Flano
JF-Expert Member
- Aug 7, 2019
- 5,844
- 16,298
Kaka mimi sizungumzii ubingwa wa Epl wala Uefa pekee, ni kweli sio kazi rahisi kupata ubingwa wa hayo makombe mawili, ila kwa ubora wa Arsenal hii mmeshindwa Epl na Uefa basi mngebeba hata hivyo vikombe vidogo vya FA na Carabao.Hivi unaujua ubingwa wa uingereza ulivyo tafu? Unadhani kushinda na klop na pep ambao hata ulaya watu wanakalishwa? Kufikisha pointi 80 ligi kuu sio poa
Hata wajukuu zenu siku mkija kuwahadithia kua Arsenal ya 2022/2023 na 2023/2024 ilikua ni ya moto kwelikweli, wakiwauliza ilishinda kombe gani? halafu mkawaambia haikushinda kombe lolote misimu yote miwili walimaliza mikono mitupu sidhani kama watawaelewa.