Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Dah... kwa structure ya league inakera namna tulivyopoteza ubingwa.
Ila kwa ubora wa city,they deserved.ingeniuma saaana kama ubingwa ungeenda kwa timu yenye ubora wa kawaida.

Kama tunahitaji kuchukua mataji siriaz hakika hatuna namna ya kulikwepa soko.we need kuingia sokoni nakuchukua watu ambao ni chaguo la kwanza.sio kila mahali tukifeli biding war tunageukia plan B.
Ili kuishinda city na kuchukua ubingwa mbele yake you need a tactical genius coach na quality players ambao wanakuja kwa pesa ya maana.

Kwa kweli mchezaji mwenye 'potential' hapana.tunahitaji ready world class players.game ya jana ya los blancos na citizens inafundisha mengi kuhusu dunia ya soka kwa sasa.we have to learn.

Kuna watu watahoji mbona inter yuko fainali kaspend kiasi gani?MUDA ni mwalimu mzuri acha aendelee kutufundisha
 
Ulivyosema Genius coach
nimemkumbuka Guardiola he is the MAN katuuzia Zinchenko and Jesus (tukasema hajitambui
)akaenda kwa Halaand na Akanji
na bado kabeba premier league
 
Lakini haiondoi ukweli juu ya mchango wa jesus na zinchenko.kitu ambacho mashabiki hamtaki kukubali ni kwamba incase of quality liverpool,chelsea walikuwa mbali na sisi.kilichotutofautisha sisi na wao ni eneo la tactics tu.kocha amefanya makubwa sana kwa anayebisha mkabidhi hichi kikosi PEP halafu uone atamaliza nafasi ya ngapi.

Kuna muda kocha hata uwe mzuri kiasi gani kama huna quality players kila eneo na wakutosha basi utateseka sana.

Nakupa hii;kama tusiposajili quality kwenye fullbacks zote,kiungo mkabaji,defined 9,kiungo mshambuliaji hasa 8 na winga ya kushoto hata baada ya miaka 2 hatutachukua ubingwa.

Epl vita na vita haswa
 
Hii City ndiyo wanafiki walikua wanatuchonganisha nayo.

Aliishindwa Ferguson, Wenger, Klopp, Mourinho wanakuja kumsakizia Arteta hata kudeal na pressure hajamaster na kikosi kipo nusu.
 
Tunamuhitaji Rice + Caicedo + Frasneda/ RCB + RW (tunahusiswa na Moussa Diaby) hapa tunaweza kushindana na Guardiola, sio Man City ni Guardiola.
 
Ubora wa Guardiola msimu huu umechangiwa na tactical masterclass kutoka kwa Mikel Arteta & RDZ. Guardiola alipokuwa Bayern aliwahi kuulizwa kama ni kocha bora duniani kwa wakati huo, alisema anachojua yeye ni mwizi wa idea, akiipenda idea yako ataiiba na kuiboresha.

Binafsi nimeona mambo mawili kwake msimu huu, matumizi ya Centre Backs wanne, 4CBs, hii idea ilianza kwa Mikel Arteta, inawezekana nyuma iliwahi fanyika, ila mimi sikuiona, mpango wa Mikel ulikuwa kutumia CBs wanne kwenye backline i.e White, Saliba, Gabriel & Lisandro Martinez. Ikumbukwe Lisandro alikukwa priority kwenye usajili wa Arsenal kabla ya Zinchenko, na role yake ni ile ile kama Zinny, anakuwa midfielder Arsenal wakiwaa na mpira anakuwa LB bila mpira. Arteta alitumia CBs wanne kwenye mechi ya nyumbani dhidi ya Liverpool (3-2), White, Saliba, Gabriel, Tomiyasu.

Guardiola alikuja na idea hii baada ya kumtoa mkopo Joao Cancelo, anawatumia Akanji, Ruben, Stones, Ake. utofauuti ni kwamba John stones anakuwa midfielder timu ikiwa na mpira, no inverted Full back, ila ni CB anayesogea mbele wakiwa na umiliki na pia kurudi kwenye majukumu yake bila mpira.

Idea ya pili ni kucheza na double pivot timu ikiwa na mpira (Stones & Rodri). RDZ anatumia idea ya double pivot kwenye build up na hajawahi kubadilika. Naelewa Guardiola huwa anatumia idea ya double pivot lakini naamini kwa sasa ameathiriwa na namna Brighton wanavyocheza, deep down kuna mfanano hapa, nilichokiona City & Brighton wanazivuta timu kwenye eneo lao then wana break that pressure thru combination & third man movements na kupelekea direct chance creation from that build up play. Fluidity kwa upande wa City & Brighton hasa kwenye build up is next to none, na mfanano wao mkubwa upo kwenye third man runs & link up. Arsenal nadhani wanahitaji more resources kwenye eneo hili, kwa sasa Brighton & City wapo dunia yao. Pep alikiri hapa juzi kuwa Brighton ni timu bora duniani kwa sasa kwenye kuanza build up. kuna kitu kajifunza hapa.

