Ringo Edmund
JF-Expert Member
- May 10, 2010
- 4,879
- 1,134
dhaifu aliserma kuwa sasa arusha iko safi.
Watajuta kwanini walimchagua yule kichaa, sasa hawana hata wa kuwa wakilisha Bungeni
Nashukuru na nimeliona limeandikwa pia kwenye blog ya michuzi. Tuacheni utani na masihara mji wa Arusha kwa sasa una hali mbaya sana. Hali ya mji wa Arusha kiuchumi kwa sasa sio maridhawa kabisa. Nilijaribu kutembelea maeneo mengi ya kibiashara km sokoni ambapo kuna maduka mbali mbali . Ikifika saa 10 tu jioni wanaanza kufunga hakuna wateja, hata zile siku za kawaida za kazi. Biashara za taxi , ma-bus ndio usiseme, karibia 90% ni mbovu mbovu sana. Hali ya usafi wa mji ni mbaya sana. Kwa kweli , wana JF tuna haja yakuutizama upya mji huu, GENEVA OF AFRICA INAPOTEA KWENYE RAMANI
Shule ni muhimu hata mpaka darasa la saba.
Mkuu usimfukuze tena kichaa aliechukua nguo zako mtoni wakati ukioga maji, utaonekana wewe ndiyo kichaa, waache waropokaji wanaomwita Lema kichaa wakati wanaona ni dhahiri hali ya uchumi ni ngumu nchi nzima.Acha ushamba mkuu si vyema kumwita mh. Mbunge G. Lema Kichaa. Je walikochagua wenye akili timamu hali za majimbo yao zikoje ukilinganisha na Arusha? Hivi huyu anayelalamika alitaka akipita mjini watu wamnunulie soda na chips ndo ajue hali ya Arusha ni nzuri? hli ya Arusha haina tofauti kiuchumi na mikoa mingine. Kigezo ambacho angekitumia ni kwenda TRA kuangalia kama mapato yameshuka kwa kiasi gani kutokana na watu kufunga biashara. Ujinga alioleta hapa hatujui unalengo gani kwani hata mikoa kama Mwanza, Morogororo na Dar hali sio nzuri je huko nako kuna Vichaa wabunge?
mkaliwakitaa unapozungumzia September 11 unarudi nyuma mpaka mwaka 2001 ile hali haina uhusiano na uchumi wa Arusha. Kwanza kabisa Uchumi wa Arusha upo juu sana kwani ni ya tatu baada ya DSM na Mwanza. Unaposema utalii umepungua unatumia vigezo gani? Kwa mawazo yako kampuni za kitalii zinaongezeka siku hadi siku au zinapungua? Jibu ni kuwa zinaongezeka; sasa kama watalii wamepungua hizo kampuni zinahudumia kina nani? Mahoteli na Camping sites zimeongezeka sana na kila moja inapata wateja wa kutosha hivyo ushawishi wenu hauna nguvu. Miaka miwili iliyopita Arusha haikuwa na "Traffic Jam" leo Jam kila kona; hayo magari yameokotwa kama Arusha Kwishney?Mi nadhani labda mtoa mada atakua amedondoka toka huko mbele mda si mrefu ndio maana anaona kama vile mji umezorota sana..hali hii ni kawaida kama ulikua nje ya nchi kwa muda flani halafu ukarudi hm.lzima utaona kama vile hali ya maisha imeshuka sana kulinganisha na zamani!!! Zamani imeshapita..sikatai hali imekua mbaya Arusha..lakini mabadiliko ya kiuchumi ya mji wa arusha yametokea kutokana na mambo mawili makubwa....kwanza ..baada ya machimbo ya tanzanite kumilikiswa makaburu na pili...baada ya september 11, na mtikisiko wa uchumi wa dunia...watalii walipungu kwakasi ya ajabu...hivyo kwa kiasi flani uchumi wa arusa umeshuka lakini sio sana ingawa bado kuna masalia ya tanzanite na watalii..lakini ikumbukwe kua idadi ya makampuni pia imeongezeka hivyo ushindani umekua mkubwa pia katika sekta zote..mji pia umetanuka sio kama zamani town ndio ilikua kila kitu..
yazewa kuwa mimi ni fisadi mwenyewe nae faidika na CCM.We majebere unaonekana ni houseboy wa fisadi!Kaa mkao wa kula bosi wako yupo hatarini 2015 mtaenda kutafuta mashamba aliyekwisha wauzia wazungu!
Uongo wa CCM kumbe upo hata ndani yako. Pole Majebere. CCM Ziiiiiiiiiiiiiiiii, Chadema Oyeeeeeeeeee!Rekebisha kidogo hapo, ni Lema sio mheshimiwa mbunge. Halafu hivi wewe umeenda Mwanza hivi karibuni? Nakushauri uende ukaone biashara inavyo kwenda.
Sio arusha tu,...mbona dar ndio zaidi
Nashukuru na nimeliona limeandikwa pia kwenye blog ya michuzi. Tuacheni utani na masihara mji wa Arusha kwa sasa una hali mbaya sana. Hali ya mji wa Arusha kiuchumi kwa sasa sio maridhawa kabisa. Nilijaribu kutembelea maeneo mengi ya kibiashara km sokoni ambapo kuna maduka mbali mbali . Ikifika saa 10 tu jioni wanaanza kufunga hakuna wateja, hata zile siku za kawaida za kazi. Biashara za taxi , ma-bus ndio usiseme, karibia 90% ni mbovu mbovu sana. Hali ya usafi wa mji ni mbaya sana. Kwa kweli , wana JF tuna haja yakuutizama upya mji huu, GENEVA OF AFRICA INAPOTEA KWENYE RAMANI