zetu kule Nyasa, huyu ni mtu wa watu anajali sana watu na ana huruma sana kwani anatambua utu wa watu ni kiongozi mzuri sana hana upendeleo yaani huyu ni tofauti kabisa.

Wakazi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kulalmika na kuonesha kusononeka sana kwani wanadai hawakufurahishwa na kitendo cha maneno watu waliyokuwa wanamrushia na kumpakazia enzi za uongozi wake mpaka kumpelekea kujiuzulu mwaka 2012 mwezi May, wanadai kujiuzulu kwa Ngeleja kulikwamisha mambo mengi sana ikiwemo mipango mingi iliyokuwa mezani kwa ajili ya kuhakikisha vijiji vingi nchini vinapata umeme na kuvihakikishia maendeleo katika nyanja tofauti tofauti.

Wanaendelea kusema kuwa sisi umeme tuliletewa na tuliunganisha kwa bei rahisi sana yaan elfu 27 tuu, zamani ilikuwa mpaka laki saba lakini yule Msukuma wa watu akapambana mpaka ikashuka kiasi hicho eti bado watu wanasema hajui kuongoza sijui wanataka wafanyiwe nini ili waone mtu anafanya kazi, wanadai kama sio Ngeleja maisha yao kule vijijini yangekuwa ya giza sana na kusingekuwa na maendeleo kamwe.

Wanadai kuwa si huyu huyu Ngeleja aliepambana kuhakikisha swala la mgawo wa umeme nchini linapungua, au watu wamesahau kuwa Ngeleja ndiye aliyebuni mradi wa kuiunganisha mikoa yote ya Tanzania kwenye grid ya taifa kupitia miradi ya North-West Grid (kutokea Shinyanga,Geita,Kigoma,Katavi, Rukwa hadi Mbeya), Makambako-Songea na ule wa kuimarisha huduma ya umeme kupitia North-East Grid (kutokea Dares salaam hadi Kilimanjaro). lakini bado watu wanasema sio kiongozi mzuri walitaka awabebe mgongoni.. Kijana wa watu anafanya kazi kubwa sana na alitusaidia na daima tutashirikiana nae na kumkumbuka kwa safari yoyote atakayoianzisha.

Niliendelea kuwahoji na niliwadokeza kuwa kuna tetesi kuwa Ngeleja atagombea uraisi mwakani yaan hapa mpaka vilugha vyao vilizungumzwa waliaikika wahehe wakisema " Uwii, Inguluvi imlete munu huyu, tuisakumunu huyu ache kwa wewe" wakimaanisha "Mungu amlete mtu huyu,tunamuhitaji kwa ukombozi wetu" maneno haya yaliambatana na furaha kubwa iloyonishtua sana kwani sikitegemea wangelipokea swala hilo kwa furaha na shangwe kubwa wanasema watampitisha kwa hali na mali ili aendelee kuwatetea wao na watanzania kwa ujumla.

Walisema kwa walio tangaza nia mpaka sasa hakuna anayefaa kuwa raisi labda kama Ngeleja akigombea kama ndugu mwandishi ulivyotudokeza hapo, walilaumu kuwa mbona kama anataka kugombea uraisi yupo kimya mpaka sasa ? Mimi nilikosa cha kuwajibu na niliwaambia sijui anatafakari nini lakini nadhani kugombea uraisi ni moja ya fikra kubwa alizo nazo, waliomba kutembelewa na Mh. Ngeleja na mimi bila hajizi kwa sababu ya kazi yangu ya uandishi namba za viongozi huwa ninazo niliitafuta ilipokuwa namba ya Ngeleja na nilimpigia nikamwambia kuhusu kuwatembelea watu wa Njombe na Mbinga na yeye aliitika na kuwaahidi kuwa atapanga siku akawatembelee wazungumze vizuri na kujua wanaendeleaje, watu hawa walifarijika sana na kuendelea kuwa na imani kubwa na mh.Ngeleja na wamesema wanamuandalia zawadi kubwa mnoo kama shukrani...

Tunashukuru ndg mwandishi kwa kututembelea na Mungu akubariki sana popote ulipo, Mungu ibariki Njombe na Mbinga, Mungu ibariki Tanzania.A
 
NJOMBE, MBINGA ASANTE NGELEJA KWA KUTUTOA GIZANI

Juzi wakati wawakilishi wa gazeti letu walipotembelea maeneo ya Njombe na Mbinga wakihoji kuhusu namna umeme ulivyovifikia vijiji vingi katika maeneo hayo walikutana na maneno mengi sana lakini mengi yalikuwa na maneno ya shukrani kwa aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini mh.Willium Mganga Ngeleja, watu hawa walio wengi kwa idadi walisikika wakisema maneno " ASANTE NGELEJA KWA KUTUJALI, ISINGEKUWA WEWE LEO TUNGEKUWA GIZANI" kauli hii ilinishangaza sana na ilinibidi kuwahoji kwanini hasa wanamtaja Ngeleja kama wakushukuriwa na si Mh.Rais au hata Waziri wa Nishati na Madini wa sasa.

