OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,344
MBIO za Uchaguzi Mdogo wa Arumeru Mashariki, zimeendelea kushika kasi baada ya makada zaidi wa CCM akiwamo Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa Arusha, Elishilia Kaaya, kuchukua fomu kuomba kuteuliwa na chama hicho kuwania nafasi hiyo.
Licha ya Kaaya ambaye ni mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), kada mwingine wa CCM waliochukua fomu hizo jana ni Rais wa Mtandao wa Maendeleo ya Vijana nchini (YDN), Elipokea Urio na Elirehema Kaaya, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza.
Wagombea hao walikabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru, Edson Lihweuli.
Wakati CCM wakijitokeza kuchukua fomu hizo, pia wanachama wa Chadema amabo ni Joshua Nassari, Samwel Shami, Francis Tembo na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Arumeru (Bawacha), Anna Mwagirwa, wanafanya idadi ya watu saba kujitokeza kuwania kiti hicho.
Akitangaza uamuzi huo jana, Urio alisema anataraji kuchukua fomu Jumamosi wiki hii kwa lengo la kuomba ridhaa ya chama chake kuipeperusha bendera katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika siku chache zijazo.
Wakati vyama CCM na Chadema vikiendelea kupiga mbizi, Chama cha NCCR- Mageuzi hakijafanya uamuzi iwapo kishiriki au la.
Katibu mkuu wa chama hicho, Samwel Ruhuza, alisema wametuma ujumbe maalumu kwenda jimboni humo kufanya utafiti wa awali kujua kama kinaweza kumsimamisha mgombea.
Sisi tumetuma task force (kikosi kazi) Siku zote tungependa ushirikiano na wenzetu, lakini yote hayo katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki yanategemea ripoti itakayoletwa na timu ya wataalamu wetu walioko katika jimbo hilo kwa sasa, alisema Ruhuza.
Alisema kazi inayofanywa na tume hiyo maalamu ya NCCR-Mageuzi, ni kufanya utafiti kujua kiwango cha kukubalika kwa chama hicho na kuona mtandao wa vyama vingine kikiwamo CCM na nafasi ya ushindi kwa upinzani.Tunaangalia vitu vingi katika hili,mtandao wa chama chetu, vyote vya siasa kiwango cha kukubalika kwa wagombea wao na wetu na nafasi ya ushindi kwa upinzani, hatua hiyo ndiyo itakayotufanya tuamue kusimamisha mgombea au kuunga mkono chama cha upinzani,alisema Ruhuza.
Kuhusu ushirikiano na Chadema, Ruhuza alifafanua kuwa utategemea ripoti hiyo inayotarajia kukamilika wakati wowote na kutolewa kwa umma.
Kwa sasa ni mapema mno kutangaza kuunga mkono chama chochote katika uchaguzi huo au kutangaza kusimamisha mgombea, tunaweza kufanya hivyo kumbe mgombea kupitia chama chetu anakubalika zaidi ama tunaweza kusimamisha kumbe wa wenzetu ni mzuri,alisema Ruhuza.
Licha ya Kaaya ambaye ni mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC), kada mwingine wa CCM waliochukua fomu hizo jana ni Rais wa Mtandao wa Maendeleo ya Vijana nchini (YDN), Elipokea Urio na Elirehema Kaaya, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza.
Wagombea hao walikabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru, Edson Lihweuli.
Wakati CCM wakijitokeza kuchukua fomu hizo, pia wanachama wa Chadema amabo ni Joshua Nassari, Samwel Shami, Francis Tembo na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Arumeru (Bawacha), Anna Mwagirwa, wanafanya idadi ya watu saba kujitokeza kuwania kiti hicho.
Akitangaza uamuzi huo jana, Urio alisema anataraji kuchukua fomu Jumamosi wiki hii kwa lengo la kuomba ridhaa ya chama chake kuipeperusha bendera katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika siku chache zijazo.
Wakati vyama CCM na Chadema vikiendelea kupiga mbizi, Chama cha NCCR- Mageuzi hakijafanya uamuzi iwapo kishiriki au la.
Katibu mkuu wa chama hicho, Samwel Ruhuza, alisema wametuma ujumbe maalumu kwenda jimboni humo kufanya utafiti wa awali kujua kama kinaweza kumsimamisha mgombea.
Sisi tumetuma task force (kikosi kazi) Siku zote tungependa ushirikiano na wenzetu, lakini yote hayo katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki yanategemea ripoti itakayoletwa na timu ya wataalamu wetu walioko katika jimbo hilo kwa sasa, alisema Ruhuza.
Alisema kazi inayofanywa na tume hiyo maalamu ya NCCR-Mageuzi, ni kufanya utafiti kujua kiwango cha kukubalika kwa chama hicho na kuona mtandao wa vyama vingine kikiwamo CCM na nafasi ya ushindi kwa upinzani.Tunaangalia vitu vingi katika hili,mtandao wa chama chetu, vyote vya siasa kiwango cha kukubalika kwa wagombea wao na wetu na nafasi ya ushindi kwa upinzani, hatua hiyo ndiyo itakayotufanya tuamue kusimamisha mgombea au kuunga mkono chama cha upinzani,alisema Ruhuza.
Kuhusu ushirikiano na Chadema, Ruhuza alifafanua kuwa utategemea ripoti hiyo inayotarajia kukamilika wakati wowote na kutolewa kwa umma.
Kwa sasa ni mapema mno kutangaza kuunga mkono chama chochote katika uchaguzi huo au kutangaza kusimamisha mgombea, tunaweza kufanya hivyo kumbe mgombea kupitia chama chetu anakubalika zaidi ama tunaweza kusimamisha kumbe wa wenzetu ni mzuri,alisema Ruhuza.