Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kitakwimu ukimuangalia Kai utasema kwamba jamaa mbona yuko sawa. Why? Coz kwa sasa Arsenal inasemekana inamtaka Cunha, but namba zao hazipishani sana kwenye assists na magoli.

Hii debate niliikuta Reddit. Mmoja akaargue kwa namba ya Cunha, jinsi Wolves wameanza msimu na waliomzunguka kumtengenezea nafasi ni sawa na waliomzunguka Kai?

So in all honesty, Kai hatoi msaada ambao unatarajia ST akupe na ukubwa wa mshahara wake.
 
Arsenal sas hivi kuiangalia hadi inachosha.

Wolves wako very open, with a lot of mistakes but still tunashindwa kufunga.
 
RED CAAAAARD

Pambaf zenu. Na leo mnakalia mti tena.
 
Nafikiri hii red imekuja kutokana na DOGSO lakini sioni ni kivipi ile inatakiwa iwe red card kwakua kwa distance ya Wolves hadi golini kwa Arsenal ni vipi inaweza kujihakikishia lile litakua goli?

Mchezaji mmoja akikosekana kwa Arsenal inakua msiba kwakua tunacheza kwa pattern, hata mchezaji wetu mwenye speed akipata mpira anasubiri wenzake waje wakamilishe pattern.

Ndiyo maana unashangaa hadi tunaenda mbele tunakuta wapinzani wameshajipanga. So akimiss mmoja tatizo linaongezeka.
 
Sub za maana nje ni calafiori, zin na kiwior

Arteta inabidi aje na plan B
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…