Wakazi hawa wa Njombe na Mbinga walisema kama sio Ngeleja na ubunifu wake leo hii tungekuwa gizani, wakaendelea yaani kama sio umeme wa wakala wa umeme vijijini REA, kitu ambacho Ngeleja alikianzisha kama mkombozi wa sisi watu tuishio vijijini leo tungekuwa gizani na hata nyuma kimaendeleo. " Tunamshukuru sana Ngeleja kwa kuianzisha REA na kuhakikisha sisi huku kijijini tunapata umeme kwa ajili ya maendeleo zaidi".

Wananchi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kusema kuwa viongozi wengi wamekuwa na upendeleo kwa maeneo wanapotoka hasa wanapopata nyadhifa kubwa kama aliyokuwa nayo Ngeleja lakini kwa huyu baba wa watu Ngeleja ni tofauti kabisa yaani ameacha huko kwao usukumani akatukumbuka wahehe na wabena na sisi wangoni pamoja na Wamatengo na hata ndugu zetu kule Nyasa, huyu ni mtu wa watu anajali sana watu na ana huruma sana kwani anatambua utu wa watu ni kiongozi mzuri sana hana upendeleo yaani huyu ni tofauti kabisa.

Wakazi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kulalmika na kuonesha kusononeka sana kwani wanadai hawakufurahishwa na kitendo cha maneno watu waliyokuwa wanamrushia na kumpakazia enzi za uongozi wake mpaka kumpelekea kujiuzulu mwaka 2012 mwezi May, wanadai kujiuzulu kwa Ngeleja kulikwamisha mambo mengi sana ikiwemo mipango mingi iliyokuwa mezani kwa ajili ya kuhakikisha vijiji vingi nchini vinapata umeme na kuvihakikishia maendeleo katika nyanja tofauti tofauti.

Wanaendelea kusema kuwa sisi umeme tuliletewa na tuliunganisha kwa bei rahisi sana yaan elfu 27 tuu, zamani ilikuwa mpaka laki saba lakini yule Msukuma wa watu akapambana mpaka ikashuka kiasi hicho eti bado watu wanasema hajui kuongoza sijui wanataka wafanyiwe nini ili waone mtu anafanya kazi, wanadai kama sio Ngeleja maisha yao kule vijijini yangekuwa ya giza sana na kusingekuwa na maendeleo kamwe.

Wanadai kuwa si huyu huyu Ngeleja aliepambana kuhakikisha swala la mgawo wa umeme nchini linapungua, au watu wamesahau kuwa Ngeleja ndiye aliyebuni mradi wa kuiunganisha mikoa yote ya Tanzania kwenye grid ya taifa kupitia miradi ya North-West Grid (kutokea Shinyanga,Geita,Kigoma,Katavi, Rukwa hadi Mbeya), Makambako-Songea na ule wa kuimarisha huduma ya umeme kupitia North-East Grid (kutokea Dares salaam hadi Kilimanjaro). lakini bado watu wanasema sio kiongozi mzuri walitaka awabebe mgongoni.. Kijana wa watu anafanya kazi kubwa sana na alitusaidia na daima tutashirikiana nae na kumkumbuka kwa safari yoyote atakayoianzisha.

Niliendelea kuwahoji na niliwadokeza kuwa kuna tetesi kuwa Ngeleja atagombea uraisi mwakani yaan hapa mpaka vilugha vyao vilizungumzwa waliaikika wahehe wakisema " Uwii, Inguluvi imlete munu huyu, tuisakumunu huyu ache kwa wewe" wakimaanisha "Mungu amlete mtu huyu,tunamuhitaji kwa ukombozi wetu" maneno haya yaliambatana na furaha kubwa iloyonishtua sana kwani sikitegemea wangelipokea swala hilo kwa furaha na shangwe kubwa wanasema watampitisha kwa hali na mali ili aendelee kuwatetea wao na watanzania kwa ujumla.

