kajekudya
JF-Expert Member
- Sep 24, 2015
- 2,469
- 4,904
Zipo taarifa ambazo wewe mwenyewe umezithibitisha kuwa mara baada ya Uchaguzi utarudi Ubelgiji, huko ulipokuwa kwa takribani miaka mitatu na kurudi siku chache kabla ya zoezi la Uchaguzi mkuu kuanza. Ni jambo jema kuwa ulijua huwezi kutoboa na ukafanya maandalizi hayo mapema.
Sasa sisi Watanzania tunao utamaduni wetu, utamaduni adhimu sana, tunapopata mgeni basi wakati wa kurudi hupenda kumumtuma salaam ili kuwapelekea wale aliowaacha huko! Basi nasi Watanzania tunakutuma salaam hizi.
1. Mwambie Robert Tanzania ni nguli katika siasa, Mwambie hadi mda huu ina vikoloni vyake inavitawala. Mpe ukweli kuwa Rais wa Tanzania hupatikana Tanzania, pale Dodoma na si kwenye hoteli za nyota tano huko Brussels, New York, London au Paris. Mkumbukeshe kuwa Watanzania wana utamaduni tofauti kabisa na ule wa zile nchi zilivyotawaliwa na Ubelggiji na Ufaransa ambazo Marais wake bado wanaamriwa Brussels na Paris.
2. Mkumbushe Watanzania wanaamini bado katika Ujamaa, umoja na kujitegemea. Waambie wanajua kuwa Mabeberu hawajawahi kuwa watu wema kwao na wanacheza nao kwa tahadhari. Waambie Watanzania linapokuja swala la maslahi ta Nchi huwa kitu kimoja, huachagua Maslahi ya Nchi bila kujali gharama zake, Mwambie uzalendo bado umetamalaki!
3. Mwambie na hii kwa Kumnong'oneza, kuwa vyama vya upinzani kikiwemo hicho chako ni vimatawi vya Chama na shughuli zake zinaratibiwa na kitengo, ndio maana ni vya msimu vinapanda na kushuka. Mwambie hata Chairman wako na Mtendaji mkuu wako ni waajiriwa watiifu. Mwambie hata huyu Sheikh na huyu Askofu nao ni waajiiriwa watiifu ndio maana wamewekwa karibu yako kipindi hiki, hawa ndio watakaomaliza mchezo. Mwambie mfumo wa siasa na ulinzi wa Tanzania ni very complex. Mkumbushe sarakasi za Mbobezi, Mkumbushe pia kuhusu yule kipenyo aliyewahi kupenya hadi ngazi ya Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa
4. Waambie kuwa kwa mjibu wa utaratibu wa Uchaguzi Tanzania hakunaga Mpinzani wa kudumu, ila wapo wa Msimu, hivyo na wewe ulikuwa wa Msimu huu tu, Msimu ujao atatengenezwa Mpinzani mwingine, waambie wakutafutie kazi nyingine kabisa. Wakumbushe kuwa hata wewe ulitengenezwa ili kuhahakikisha Lowassa anasahaulika vichwani mwa Watanzania na kura zake millioni 6, kazi ambayo umeifanya kwa uaminifu na kwa uadilifu, Lowassa Sasa yupo CCM baada ya kupuuzwa, hiyo yote ilikuwa kazi yako. Hivyo waambie kuwa Mara baada ya Uchaguzi ataandaliwa Mpinzani mwingine ili kuhakikisha wewe unafifia.
Tafadhali Fikisha salamu zetu na Asante kwa kuja.
Sasa sisi Watanzania tunao utamaduni wetu, utamaduni adhimu sana, tunapopata mgeni basi wakati wa kurudi hupenda kumumtuma salaam ili kuwapelekea wale aliowaacha huko! Basi nasi Watanzania tunakutuma salaam hizi.
1. Mwambie Robert Tanzania ni nguli katika siasa, Mwambie hadi mda huu ina vikoloni vyake inavitawala. Mpe ukweli kuwa Rais wa Tanzania hupatikana Tanzania, pale Dodoma na si kwenye hoteli za nyota tano huko Brussels, New York, London au Paris. Mkumbukeshe kuwa Watanzania wana utamaduni tofauti kabisa na ule wa zile nchi zilivyotawaliwa na Ubelggiji na Ufaransa ambazo Marais wake bado wanaamriwa Brussels na Paris.
2. Mkumbushe Watanzania wanaamini bado katika Ujamaa, umoja na kujitegemea. Waambie wanajua kuwa Mabeberu hawajawahi kuwa watu wema kwao na wanacheza nao kwa tahadhari. Waambie Watanzania linapokuja swala la maslahi ta Nchi huwa kitu kimoja, huachagua Maslahi ya Nchi bila kujali gharama zake, Mwambie uzalendo bado umetamalaki!
3. Mwambie na hii kwa Kumnong'oneza, kuwa vyama vya upinzani kikiwemo hicho chako ni vimatawi vya Chama na shughuli zake zinaratibiwa na kitengo, ndio maana ni vya msimu vinapanda na kushuka. Mwambie hata Chairman wako na Mtendaji mkuu wako ni waajiriwa watiifu. Mwambie hata huyu Sheikh na huyu Askofu nao ni waajiiriwa watiifu ndio maana wamewekwa karibu yako kipindi hiki, hawa ndio watakaomaliza mchezo. Mwambie mfumo wa siasa na ulinzi wa Tanzania ni very complex. Mkumbushe sarakasi za Mbobezi, Mkumbushe pia kuhusu yule kipenyo aliyewahi kupenya hadi ngazi ya Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa
4. Waambie kuwa kwa mjibu wa utaratibu wa Uchaguzi Tanzania hakunaga Mpinzani wa kudumu, ila wapo wa Msimu, hivyo na wewe ulikuwa wa Msimu huu tu, Msimu ujao atatengenezwa Mpinzani mwingine, waambie wakutafutie kazi nyingine kabisa. Wakumbushe kuwa hata wewe ulitengenezwa ili kuhahakikisha Lowassa anasahaulika vichwani mwa Watanzania na kura zake millioni 6, kazi ambayo umeifanya kwa uaminifu na kwa uadilifu, Lowassa Sasa yupo CCM baada ya kupuuzwa, hiyo yote ilikuwa kazi yako. Hivyo waambie kuwa Mara baada ya Uchaguzi ataandaliwa Mpinzani mwingine ili kuhakikisha wewe unafifia.
Tafadhali Fikisha salamu zetu na Asante kwa kuja.