ARUMERU NA TAFITI: TABIA MBAYA SANA__sana.!!

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
TABIA MBAYA SANA
Kuna wanadam wana akili zilizochoka kweli kweli hawa wenye mashirika ya Tafiti pale wanapofanya tafiti za Kikampeni(sio kisiasa)..
Kwa mujibu wa maelezo niliyoyapata kutoka kwa wananchi mbalimbali hapa Arumeru mashariki, wakati ambapo mbio za kampeni zikiendelea, kuna watu wemevaa vaa vifulana na kujitambulisha kwa wananchi kama wakala kutoka mashirika ya Utafiti. Na wanatafiti nani atashinda kwenye kinyan’ganyiro cha Ubunge Jimboni humo. Mbona akili hizi zingine za kihayawani this way, Unatafiti nani ashinde!!.. UTAFITI.. au UBASHIRI?.. kwani utafiti si uchunguzi wa jambo ili kupata suluhu au tiba kwa jambo husika, sasa unapotafiti nani ashinde manake nini hasa.. mbali na maana hii ya Utafiti, watu hawa wamekuwa wakikiuka misingi ya haki-lindo ya mwananchi, ni TABIA MBAYA SANA
Kila mwananchi wanayekutana nae kwanza wao wanajitambulisha ni akina nani na lengo lao ni nini, kisha wanamnanga mwananchi ajielezee na yeye ni nani(wanaandika), anatokea wapi (wanaandika), kadi yake ya kupigia kura kama anayo ni namba ngapi(wanaandika) na ikiwezekana wanamuuliza hadi vitambulisho vyake vingne na wanaviorodhesha vyote, hatimae ndipo wanamnanga atoe maoni yake nani atashinda kwenye kinyan’ganyiro hicho. Hali hii huwatisha wananchi wengi na wengi huwa hawataji hasa mwelekeo wao kwa kuhofia madhara ambayo wanaweza wakayapata baada au kabla ya Uchaguzi.
Rai yangu mtindo huu wa tafiti (za Kikampeni hasa za kwetu TZ) zipigwe marufuku kabisa kwa sababu kuu tatu.
1. Ingawa mwananchi halazimishwi kutoa maoni yake ila kwa mlolongo wa utambulisho anaoutoa ni lazima awajibike kwenye tafiti husika.
2. Wananchi wananyang’anywa uhuru wa kujieleza kwa sababu mifano miwili.. mama mmoja alipohojiwa alisema “mimi ilibidi iseme itashinda CCM kwa sababu nikisema chama chochote cha upinzani sijui wangenifanya nini vijana wale, naskia unaweza kuchomewa hata nyumba yako” kijana mwingine aliyevaa kilemba kinachoashiria yeye ni kutoka chama cha upinzani, alipohojiwa kwa hofu alijibu haraka haraka, “itashinda CCM”. Na baada ya watafiti hao kupita akawa anawasimulia wenzake kwamba hao ndio usalama wa taifa wanasaka CHADEMA wawamalize. Kuna watu wengi sana wameathirika na kadhia hii ya hawa wanaojiita watafiti ambao huwatumia vijana wadogowadogo ambao huonekana kama makachero flani kutoka kambi zetu...
3. Wananchi wanaopitiwa na watafiti hao, hujikuta wakilazimika kupigi kura chama kile walichokitamka mbele ya watafiti hao kwa sababu wasipokipigia kura hawajui nini kitatokea baada ya wasifu wao kuchukuliwa na Watafiti hao. Hii ni namna ya kunyonga uhuru wa mwananchi wa kupiga Kura.
Taifa letu lina uhaba mkuwa wa tafiti hasa za mazao ya chakula na biashara, tafiti za madawa hasa baada ya kugundua dawa nyingi zinaingizwa nchini kwetu kama majaribio mfano Chanjo wanazochanjwa wanafunzi wetu ni za kujaribishia ndio maana wengi hupata umauti na madhara makubwa kutokana na chanjo hizo labda ufanyike utafiti kuona ni watu wa group gani la damu wapate chanjo ipi na si kukurupuka tu kukimbilia kwenye tafiti za kikampeni ukiacha watu wakifa. vilevile kunai ile tafiti a sindano ya kinga kuhusu magonjwa ambukizi ikiwemo HIV kwamba ukishachomwa ile sindano mwanetu unapitiwa tu chochote na huambukizwi wala nini.. sijui imefikia wapi , kwa mara ya mwisho tulisikia wanajeshi kadhaa walichanjwa .. hatufaham zaidi. Nadhani kuna tafiti nyinginyingi zinazohitajika nchini, kwenye elimu ndio usiseme watutafitie kwanini mwaka juzi (2010) hakukuwa na “A” ya Kiswahili kwenye matokeo ya kidato cha nne(NECTA)wakati ambapo Kiswahili ndio lugha hii hii ya kwetu iweje iwe Ngumu kiasi kwamba taifa zima hakuna A ya somo hilo. Nadhani tafiti ni nyingi sana hasa nchini kwetu sasa kwanini kuwekeza kwenye tafiti za kisiasa zenye malengo ya kuwachanganya wananchi maskini ya mungu hawa ambao welewa wa kuchanganua mambo kwao si mkubwa sana, wakitishwa kidogo wananywea...nadhani nyie si-mbioni, rede-T na hizi za kikwetu..nadhani data mmeipata..
Kwamba CUF itashinda kwa asilimia kadhaa au CDM au CCM vinawahusu nini ninyi na UBASHIRI WENU, ambao mwisho wa huo UBASHIRI wa KIKAMPENI mnaacha uadui, utengano, chuki na kuwachanganya wananchi. Ni uhaini kumchanganya mtanzania kwenye matumizi halali ya haki yake. TAFADHALI fanyeni tafiti za KISIASA sio za KIKAMPENI.. ni TABIA MBAYA IPIGWE MARUFUKU.
 
