Arusha imebadilika kabisa

Arusha imebadilika kabisa

Huu mji utashuka mapato saana...miji inayotegemea utalii duniani kote inaisoma namba... Poleni aisee.
 
Huu mji utashuka mapato saana...miji inayotegemea utalii duniani kote inaisoma namba... Poleni aisee.
Watu tunaisoma namba haswa hapa, hoteli zote kubwa zimefungwa biashara hamna, migahawa ya kizungu yote nayo imefungwa,
Magari ya kitalii nayo yamepaki hayana PA kwenda, makampuni mengi hapa yamekufa.
 
Mtakufa njaaa Arusha. Taften alternative kwa miaka miwili ijayo. Corona inaimpact kubwa sana kiuchumi. Watu hawawezi toka lockdown waje kutalii. Wanaenda kutafta pesa kwanza. Hata wenye pesa wanapenda maisha yao. Kutalii ni kama sucide mission.
 
Mtakufa njaaa Arusha. Taften alternative kwa miaka miwili ijayo. Corona inaimpact kubwa sana kiuchumi. Watu hawawezi toka lockdown waje kutalii. Wanaenda kutafta pesa kwanza. Hata wenye pesa wanapenda maisha yao. Kutalii ni kama sucide mission.
Watalii watakuja tu kijana. Wengi wameshachoka kukaa ndani huko nchi za watu
 
Arusha tunalia sana,ajira,watu wengi wapo majumbani kwa miezi miwili sasa,hakuna kazi,utalii hoi.
 
Nadhani hayapo...Manyara labda.
Watu huwa wanachanganya wanadhani madini hasa Tanzanite ipo Arusha....Na vijana wa Arusha wanawa-indoctrinate hivyo.
Huwa nacheka sana, unakutana na mtu na manyonyo yake yameshalalaga au mtu na madevu yake kidevu kimeshakomaaga anasema anaenda zake Arusha mererani au Arusha ina Tanzanite.😝
 
We jombii umekuja kuwaje mbona unatuzalilisha arif. We kama unalia lia, lia tu kimpango wako kwaiyo bila utalii maisha hayaendi au we ndo wale ulikuwa ukitoka safari unatusumbua kitaa hukujua nn maana ya saving wala huku taka kusikia ni bia na wine sasa utachemsha supu ya mawe ukunywe mpaka korona ikate mta nyooka kama spoku. Saivi nadhani kila mtu kapata uhalisia wa life sasa season ukirudi bugia tena
Wakuu Amani iwe nanyi., Peace and love wana jf.

Jambo ambalo nataka kusema ni kuwa Arusha imebadilika kwa kiasi kikubwa sana tangu hili gonjwa liingie yaani ni balaa.

Arusha ni mji uliojaa wazungu kila Kona utafikiri tupo South Africa na tushazoea kufanya biashara au mazungumzo ya hapa na pale na hawa wadoshi wakiwa hapa jijini.

Na wazungu wengi wao wamewekeza sana hapa. Asilimia kubwa sana ya wana Arusha pato Lao kubwa achia mbali madini la pili ni utalii.

Lakini kwa sasa hali ni tofauti kabisa urafikiri tupo singida au wap sijui hatuoni wazungu kabisa kabisa hata Ile migahawa wazungu hukaa hamna mtu mweupe hata kidogo.

Hotel, migahawa, na kule vinyagago na sehemu zote wazungu wanapopendelea kutembea au kukaa hamna kabisa watu weupe.

Makampuni mengi, migahawa, maduka na hata masoko wengi tunategemea utalii, sahiv kila mtu analia.

Watu weusi tunalia Arusha kwa kweli sijui kwa mikoa mingine mimi ila hapa chuga tunalia
 
kwamba wazunguu😅😅😅😅 sasa rasta man wanyoe tu waende veta
 
Back
Top Bottom