allypipi
JF-Expert Member
- May 10, 2020
- 3,324
- 10,895
Ila arteta ni wakufukuzwa hapo Arsenal mnaitajika mpate kocha mfano wa Mourinho au Conte hatawafaa sana.Ushabiki ndivyo ulivyo. Ingawa msimu huu kiukweli ubingwa ulikuwa nje nje. Kina Arteta na timu wamezingua sana nao wanajua hilo. Kwa shabiki ni sahihi kabisa kuona ubingwa upo toka October huko na kina Mkorea na Hamis walikuwa sahihi kabisa.
Ila ndio ushabiki huo. Nyie hamjaperform vibaya msimu huu. Shida ni kuwa hamfungi sana na mmepokea vipigo vichache vikubwa na kuwapatia goal difference ya hovyo. Ila kiushabiki Lazima tuwaponde kuwa mna timu mbovu na mpira wa janja janja.
Simba hatujawapita sana msimu huu ila tumekuwa mabingwa na tunawaponda utadhani wamepona kushuka daraja.
Sisi tumesota na kukosa ubingwa kizembe na tutamaliza wa 2. Ila ukiingia humu utadhani tuko chini ya Chelsea
Inabidi muachane tu na uo mpira wa pasi pasi labda mtapata hata mafanikio ya msimu mmoja.