Mimi nilipata jana 26240 na leo nimepata 8900. Ili uweze kupata gawio la kutosha jenga utamaduni wa kuweka pesa kwenye akaunti yako bila kutoa angalau kwa mwezi mmoja. Km unaingiza pesa na kuzitoa hata ungefanya miamala ya thamani kubwa kiasi gani haitakusaidia kupata gawio kubwa. Nawashauri mjitahidi kuweka akiba kwa kuweka pesa kwenye akaunti zenu kupitia wakala M-PESA na si kutumiwa na mtu. Pesa ya kutumiwa haihesabiwi. Zile pesa unazoweka akiba kwenye akaunti yako huwa zinaingizwa kwenye mzunguko wa biashara na ndo maana unapata gawio. Mfumo wa mpesa ni mfumo uleule wa bank.