Arsenal (The Gunners) | Special Thread

🤣🤣🤣 Sio kwa lengo baya bali ni katika kukumbushana tu maana binaadamu tumeumbiwa kusahau, miaka 8 iliyopita Bayern Munich ndie alie wafungisha virago kwenye michuano ya Uefa kwa fedheha ya kuwagonga goli 10.
Tunashukuru kwa taarifa mkuu...umeshashiba tambi unakuja kutufanyia Fujo sasa
 
Tunashukuru kwa taarifa mkuu...umeshashiba tambi unakuja kutufanyia Fujo sasa
Mkuu ni tambi na maharage mixer lile kombe kubwa la uji.
Ila kuweni makini ndugu zangu huyu Bayern akikufunga ni kama vile anakuachia na laana kabisa ya haya mashindano, ingawa kweli tembo yuko mtini ila hatutaki tuwakose kwenye hii michuano kwa miaka 8 tena mingine ijayo.
 
Tunatakiwa kulipa kisasi dhidi ya Barcelona siku ya fainali.

Naombea tukutane na Barcelona.

Uhuni walioufanya 2006, hatujausahau. Barcelona timu ya majizi sana.

Japo ili kufika hapo tutahitaji kupanda milima mirefu kwelikweli. Uzuri Arsenal hii inaweza kupambana na timu yoyote na ikapata matokeo.
 
Sisi hatuna msalie mtume safari hii...tutawadunda kama Ngoma wale watu
 
Kati ya Madrid na City ya sasa ni nafuu kukutana na Madrid.

Bayern ina beki Eric Dier. Ina kocha Tuchel.

Timu nyingine ambayo ilikua inatutishia historia ilikua Porto. Ni miongoni mwa timu ambazo zimemaster kufanya mid na low block.

Kitakwimu ni rahisi kupata goli ukicheza na Madrid/ Bayern kuliko Porto. Walipotupiga 1 wote tukaona historia iko upande wetu.

Ikawa upande wetu ila kwa dakika 30 zaidi na Raya kuhusika kutuokoa.

Arsenal ni underdog kwa yeyote atakayekutana naye CL na siyo kwa ajili ya quality ya wachezaji ila ni kwaajili ya uzoefu wa kua humo CL.

Arteta aliwazia mwaka wa kwanza wa CL uwe ni kutembea kisha unaofuata kuchukua. Kutokana na jinsi muda ulivyoenda mashabiki tunaona tunastahili kombe, mwaka ujao be damned.
 
Njia imekaa vzr ,tukifika fainal inakuwa rahisi ,

Bayern anakuja Emirates,amefungiwa kuja na mashabiki,kwahiyo Emirates itajazwa na mashabiki 60,000 wote wa Arsenal


Bayern ana ego ya kupishana ,

Tukifika Fainal itakuwa kazi ngumu tumeifanya nusu ,
 
Tuchel: "We now face one of the best teams in Europe."

Neuer: "They're a very strong team with a very good spirit"

Müller: "Arsenal are a team who'll give us two thrilling games"

Eric Dier: "Arsenal have a young team who are performing very well."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…