Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Taarifa ni kwamba Hitimisho la FA kuhusu comment ya Mikel Arteta kwa waamuzi kwenye mechi yetu dhidi ya Newcastle lipo mbioni kutolewa. Na tetesi ni kwamba wanavizia ili mechi yetu dhidi ya Liverpool asiwepo kwenye touchline.
 
Hivi kuna mtu anakumbuka kipindi kile mzee Wenger alifungiwa kuwa kwenye touchline, sababu ilikuwa ni nini? na alifungiwa mechi ngapi?
 
Yes. Hicho ndicho nasema. Nilishaulizaa hili la je bodi inaweza kuitamani pesa na kumsukuma Arteta atumie kikosi bora badala ya benchi? Aachane na hiyo 2.8. Asirisk injuries na uchovu wakati tunaafari ya kurudi kileleni na kupambania EPL ambayo ni mbio ndefu kisa hii 2.8m euros za mechi moja. Tukichosha au kuumiza wachezaji halafu tupoteze kwa akina Brighton na wengine, timu itapoteza momentum, morale na confidence. Ikitokea hivyo tutahangaika sana kupambania ubingwa na nafasi ya 4 bora amayo itatugharimu pesa nyingi zaidi. Awape vijana jukumu la kuipambania.

Context nyinine ni superstar kama Rice ni 100m pounds. 2.8M euros hatuwezi kusema tunaihitaji kujazia kumpata mchezaji wa 100m au hata 50m. Tuache tamaa zenye uwezekano wa kuzaa hasara.
 
Taarifa ni kwamba Hitimisho la FA kuhusu comment ya Mikel Arteta kwa waamuzi kwenye mechi yetu dhidi ya Newcastle lipo mbioni kutolewa. Na tetesi ni kwamba wanavizia ili mechi yetu dhidi ya Liverpool asiwepo kwenye touchline.
Wanatuandama sana wale wapuuzi. Ila ndiyo maisha yetu EPL na wengine hawawezi kuelewa. Tunalazimika kuruka pale wengine wanapoendesha, na kukimbia pale wengine wanapotembea.
 
Nimejitahidi Sana lakini nimeshindwa
Labda wenzangu mniambie mnawezaje?
Ni kumchukulia poa tu na imani zake. Yeye si ana facts kwamba Gordon na Wilson wanafunga kuliko Saka na Jesus na kwamba hatujauza wachezaji zaidi ya 50m? Tulikuwa na wachezaji wanalipwa 350k kwa wiki, tukawaondoa kwenye timu. Haya mambo ya kuosha gari kwa bia timu yake haiwezi kufanya. Tuupokee tu wivu wake.
 
Labyrinth 84 akiingia humu hoja zake zinakua na facts kabisa, yaani yule jamaa hua hacomments bila ya kua na evidence za kutosha, sasa mtu wa namna hiyo unapata wapi hoja za kumjibu zaidi ya kumtukana tu na kumpiga marufuku asikuquote?
 
Arsenal inajulikana kuwa ina tatizo ndani ya suluhu na suluhu ndani ya tatizo. Ila rafiki yetu naona analileta hilo suala kama vile kwetu ni tatizo kubwa sana au kama linatuathiri zaidi ya kiasi, wakati siyo hivyo. Tunakuwa maeneo ya juu kwenye goal difference ila siyo kuongoza goal difference (Unaweza kuta tutapitwa na timu 1-3). Unakuta tumefunga magoli mengi lakini wachezaji wetu hawafikishi hata magoli 20 kila mmoja, huku timu za chini yetu zinawachezaji wenye magoli zaidi ya wakwetu. Lakini hizo timu hazifungi magoli mengi kuliko sisi. Tumeshawahi kuwa na Aubameyang aliyehinda kiatu na Mane na Salah ila tuliishia wapi?

Hatusemi hatutaki wafungaji wa magoli 20+, of course tunataka na kila siku unasikia tunahusishwa nao. Ila ni wazi pia kuwa kumetengenezwa mfumo wa kufanya tufunge mengi na kushinda zaidi ya hao wenye 20+ goal strikers ila tunajua bado haitoshi. Nadhani Nketiah labda na Saka kama ikosei ndiyo wana hat-trick kwetu, ila kuna timu zimepiwa 5-0, 6-0. Lens alipiwa 6-0 hapa juzi juzi na tulikuwa na wafungaji 6, yaani nusu ya timu imefunga. Tunataka tufunge zaidi kwa system hii hii, kwa kuboresha wafungaji na system. Inawezekena yeye hajaelewa hili. Ndiyo maana hata watu walimuuliza nani anamtaka Wilson ama Isak? Na akaambiwa kuwa kiukweli hao jamaa wakija Arsenal wakimkuta Jesus yuko fit, hawamuweki bench. Mfumo. Theory yetu ni kwamba Arteta atakuwa radhi akomae kuboresha ufungaji wa Jesus kuliko kumweka bench kwa Isak au Wilson.
 
Yule kijana ni kama amechanganyikiwa hivi🤠🤠🤠...muelewesheni taratibu ila mwambieni atafute kikundi kingine cha kushabikia...kile kitamtia wazimu
 
Anakuambia saka ni Bora kuliko Gordon

Unaamua utoke jf uingie LinkedIn kutafuta michongo tu
Typing error

Ilikua ni saka si Bora kuliko Gordon.

Sasa huyo Gordon anamfikia vipi saka
Saka ata akiamua kucheza mguu mmoja Gordon hafui dafu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…