Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Defence sio mbovu lakini bado haipo sawa, wanapitika kirahisi. Halafu ukiwapgia mipira mirefu kuzuia kwa tabu sana.
Hiyo ni kwasababu ya midfielder sio Defence hili nimewahi kulisema Chelsea haina midfielder anaeweza kunusa hatari kama Caicedo kitu ambacho kimeshindwa kufanywa na Lavia na James
 
Ubaya wa defence huko wapi sema ni vile haukuangalia mpira Sanchez mguuni ni mbovu na kudaka napo ana makosa yake mipira ansyopiga sio sahihi ndio maana anaiweka team kwenye hatari lakini defenders unaona kazi wanaifanya
Nimeangalia highlights

Goli lao la kwanza la Fulham mtu aliyepiga shuti alikua amefanya run ya ndani ya box huku akiwa peke yake.

Akaweza kuupokea mpira na kujiandaa na kuweza kupiga shuti huku defense yote ikiwa ipo mbali naye. Zamani nilikua nasema Cucurella ni mbovu kwakua hizi ndiyo zilikua mistakes zake.

Goli la pili, kipa kapigiwa shuti katema miguuni kwa adui ambaye alikua na beki wenu ila akachelewa kuweka mguu jamaa akascore.

Naona rating ya colwill kwenye hiyo game ipo chini kuliko wenzake. Notice kwamba hata Calum alijaribu back 3 alivyoachiwa timu na mlikua mnafungwa.

Tuendelee kucheki mechi tujionee
 
Nimefurahi kuona Uzi spesheli wa Asenali sasa ndio unaotumiwa kujadili timu zingine zote pale England.

Hii ndiyo kusema kuwa kwa sasa Arsenal ndiye baba wa mababa pale EPL

Tunazidi kuwakaribisha wapenda soka katika uzi huu.
 
BRUNO FERNANDES ni player of the season.
Wapiga kura ni wachezaji tu, sio mashabiki Wala waandishi wa habari
Haiitaki kuelezea sana jinsi alivyostahili alifanya kazi kubwa msimu uliopita.
Class yake ni permanent, msimu huu najua atatufaa sana na tutakuwa bora zaidi coz tunawachezaji wazuri

Hope tutakuwa mabingwa au nafasi ya pili.
Arteta anajua mpizani wake ni carrick tu, lkn nyie mashabiki wenye chuki mnatutoa mpaka top four πŸ˜…πŸ˜… kisa game ya ufunguzi
Ni kama hakuna atakaefungwa
 
1. Una beki bora ya kuizuia arsenal, man city au Brighton?

2. Una kiungo kinachoeleweka ambacho kinaweza ku-battle na arsenal?

3. Una forward ya kutishia timu zenye beki nzuri kama arsenal?
Soma comment yangu kuhusu team yenu utajijibu hayo maswali
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…