Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kuna kitu wazungu wanaita ANGLED PRESSING , ndicho alichofanya havertz vs City , why?

Buildup ya mancity inapoanza mlengwa mkuu ni John stones anayekuwa kiungo wa uongo aliye free, nafasi yake ya beki anaichukua GK , hivo Stones akipata mpira eneo la Midfield tayari mnakuwa mmefanyiwa overload na matokeo yake mnapigwa kirahisi

Ili kuutoka mtego huu , Kai ndiye alikuwa muhusika mkuu ,alikuwa anafanya ANGLED PRESS ya kulazimisha GK wa mancity ambaye anakuwa katikati ya Ma CB wawili apeleke mpira upande wa kushoto , na sio kumpa Stones ambaye Mara nyingi anakuwa kasogea eneo la kiungo

Anapoenda kufanya Press anakuwa na timing ya kuhakikisha Saka ameshajiandaa kumpress Beki wa kushoto wa mancity ambaye anapokea mpira ,

Mbinu hii ilisababisha mancity wacheze mpira mwingi eneo lao tu ,nakusababisha Hadi dk za 60+ wasiwe na On target hata moja


 
Martinelli ana advantage moja. Jamaa ni mchapa kazi, msumbufu na ana pumzi. Utamkuta nyuma anakaba na wapinzani wakifanya turnover unamkuta kashakimbia mbele kumalizia through ball. Na anaweza kufanya hivyo mechi nzima hivyo anawasaidia wachezaji wenzake kuvuta pumzi kidogo wakati wa Hali ngumu. Ni kama Kante wa Leicester au Ramirez wa Chelsea ila yeye ni forward.

Pia ni mshapu kwenye kupiga shots na huwa hazidishi touches sana Ili akae vizuri apige. Ni wale wachezaji ambao beki akifikiri atasogeza mpira kidogo na mguu wa kushoto Ili apige na kulia, anashangaa jamaa keshashoot na wa kushoto. Makipa pia wanajikutaga washafungwa na jamaa Kwa style hii.
 
Arsenal are seeking to make at least one more significant sale in order to bring in a number six, as Mikel Arteta seeks to add more variety to his midfield.

The issue is that there aren’t many midfielders of that profile available for purchase at the moment. [@MiguelDelaney]
 
Battle ya Martinelli na Trossard kuna mda nahisi Arteta anapata tabu kuamua nani aanze, maana Trossard anatisha kushoto anaweka kulia hatari sana
 
Battle ya Martinelli na Trossard kuna mda nahisi Arteta anapata tabu kuamua nani aanze, maana Trossard anatisha kushoto anaweka kulia hatari sanaView attachment 2713422
Arsenal Pre-season goals & assists


Goals Assists
Saka: 2 3
Trossard: 3 1
Jesus: 1 2
Havertz: 2 0
Martinelli: 1 1
Odegaard: 0 2
Nketiah: 1 0
F. Vieira: 1 0
Tierney: 0 1
Jorginho: 1 0
Marquinhos: 1 1
White: 0 1

Vita ni nzito sana pale Emirates msimu huu..
 
With Jorginho, Mohamed Elneny and Thomas Partey all not getting any younger, there is a clear route into the Arsenal first-team for Charlie Patino if he wants it in the coming years.

That’s most likely what Mikel Arteta explained to him with the player now happy to return to the club next season.
 
Battle ya Martinelli na Trossard kuna mda nahisi Arteta anapata tabu kuamua nani aanze, maana Trossard anatisha kushoto anaweka kulia hatari sanaView attachment 2713422
Trosaard kiukweli napenda kumuona Sana LCM , sababu ya uwezo wake wa kukaa na mpira ,kupiga miguu yote , mfano mech na mancity kafunga na Left ,huyu jamaa ndiye Carzola


Trosaard kucheza LW naona atasubiri sababu EPL inahitaji wingers viberenge angalau upande mmoja

Saka sio runner , Martinelli ni runner

So mechi nyingi zinahitaji winger runner
 
️ |
Baada ya kukutana na Mikel Arteta, Charlie Patino ameamua kwamba mustakabali wake utabaki Arsenal na kwamba yuko tayari kuhamia kwa mkopo tena, kulingana na

@FabrizioRomano.


Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 anatazamiwa kujiunga na Swansea kwa mkopo kabla ya kurejea Gunners msimu ujao.


Habari nzuri
 
Kai atatamba sana akiwa arsenal msimu huu.watu wanasema tusajili cf wa nini ? mpira wa siku hizi hautegemei mtu afanye kazi moja tu uwanjani,akitaitiwa akashindwa kufunga anakuwa mzigo kwenye mechi,angalia juzi halland kwenye mechi yetu baada ya kubawa na mabeki akakosa cha kufanya ikabid wamtoe.ila unapokuwa na mtu kama kai au G.Jesus,Hawa mechi ikiwa ngumu wanarud nyuma wanaenda kukaba,wanachukua mpira wanapiga changa adui then wanatengeneza space kwa kina ode,saka na martinell kuscore,huu ndio mpira wa kisasa,ni kitu cha ajabu kusema arsenal anahitaji cf,wakati msimu uliopita wamemaliza na goli 88,hata wakati kina henry wapo hawakuwahi kufikisha hizo goli.
 
Arsenal hope to have David Raya available for Premier League opener vs Nottingham Forest as goalkeeper undergoes medical on thursday ( today)

(@sr_collings )
Ramsdale......onana
Your browser is not able to display this video.
 
Battle ya Martinelli na Trossard kuna mda nahisi Arteta anapata tabu kuamua nani aanze, maana Trossard anatisha kushoto anaweka kulia hatari sanaView attachment 2713422
Huyu Trossard sijui nimuweke kundi la Cazorla Kwa matumizi ya miguu yote haswa kwenye shooting. Kwa mbali huwezi jua anatumia mguu gani. Martinelli ana shoot na kushoto lakini zaidi akiwa ndani ya box. Saka anashoot na kulia lakini anakuwa confident kushoot na kulia akiwa ndani ya box. Trossard hajali Yuko ndani ama nje ya box. Halafu anajua kulenga goli. Namuona akiwa na 15+ goals na 10+ assists kama tukicheza kama last season
 
Mimi nakubaliana na wewe , lakin pia hatuna tatizo kubwa la kuhitaji a CF ,tulishakuwa na lacazette ,Hakuna alichofanya

Kuna swali Ambangile aliwauliza Mashabiki wa Arsenal Kweye space siku moja wanaolalamika tusajili CF , Aliuliza huyo CF atakuwa kila mpira anapigiwa yeye tu ili afunge

Wengi wanaona Halland anafunga Sana ni sababu City Wana xG kubwa ya kutengeneza nafasi lakin pia KDB ndiye anamjulia Sana kuliko wenzie ,

Halland yule angeenda manjesta huenda angekuwa Kama Weghost tu, tumeona mechi ambazo mabeki wanamuweka mfukoni ,kurudi chini hawez ,kwenda pemben hawezi ,

Mimi naamini tutasajili CF lakin ni cariber ya Ole watikins,au Ivan Toney ,

Arsenal tuna create nafasi nyingi Sana, Juz vs city bado tulitengeneza nafasi nyingi kuliko city ,

Mfano mzuri ni Chelsea ya Tuchel Iliyotoka kubeba UCL zilipigwa kelele asajiliwe CF wapiganie EPL , akaletwa CF kwa £97m , ikafika muda akawa anagusa mpira Mara 8,na timu ikazidi kupotea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…