Walisema kwa walio tangaza nia mpaka sasa hakuna anayefaa kuwa raisi labda kama Ngeleja akigombea kama ndugu mwandishi ulivyotudokeza hapo, walilaumu kuwa mbona kama anataka kugombea uraisi yupo kimya mpaka sasa ? Mimi nilikosa cha kuwajibu na niliwaambia sijui anatafakari nini lakini nadhani kugombea uraisi ni moja ya fikra kubwa alizo nazo, waliomba kutembelewa na Mh. Ngeleja na mimi bila hajizi kwa sababu ya kazi yangu ya uandishi namba za viongozi huwa ninazo niliitafuta ilipokuwa namba ya Ngeleja na nilimpigia nikamwambia kuhusu kuwatembelea watu wa Njombe na Mbinga na yeye aliitika na kuwaahidi kuwa atapanga siku akawatembelee wazungumze vizuri na kujua wanaendeleaje, watu hawa walifarijika sana na kuendelea kuwa na imani kubwa na mh.Ngeleja na wamesema wanamuandalia zawadi kubwa mnoo kama shukrani...

Tunashukuru ndg mwandishi kwa kututembelea na Mungu akubariki sana popote ulipo, Mungu ibariki Njombe na Mbinga, Mungu ibariki Tanzania.A

Hizo mbwembwe tu za mwandishi mganga njaa.
 
Ngeleja yupi? Yule aliyekuwa mwajiri wa riz one?ambaye jk anataka awe Rais ili amfanye riz kuwa Waziri mkuu wake? Ama kweli watz wote twadhaniwa kuwa tayari mazezeta baada ya kuhalalishwa 'sembe' na viroba kuuzwa kila mahali nchini. Mshindwe na mlegee kwa jina la Yesu Kristo aliye hai.
 
Huyu Ngeleja ni mzuri sana, yaani kama tukiendeleza chuki na siasa chafu,tutakuja kupoteza jembe hili,asante sana watu wa njombe na mbinga kwa kumuona kamanda wetu huyu, yuko vzur kabisa mi nimempitisha ndani ya nafsi yangu
 
Khe khe khe khe kuomba mgao kuko kwa kila namna lol!!!! Zile 40m kazigusa kiduchu hujachelewa, kila la heri.
 
Ngeleja yupi? Yule aliyekuwa mwajiri wa riz one?ambaye jk anataka awe Rais ili amfanye riz kuwa Waziri mkuu wake? Ama kweli watz wote twadhaniwa kuwa tayari mazezeta baada ya kuhalalishwa 'sembe' na viroba kuuzwa kila mahali nchini. Mshindwe na mlegee kwa jina la Yesu Kristo aliye hai.

Naomba ujitahd kuwa muelewa ndugu, yaani kama unataka raisi kwa kizaz hiki, ni dhahiri kuwa mtu mwenye akili ya ujana anahtajika na sio masihara, na kijana mwenyewe ni Willium Mganga Ngeleja hao wengine wote chenga tuu
 
Umelipwa kiasi gani kuweka post hii? Hivi kweli hata kwa kufikiria kwa mbali Ngeleja anaweza kuwa Rais? Be serious bwana!

Kwanini asiwe raisi,ww unazijua principles za good leadership? Kama unazijua weka jamvini then niambie nini Ngeleja amekosa, ukifanya hivyo nitakubaliana na ww,lakini ni dhahiri kuwa Ngeleja atosha uraisi 2015
 
Umejiunga jana JF na umebandika post ya aina hii, Labda wewe umezaliwa leo. Nakuhakikishia Ngereja angekuwa waziri, mpaka leo tungekuwa kwenye mgao! Hizi zinazokusumbua ni hela alizotengeeza kwa kuutengeneza mgao feki siku zake
 
Ngeleja ndie mtu pekee anayeweza kutufikisha mahali fulani, ana akili za kipekee, ana mitazamo chanya ama kweli Ngeleja atosha
 
Naomba ujitahd kuwa muelewa ndugu, yaani kama unataka raisi kwa kizaz hiki, ni dhahiri kuwa mtu mwenye akili ya ujana anahtajika na sio masihara, na kijana mwenyewe ni Willium Mganga Ngeleja hao wengine wote chenga tuu

Hahahaaaa pole sana
 
Ngeleja yupi? Yule aliyekuwa mwajiri wa riz one?ambaye jk anataka awe Rais ili amfanye riz kuwa Waziri mkuu wake? Ama kweli watz wote twadhaniwa kuwa tayari mazezeta baada ya kuhalalishwa 'sembe' na viroba kuuzwa kila mahali nchini. Mshindwe na mlegee kwa jina la Yesu Kristo aliye hai.

Hahahahaha saizi kashfa ya escrow imemmaliza kabisa sidhani kama bado ana hizo ndoto........
 
