Mjanga
JF-Expert Member
- Feb 13, 2011
- 1,238
- 325
Salaam kwako Mzee Mwanakijiji na wanavijiji wengine!
Kwa haya tunayoyaona, wale waliotuhaminisha kwamba wanatuongoza kuelekea kwenye ukombozi wa pili wa Kifikra na Kiuchumi, wanageuka na kutaka kutuaminisha kwamba "Kijani" ndiyo chagua sahihi-nina mashaka. Tunajuwa wanaye kiongozi mwenye uwezo wa kukariri maili za barabara, idadi ya samaki na mifugo wengine, hata idadi ya wapiga kura. kama hiyo ni sifa, anafaa kwelikweli.
Kwa kiongozi, ambaye, katika karne hii bado anaamini katika kutembeza bakuli kwa wafadhili-ndiko kunakoleta maendeleo- ilhali nchi yake ina rasilimali nyingi kuliko hata kwa hao mabwana wakubwa-kweli anatufa kwelikweli!
Karne hii, kama tumefika sehemu tunataka tuwaaminishe watanzania kuwa bila Kijani, nchi itakuwa kama Libya...this is too wrong. Kwani ni mazingira mawili tofauti kabisa. watanzania wanaenda kupiga kura na kupractice democracy, ya Libya ilikuwa ni uhasi uliochochewa na Mataifa ya Magharibi-hatufanani nao hata kwa chembe....Kiongozi wa aina hii- waTanzania, anatufaa kwelikweli...
Wataalamu wa saikolojia ya elimu wanasema, miongoni mwa vitu vinavyoathiri afya ya akili ni pamoja na kukariri bila utaratibu, kwani hii hali inamfanya mtu kupoteza uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo (Critical thinking). Ikifikia hapa mtu hujaa sifa akiamini anaweza...
Naamini UKAWA ni ya waTanzania, naamini CHADEMA ni ya waTanzania,..Naamini CCM ni ya baadhi ya waTanzania wachache sana. Hii ndiyo maana waTanzania wanaonekana "Wapumbavu na Malofa". Wanasababu ya kuwaita watanzania hivyo, kwa sababu kila mwaka wa uchaguzi wanatuahidi vitu vingi visivyotekelezeka, na tunawachagua iwe kwa uhalali wa kura ama vinginevyo, na waTanzania hatusemi, na hatulalamiki....
Naamini waTanzania wamefikia kiwango cha juu cha uelewa, wameshalalamika vyakutosha, sasa ni muda wa vitendo. Naamini "vichinjio" vyao vitatumika vyema kutupa kiongozi atakaye tuongoza kuelekea ukombozi wa pili...
Mimi siyo muumini wa Chama chochote cha Siasa, ila ni muumini wa mabadiliko, hasa mabadiliko ya kweli...ukitaka kupitisha njia penye mlima, ni vema ukauvunjilia mbali huo mlima ili upate njia...
Watanzania lazima wajiulize...siku zote hizo alikuwa wapi? kwanini hakutokea siku walipofanyamakubaliano? Tumewaona akina Gasia na Nchimbi walivyoreact siku mpendwa wao alipokatwa...angalau ilileta mashiko...huyu wetu alikuwa anasubiri nini?????........
Mabadiliko ni sasa, mabadiliko ni wewe, yule, na mimi, mabadiliko ni sisi! Tusipuuze maumivu na vilio vya waTanzania vinavyotokana na ukosefu na uhaba wa huduma za msingi na ajira...waTanzania wamechoka kuwachoma watoto na vijana wao kwa kesi za ukabaji na uporaji mdogomdogo, huku tukiambiwa kuwa rasilimali zetu zinatoroshwa kwa ving'ora! Tusipuuze kabisa.
Kwa haya tunayoyaona, wale waliotuhaminisha kwamba wanatuongoza kuelekea kwenye ukombozi wa pili wa Kifikra na Kiuchumi, wanageuka na kutaka kutuaminisha kwamba "Kijani" ndiyo chagua sahihi-nina mashaka. Tunajuwa wanaye kiongozi mwenye uwezo wa kukariri maili za barabara, idadi ya samaki na mifugo wengine, hata idadi ya wapiga kura. kama hiyo ni sifa, anafaa kwelikweli.
Kwa kiongozi, ambaye, katika karne hii bado anaamini katika kutembeza bakuli kwa wafadhili-ndiko kunakoleta maendeleo- ilhali nchi yake ina rasilimali nyingi kuliko hata kwa hao mabwana wakubwa-kweli anatufa kwelikweli!
Karne hii, kama tumefika sehemu tunataka tuwaaminishe watanzania kuwa bila Kijani, nchi itakuwa kama Libya...this is too wrong. Kwani ni mazingira mawili tofauti kabisa. watanzania wanaenda kupiga kura na kupractice democracy, ya Libya ilikuwa ni uhasi uliochochewa na Mataifa ya Magharibi-hatufanani nao hata kwa chembe....Kiongozi wa aina hii- waTanzania, anatufaa kwelikweli...
Wataalamu wa saikolojia ya elimu wanasema, miongoni mwa vitu vinavyoathiri afya ya akili ni pamoja na kukariri bila utaratibu, kwani hii hali inamfanya mtu kupoteza uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo (Critical thinking). Ikifikia hapa mtu hujaa sifa akiamini anaweza...
Naamini UKAWA ni ya waTanzania, naamini CHADEMA ni ya waTanzania,..Naamini CCM ni ya baadhi ya waTanzania wachache sana. Hii ndiyo maana waTanzania wanaonekana "Wapumbavu na Malofa". Wanasababu ya kuwaita watanzania hivyo, kwa sababu kila mwaka wa uchaguzi wanatuahidi vitu vingi visivyotekelezeka, na tunawachagua iwe kwa uhalali wa kura ama vinginevyo, na waTanzania hatusemi, na hatulalamiki....
Naamini waTanzania wamefikia kiwango cha juu cha uelewa, wameshalalamika vyakutosha, sasa ni muda wa vitendo. Naamini "vichinjio" vyao vitatumika vyema kutupa kiongozi atakaye tuongoza kuelekea ukombozi wa pili...
Mimi siyo muumini wa Chama chochote cha Siasa, ila ni muumini wa mabadiliko, hasa mabadiliko ya kweli...ukitaka kupitisha njia penye mlima, ni vema ukauvunjilia mbali huo mlima ili upate njia...
Watanzania lazima wajiulize...siku zote hizo alikuwa wapi? kwanini hakutokea siku walipofanyamakubaliano? Tumewaona akina Gasia na Nchimbi walivyoreact siku mpendwa wao alipokatwa...angalau ilileta mashiko...huyu wetu alikuwa anasubiri nini?????........
Mabadiliko ni sasa, mabadiliko ni wewe, yule, na mimi, mabadiliko ni sisi! Tusipuuze maumivu na vilio vya waTanzania vinavyotokana na ukosefu na uhaba wa huduma za msingi na ajira...waTanzania wamechoka kuwachoma watoto na vijana wao kwa kesi za ukabaji na uporaji mdogomdogo, huku tukiambiwa kuwa rasilimali zetu zinatoroshwa kwa ving'ora! Tusipuuze kabisa.
Na kweli mpo mnaoamini ni mali ya Watanzania? well.. labda kweli mpo mnaoamini hivyo.