ARUSHA: Lowassa kumtembelea Lema gerezani Kisongo

ARUSHA: Lowassa kumtembelea Lema gerezani Kisongo

Hivi ni kweli EL haelewani kisiasa na kimtazamo kwenye siasa za CDM na Lema?? Ni kheri wazike tofauti zao kwa sasa na kuangalia mbele kutatua tatizo lililopo sasa kw faida ua ubinadamu na chama! Tofauti za itikadi zao na ideology ifuate baadae
 
Hapo lowasa anaenda kuhakiki kuwa kweli mbaya wake Lema yuko KIsongo.Kimoyo moyo LOwasa atakuwa anachekelea sababu ni Lema ni mmojapo wa waliomnanga sana bado hawa wengine kwenye hilo kundi

13233029_1590768097881921_7440964151336377693_n-jpg.360620
Kwenye siasa hakuna adui wa kudumu
 
Labda watatafuta suluhu na kumaliza tofauti zao, yaani kati ya Lema na fisadi Lowasa!

Dah hapo CDM ndio huwa nashindwa kuwaelewa, mtu ambaye walizunguka kuhubiri kuwa ni fisadi mkubwa leo hii eti ndio mleta mabadiliko?, non sense kabisa, siungi mkono CCM but also siwezi unga mkon CDM kwa kuhubiri wasichokiamin na kukiishi
 
Ufisadi mkuu wa EL ni Richmond, je, mwenye Richmond in EL!?
Hata kama EL aliamua wakati huo kushirikiana na watu katika kuwafichia madhambi ni wazi sasa kaenda mbele zaidi kwa kulikana hilo kundi hadharani (kutubu) na kujiunga na upande mwingine, sisi ni nani mpaka tusimpokee!?
 
Kama ingekuwa ni MIMI ningempigia simu DPP na kumwambia aweke NOLLE PROSEQUI/Serikali haina haja ya kuendelea na kesi hii.
Hapo ANGEZIMA UKAWA!

Si kwamba LEMA hajakosa bali Magufuli angekuwa amecheza KARATA ya kisiasa kubwa sana na FAIDA kwa upande wake.

Maana the more LEMA anahangaika kupata DHAMANA, ndivyo Magufuli ANAVYOUJENGA na kuupa NGUVU upinzani.

Wazungu walimfunga Mandela ili kumnyamazisha kwa miaka 27.
Ilibidi De Klerk amsamehe na kusema aruhusiwe kugombea URAIS na hatimaye akawa RAIS.

NGUVU na VITISHO havisaidii. bali ni UJANJA na HEKIMA za kisiasa ambazo ni LAZIMA Magufuli ajue kuzicheza!

Kubalansi kati ya USOMI, UTAWALA, Na more importantly kuwa MWANASISASA mjanja.
Kiasi kuwa unaweza kufanya kazi hata na yule aliyekuwa anakuombea mabaya.

Nchi ya jirani zetu. Moi wa Kenya alimfunga Odinga mara nyingi sana akijaribu kumnyamazisha.Lakini Haikumsaidia mpaka ilibidi Moi kuwa mwana siasa MWELEVU na MJANJA.
Akamwingiza katika chama chake cha KANU na kumfanya kuwa katibu mkuu.NCHI IKATULIA KIASI.
HUO NDO UJANJA wa KISIASA.

KUTUMIA NGUVU na mamlaka na vyombo vya dola mara nyingi HAKULIPI bali huzaa REBELLION/UASI na political tensions ambazo HAZINA maana na impact zake ni kubwa sana kitaifa!
Kwanza CV yetu kama taifa na ya RAIS kimataifa INAHARIBIKA sana!!!

Rais Magufuli AKIMSAMEHE Lema hatakuwa AMEPOTEZA chochote bali atakuwa amewafunga wapinzani MAGOLI.
Hata hivyo akili ni nywele kila mtu ana zake!
Kama Putin alivyofunga Goli kwa kutolipiza kufukuzwa maofisa wake.
 
Kama Putin alivyofunga Goli kwa kutolipiza kufukuzwa maofisa wake.
Huo ndo UJANJA na WELEVU wa KISIASA. Maana Putin alijua AMEWEKEWA MTEGO na Obama ili AKASIRIKE na ALIPIZE KISASI.

Badala yake Pitin AKAALIKA watoto wa MABALOZI wa Marekani kusherehekea Krismasi IKULU ya Kremlin Moscow.
Akawa amemfunga Obama magoli 10 kwa BILA na hana hamu tena na ujanja wa kisiasa wa Putin.
 
Haisaidii kutafuta kiki ya Kisiasa kwa muhalifu Lema! Hata angefanyaje Lowassa haibuki tena Kisiasa! He is completely and politically finished!!!

Kila kizuri kina ubaya wake na kila kibaya kina uzuri wake! Watu wa caliber ya Lema wana mchango mkubwa katika kuendeleza relevance ya magereza yetu na vyombo vyetu vingine vya dola. Bila wao, waajiriwa wa vyombo vyetu hivyo watapoteza ulazima wa kuwepo kwao na hivyo kulazimika kuachishwa kazi. Tuwashukuru hata kwa hilo!
 
Kwa iyo wamempelekea machungwa huko lupango au wameenda kumsanifu tu?
 
Hizo Political science za kwenye madaftari ni mbwembwe tu.

Mimi sizungumzii jamaa yetu ama siyo yetu.
Nazungumzia UJANJA wa kisiasa . Kama ungekuwa unajua POLITICAL SCIENCE ungenielewa
Lakini kama wewe ni shabiki tu.
HUTANIELEWA!
 
Back
Top Bottom