Vip ww pia ni mtafiti...mbona hujatupa mtoke ya utafiti wako..??



napita tu
 
Wameajiriwa na ******* ili walete tabiri za uongo ili wapete kuongeza vigezo vya kuchakachua kura. Ila kwa hapo Alumeru Msh hawatavua dafu!!!
 
Hizo ni tafiti uchwara mimi naziita. Hazina msingi na wanaojiita waafiti hufanya kitu kinachoitwa leading questions jambo ambalo linapelekea matokeo yasiyo sahihi.

Halafu uelewa wa watafiti still ni questionable kwa sababu mtu anaibuka tu kusema tu CCM au CDM itashinda kwa asilimia fulani.

Kitu kingine katika tafiti yako ni uhuru wa tume ya uchaguzi. Wao wanabase kwa mpiga kura bila kuangalia external influence ambazo zinapigiwa kelele kila kukicha.

Ni imani yangu hakuna asiyejua CCM itashindwa Arumeru kihalali lakini inachojitahidi NI KUTOSHINDWA TENA KUIBA KURA. KWA TAFSIRI NYEPESI IKISHINDWA KUCHAKACHUA INAJUA WAZI ITAKWA IMESHINDWA MAANA KWENYE BOX LA KURA beyond resonable doubt imeshashindwa.
 
Wana Jf.
Hilo hata mimi limenikuta,wao wanataka kujua ni nani anamwelekeo wa chadema ili ikibidi
hata waondoe jina lake kwenye orodha itakayobandikwa siku ya kupiga kura.Wamepita
wanatangaza kuwa majina yatabandikwa siku hiyo hiyo asubuhi badala ya siku saba kabla
ya uchaguzi kama ilivyo ktk sheria za uchaguzi.Hii yote ni ili mpiga kura atakayekosa jina
lake asiwe na muda wa kufuatilia.Huu si wizi?
 
TABIA MBAYA SANA

Kuna wanadam wana akili zilizochoka kweli kweli hawa wenye mashirika ya Tafiti pale wanapofanya tafiti za Kikampeni(sio kisiasa)..

Kwa mujibu wa maelezo niliyoyapata kutoka kwa wananchi mbalimbali hapa Arumeru mashariki, wakati ambapo mbio za kampeni zikiendelea, kuna watu wemevaa vaa vifulana na kujitambulisha kwa wananchi kama wakala kutoka mashirika ya Utafiti. Na wanatafiti nani atashinda kwenye kinyan’ganyiro cha Ubunge Jimboni humo.

Mbona akili hizi zingine za kihayawani this way, Unatafiti nani ashinde!!.. UTAFITI.. au UBASHIRI?.. kwani utafiti si uchunguzi wa jambo ili kupata suluhu au tiba kwa jambo husika, sasa unapotafiti nani ashinde manake nini hasa.. mbali na maana hii ya Utafiti, watu hawa wamekuwa wakikiuka misingi ya haki-lindo ya mwananchi, ni TABIA
MBAYA SANA

Kila mwananchi wanayekutana nae kwanza wao wanajitambulisha ni akina nani na lengo lao ni nini, kisha wanamnanga mwananchi ajielezee na yeye ni nani(wanaandika), anatokea wapi (wanaandika), kadi yake ya kupigia kura kama anayo ni namba ngapi(wanaandika) na ikiwezekana wanamuuliza hadi vitambulisho vyake vingne na wanaviorodhesha vyote, hatimae ndipo wanamnanga atoe maoni yake nani atashinda kwenye kinyan’ganyiro hicho. Hali hii huwatisha wananchi wengi na wengi huwa hawataji hasa mwelekeo wao kwa kuhofia madhara ambayo wanaweza wakayapata baada au kabla ya Uchaguzi.