Ngeleja ndie mtu pekee anayeweza kutufikisha mahali fulani, ana akili za kipekee, ana mitazamo chanya ama kweli Ngeleja atosha

Amini amini nakuambia Huyo ngeleja hawezi kua raisi hata usiponisadiki, yaani hata yeye mwenyewe anajua kabisa kwamba hawezi kua raisi.

Unajua ungekua unaleta hizo hoja za ngeleja tuko face to face lazima ungerusha ngumi, maana ningekucheka sana hadi uchukie
Eti ngeleja!! Lol!!
 
Amini amini nakuambia Huyo ngeleja hawezi kua raisi hata usiponisadiki, yaani hata yeye mwenyewe anajua kabisa kwamba hawezi kua raisi.

Unajua ungekua unaleta hizo hoja za ngeleja tuko face to face lazima ungerusha ngumi, maana ningekucheka sana hadi uchukie
Eti ngeleja!! Lol!!

Najua haumjui Ngeleja that's y..pata kumjua kidogo

WASIFU WA MHESHIMIWA WILLIUM MGANGA NGELEJA (THE CURRICULUM VITAE)

Particulars/ Husishi/Moja moja
Jina: WILLIUM
Jina la kati: MGANGA
Jina la mwisho/ukoo: NGELEJA
Tarehe kuzaliwa: 05/10/1967
Wasifu wa ndoa: AMEOA
Anuani: SLP 2000 DAR ES SALAAM
Simu ya kazi: 0754710070

Taaluma yake
2001-2002: CERTIFICATE YA SHERIA YA MAWASILIANO YA MITANDAO YA SIMU WITWATERSRAND UNIVERSITY SOUTH AFRICA
1996-1999: MASTERS IN LAW (LLM)UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
1991-1994: LLB UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
1987-1989: A-LEVEL IHUNGO HIGH SCHOOL
1983-1986: O-LEVEL MPWAPWA SECONDARY SCHOOL
1976-1982: PRIMARY EDUCATION(ELIMU YA MSINGI) BITOTO PRIMARY SCHOOL

Historia ya kazi
2005-2015: MBUNGE BUNGE LA TANZANIA (JIMBO LA SENGEREMA)
1/12/2007-08/02/2008: NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI
Feb 2008-May 2012: WAZIRI NISHATI NA MADINI
2000-2005: MWANASHERIA MKUU VODACOM TANZANIA
1995-2000: MWANASHERIA MKUU PRICE WATERHOUSE COOPERS COMPANY
1994-1995: OFISI YA MWANASHERIA MKUU KWA AJILI YA MAFUNZO YA SHERIA YA NCHI NA UTUMIZI SAMBAMBA NA USIMAMIZI WAKE

Wasifu kisiasa ndani ya chama (CCM)
1980-1981: MWENYEKITI WA VIJANA SHULE YA MSINGI BITOTO
2012-2017: MJUMBE HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA

Na huo ndioo wasifu wa mheshimiwa Ngeleja...
 
NJOMBE, MBINGA ASANTE NGELEJA KWA KUTUTOA GIZANI

Na mwandishi wetu,

Juzi wakati wawakilishi wa gazeti letu walipotembelea maeneo ya Njombe na Mbinga wakihoji kuhusu namna umeme ulivyovifikia vijiji vingi katika maeneo hayo walikutana na maneno mengi sana lakini mengi yalikuwa na maneno ya shukrani kwa aliyekuwa waziri wa Nishati na Madini mh.Willium Mganga Ngeleja, watu hawa walio wengi kwa idadi walisikika wakisema maneno " ASANTE NGELEJA KWA KUTUJALI, ISINGEKUWA WEWE LEO TUNGEKUWA GIZANI" kauli hii ilinishangaza sana na ilinibidi kuwahoji kwanini hasa wanamtaja Ngeleja kama wakushukuriwa na si Mh.Rais au hata Waziri wa Nishati na Madini wa sasa.

Wakazi hawa wa Njombe na Mbinga walisema kama sio Ngeleja na ubunifu wake leo hii tungekuwa gizani, wakaendelea yaani kama sio umeme wa wakala wa umeme vijijini REA, kitu ambacho Ngeleja alikianzisha kama mkombozi wa sisi watu tuishio vijijini leo tungekuwa gizani na hata nyuma kimaendeleo. " Tunamshukuru sana Ngeleja kwa kuianzisha REA na kuhakikisha sisi huku kijijini tunapata umeme kwa ajili ya maendeleo zaidi".