Guardiola alipokuwa bayern alikuja na idea ya sole midfielder( Organising midfielder) baada ya mtangulizi wake Jupp heynckes kuwin treble akiwa na double pivot( Javi Martinez & schweinsteiger). Guardiola aliwahi kukiri si mpenzi wa double pivot, Why? anasema akiwa mchezaji alichukia kuwa na msaidizi pembeni, why? it limited his space & his ability to anticipate the next pass. lakini kwa sasa amebadilika, anatumia double pivot.

Kama shabiki wa Arsenal naamini kwamba with the right signings( ambazo tunahusiswa nazo), next season we will be there with the best in the World.
 
"Ubora wa Guardiola msimu huu umechangiwa na tactical masterclass kutoka kwa Mikel Arteta & RDZ"

Kwa kua masterclass Mikel Arteta amechangia kwa kiasi kikubwa Ubora wa Guardiola na timu yake kwa ujumla, sisi kama mashabiki lialia wa Arsenyau tutamuomba katika hayo makombe matatu atakayobeba msimu huu atugee japo kombe moja ili na sisi Arsenyani tusiondoke mikono mitupu.
Au nasema uongo ndugu zangu????
 
Hii City ndiyo wanafiki walikua wanatuchonganisha nayo.

Aliishindwa Ferguson, Wenger, Klopp, Mourinho wanakuja kumsakizia Arteta hata kudeal na pressure hajamaster na kikosi kipo nusu.
Ila sisi mashabiki lialia wa Arsenyani si tulikubaliana kwa pamoja kua:
Ubora wa Guardiola na City yake unachangiwa kwa kiasi kikubwa na tactical masterclass kutoka kwa Mikel Arteta?
 
kwa bahati mbaya hatushindani na watoto wadogo, level za watoto tushavuka. Target ni moja tu, kushindana na Man city ya Pep Guardiola, nyie wengine mkakojoe mlale, au endeleeni kumshabikia bwana wenu awasaidie. Mwanaume Support timu yako, sio upo bize kushabikia mwanaume mwenzio akusaidie upate cha kuongea kijiweni.
 
Hizi kauli ndo zinawaponzaga sana tuna kesha hapa tuna wapiga spana Yani timu yako.

FA ilitolewa
Carabao cup ilitolewa
Ueropa league ilitolewa

Sasa fans wa arsenyani mnafukuzana na Nani nyie mapimbi.
 
Hizi kauli ndo zinawaponzaga sana tuna kesha hapa tuna wapiga spana Yani timu yako.

FA ilitolewa
Carabao cup ilitolewa
Ueropa league ilitolewa

Sasa fans wa arsenyani mnafukuzana na Nani nyie mapimbi.
FA cup & Europa? Nani anataka hivyo vikombe? ukiwa na timu nzuri huwezi kufikiria hivyo vikombe, hivyo ni kwa ajili yenu mnaojitafuta.
 
FA cup & Europa? Nani anataka hivyo vikombe? ukiwa na timu nzuri huwezi kufikiria hivyo vikombe, hivyo ni kwa ajili yenu mnaojitafuta.
Nyie wenye mmejipata msimu mzima mmetoka patupu kweli fans wa arsenyani mmedata sio bure.

Mafanikio yenu mwaka huu ni kwenda uefa tu nako mnaenda kutia aibu mnataishia makundi kwa wachezaji wenu wa mafungu mafungu.
 

World classic players hawawezi kucheza average team hilo pia weka akilini! Arteta hadaiwi chochote kwa jinsi arsenal ilivyokua inacheza kipindi cha msimu wa 2 wa unai emery it was disaster .
Ake, akanji , stones , grealish na wengine unawaona world classic players kwasababu wako kwenye timu ya kibingwa ila wangekua bado wapo aston villa, bournmouth na everton ungewaona wakawaida tu
Nikukumbushe tu martinelli kamzidi grealish goals pamoja assists, anaonekana average player kwasababu yupo loser team!! . Saka odergard na martineli wako loser team thats why wanaonekana kama wachezaji wa kawaida!
ARSENAL NI LOSER IN AND OUTSIDE OF THE PITCH ( kwenye usajili)
 

arteta msimu mzima kakomaa na formation ile ile hata sub zenyewe anabahatisha sometimes .
Refer gemu ya liver anamuingiza kiwior anamtoa odergard
halafu jorginho yupo nje alipozingua zaidii mapema kabisa unaona zinchy game ile ilimshinda kabisa kamuacha akala tobo bob akatuweka ndo anamtoa wakati tayari kashachoma. Game na soton akaanza na viera
. Huo u masterclass wa arteta sijuiii ukwapii??? Angalia approach ya genius Pep game yetu ya kwanza silva alicheza namba ngap angalia game ya bayern pep anabadilikabadilika!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…