Rai yangu mtindo huu wa tafiti (za Kikampeni hasa za kwetu TZ) zipigwe marufuku kabisa kwa sababu kuu tatu.

1. Ingawa mwananchi halazimishwi kutoa maoni yake ila kwa mlolongo wa utambulisho anaoutoa ni lazima awajibike kwenye tafiti husika.

2. Wananchi wananyang’anywa uhuru wa kujieleza kwa sababu mifano miwili.. mama mmoja alipohojiwa alisema “mimi ilibidi iseme itashinda CCM kwa sababu nikisema chama chochote cha upinzani sijui wangenifanya nini vijana wale, naskia unaweza kuchomewa hata nyumba yako” kijana mwingine aliyevaa kilemba kinachoashiria yeye ni kutoka chama cha upinzani, alipohojiwa kwa hofu alijibu haraka haraka, “itashinda CCM”. Na baada ya watafiti hao kupita akawa anawasimulia wenzake kwamba hao ndio usalama wa taifa wanasaka CHADEMA wawamalize. Kuna watu wengi sana wameathirika na kadhia hii ya hawa wanaojiita watafiti ambao huwatumia vijana wadogowadogo ambao huonekana kama makachero flani kutoka kambi zetu...

3. Wananchi wanaopitiwa na watafiti hao, hujikuta wakilazimika kupigi kura chama kile walichokitamka mbele ya watafiti hao kwa sababu wasipokipigia kura hawajui nini kitatokea baada ya wasifu wao kuchukuliwa na Watafiti hao. Hii ni namna ya kunyonga uhuru wa mwananchi wa kupiga Kura.

Taifa letu lina uhaba mkuwa wa tafiti hasa za mazao ya chakula na biashara, tafiti za madawa hasa baada ya kugundua dawa nyingi zinaingizwa nchini kwetu kama majaribio mfano Chanjo wanazochanjwa wanafunzi wetu ni za kujaribishia ndio maana wengi hupata umauti na madhara makubwa kutokana na chanjo hizo labda ufanyike utafiti kuona ni watu wa group gani la damu wapate chanjo ipi na si kukurupuka tu kukimbilia kwenye tafiti za kikampeni ukiacha watu wakifa.

vilevile kunai ile tafiti a sindano ya kinga kuhusu magonjwa ambukizi ikiwemo HIV kwamba ukishachomwa ile sindano mwanetu unapitiwa tu chochote na huambukizwi wala nini.. sijui imefikia wapi , kwa mara ya mwisho tulisikia wanajeshi kadhaa walichanjwa .. hatufaham zaidi. Nadhani kuna tafiti nyinginyingi zinazohitajika nchini, kwenye elimu ndio usiseme watutafitie kwanini mwaka juzi (2010) hakukuwa na “A” ya Kiswahili kwenye matokeo ya kidato cha nne(NECTA)wakati ambapo Kiswahili ndio lugha hii hii ya kwetu iweje iwe Ngumu kiasi kwamba taifa zima hakuna A ya somo hilo. Nadhani tafiti ni nyingi sana hasa nchini kwetu sasa kwanini kuwekeza kwenye tafiti za kisiasa zenye malengo ya kuwachanganya wananchi maskini ya mungu hawa ambao welewa wa kuchanganua mambo kwao si mkubwa sana, wakitishwa kidogo wananywea...nadhani nyie si-mbioni, rede-T na hizi za kikwetu..nadhani data mmeipata..

Kwamba CUF itashinda kwa asilimia kadhaa au CDM au CCM vinawahusu nini ninyi na UBASHIRI WENU, ambao mwisho wa huo UBASHIRI wa KIKAMPENI mnaacha uadui, utengano, chuki na kuwachanganya wananchi. Ni uhaini kumchanganya mtanzania kwenye matumizi halali ya haki yake. TAFADHALI fanyeni tafiti za KISIASA sio za KIKAMPENI.. ni TABIA MBAYA IPIGWE MARUFUKU.
 
Back
Top Bottom