Wananchi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kusema kuwa viongozi wengi wamekuwa na upendeleo kwa maeneo wanapotoka hasa wanapopata nyadhifa kubwa kama aliyokuwa nayo Ngeleja lakini kwa huyu baba wa watu Ngeleja ni tofauti kabisa yaani ameacha huko kwao usukumani akatukumbuka wahehe na wabena na sisi wangoni pamoja na Wamatengo na hata ndugu zetu kule Nyasa, huyu ni mtu wa watu anajali sana watu na ana huruma sana kwani anatambua utu wa watu ni kiongozi mzuri sana hana upendeleo yaani huyu ni tofauti kabisa.

Wakazi hawa wa Mbinga na Njombe waliendelea kulalmika na kuonesha kusononeka sana kwani wanadai hawakufurahishwa na kitendo cha maneno watu waliyokuwa wanamrushia na kumpakazia enzi za uongozi wake mpaka kumpelekea kujiuzulu mwaka 2012 mwezi May, wanadai kujiuzulu kwa Ngeleja kulikwamisha mambo mengi sana ikiwemo mipango mingi iliyokuwa mezani kwa ajili ya kuhakikisha vijiji vingi nchini vinapata umeme na kuvihakikishia maendeleo katika nyanja tofauti tofauti.

Wanaendelea kusema kuwa sisi umeme tuliletewa na tuliunganisha kwa bei rahisi sana yaan elfu 27 tuu, zamani ilikuwa mpaka laki saba lakini yule Msukuma wa watu akapambana mpaka ikashuka kiasi hicho eti bado watu wanasema hajui kuongoza sijui wanataka wafanyiwe nini ili waone mtu anafanya kazi, wanadai kama sio Ngeleja maisha yao kule vijijini yangekuwa ya giza sana na kusingekuwa na maendeleo kamwe.

Wanadai kuwa si huyu huyu Ngeleja aliepambana kuhakikisha swala la mgawo wa umeme nchini linapungua, au watu wamesahau kuwa Ngeleja ndiye aliyebuni mradi wa kuiunganisha mikoa yote ya Tanzania kwenye grid ya taifa kupitia miradi ya North-West Grid (kutokea Shinyanga,Geita,Kigoma,Katavi, Rukwa hadi Mbeya), Makambako-Songea na ule wa kuimarisha huduma ya umeme kupitia North-East Grid (kutokea Dares salaam hadi Kilimanjaro). lakini bado watu wanasema sio kiongozi mzuri walitaka awabebe mgongoni.. Kijana wa watu anafanya kazi kubwa sana na alitusaidia na daima tutashirikiana nae na kumkumbuka kwa safari yoyote atakayoianzisha.

Niliendelea kuwahoji na niliwadokeza kuwa kuna tetesi kuwa Ngeleja atagombea uraisi mwakani yaan hapa mpaka vilugha vyao vilizungumzwa waliaikika wahehe wakisema " Uwii, Inguluvi imlete munu huyu, tuisakumunu huyu ache kwa wewe" wakimaanisha "Mungu amlete mtu huyu,tunamuhitaji kwa ukombozi wetu" maneno haya yaliambatana na furaha kubwa iloyonishtua sana kwani sikitegemea wangelipokea swala hilo kwa furaha na shangwe kubwa wanasema watampitisha kwa hali na mali ili aendelee kuwatetea wao na watanzania kwa ujumla.

Walisema kwa walio tangaza nia mpaka sasa hakuna anayefaa kuwa raisi labda kama Ngeleja akigombea kama ndugu mwandishi ulivyotudokeza hapo, walilaumu kuwa mbona kama anataka kugombea uraisi yupo kimya mpaka sasa ? Mimi nilikosa cha kuwajibu na niliwaambia sijui anatafakari nini lakini nadhani kugombea uraisi ni moja ya fikra kubwa alizo nazo, waliomba kutembelewa na Mh. Ngeleja na mimi bila hajizi kwa sababu ya kazi yangu ya uandishi namba za viongozi huwa ninazo niliitafuta ilipokuwa namba ya Ngeleja na nilimpigia nikamwambia kuhusu kuwatembelea watu wa Njombe na Mbinga na yeye aliitika na kuwaahidi kuwa atapanga siku akawatembelee wazungumze vizuri na kujua wanaendeleaje, watu hawa walifarijika sana na kuendelea kuwa na imani kubwa na mh.Ngeleja na wamesema wanamuandalia zawadi kubwa mnoo kama shukrani...

Tunashukuru ndg mwandishi kwa kututembelea na Mungu akubariki sana popote ulipo, Mungu ibariki Njombe na Mbinga, Mungu ibariki Tanzania.
 
How much are you paid for this work ?lakini nina ku-admire ,una courage na bidii sana ya kufanya promo,I am sure hata ukipewa maandazi meusi unaweza kuyatafutia soko vizuri tu.
 
Back
Top Bottom