Nteko Vano
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 434
- 111
Saa za ukombozi zitaanzia Arumeru. Ni wakati muafaka kabisa kwakuwa serikali yetu inafanya mambo bila kufikiria na kwa manufaa ya chama chake hususan matukio yanayotokea huko Arumeru na tetesi tunazozipata kuwa kwa kushirikiana na tume wanataka kuchakachua uchaguzi... Nasema saa za ukombozi zinawadia, Arusha ndio zitaanzia harakati hizo.
Soma hapo chini kauli za Dk. Slaa
Dk. Slaa ametoa masaa 24 ya kukamatwa viongozi wa CCM waliohusika katika utekaji nyara na utesaji wa kiongozi mmojawapo wa CDM. Amefika mbali na kusema uvumilivu haupo tena na hawatavumilia kuona unyanyasaji kwa wananchi na wana CDM, wizi wa kura au uchakuaji unaendelea kama walivyofanyiwa katika majimbo mengine.
"Dk. Slaa anasema.....
"Hapa Arumeru itakuwa mwisho…Kiteto watu wangu walipigiwa kituoni na kuumizwa vibaya, kituo kikuu cha polisi, Biharamulo pia hivyo hivyo….jua sasa litaamkia na kushukia Arumeru Mashariki…nataka ndani ya masaa 24 viongozi wa CCM wakamatwe................. tutauona mwisho hapa Arumeru Mashariki," alisema Dk. Slaa.
Source: Tanzania daima
Soma hapo chini kauli za Dk. Slaa
Dk. Slaa ametoa masaa 24 ya kukamatwa viongozi wa CCM waliohusika katika utekaji nyara na utesaji wa kiongozi mmojawapo wa CDM. Amefika mbali na kusema uvumilivu haupo tena na hawatavumilia kuona unyanyasaji kwa wananchi na wana CDM, wizi wa kura au uchakuaji unaendelea kama walivyofanyiwa katika majimbo mengine.
"Dk. Slaa anasema.....
"Hapa Arumeru itakuwa mwisho…Kiteto watu wangu walipigiwa kituoni na kuumizwa vibaya, kituo kikuu cha polisi, Biharamulo pia hivyo hivyo….jua sasa litaamkia na kushukia Arumeru Mashariki…nataka ndani ya masaa 24 viongozi wa CCM wakamatwe................. tutauona mwisho hapa Arumeru Mashariki," alisema Dk. Slaa.
Source: Tanzania daima