Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Toobiter kwenye moja na mbili
 
kuna matukio umenikumbusha hapo kati nimecheka sanaa..

washabiki wenzako wanadi mna project... hilo me sina neno tukiludi makwetu mkae mliangalie
 
Tujifunze kwa City na Liverpool
Izi kweny game 10+za mwisho form wanayokuaga nayo kwenye kila msimu ni Majini haya matimu,form wanayomaliza nayo ligi Liver ndo tungekua nayo sie kwasasa tungekua tunaongea habari zingine kabisa..
 
Kwahio unahama club au sijakuelewa

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
 
Napoli wamebeba ubingwa wao wa Serie A mwaka huu baada ya miaka 33. Huoni kama miaka mingi ya kujaribu na kufeli ndiyo itaongeza furaha na thamani ya ubingwa siku Arsenal watakayoweka mikono yao kwenye taji la EPL.
 
Mimi napenda mpira kwa ujumla wake ila naifuatilia Arsenal ndiyo maana nikiwa na nafasi naangalia mechi zote na ligi zote. Ukiwa hivi haitakusumbua kuona na kutarajia.

Kwa ligi ua Serie A Juve alipokonywa point 15 akashuka hadi nafasi ya 9 leo yupo nafasi ya pili. Sijisikii kuongeza ligi zingine lakini lakini point yangu ni kwamba kwa miaka yote timu za kariba ya Juve zinakua kwenye pressure na zinasurvive zina wachezaji wanaojua nini wafanye wanaojua umuhimu wa game hii au ile.

Arsenal ina wachezaji wawili wa hivyo Zinchenko na Jesus, hawa wengine wamekuzwa kisystem mno so system ikicollapse na wenyewe wameenda, wakati timu kama City, Juve, Bayern, system ikicollapse individual brilliance inawabeba.

Hao sasa ndiyo wachezaji wanaotakiwa kuja, wanaoweza kuwasha moto kila inapohitajika.
Nilikua nawaambia ndugu zangu wasiishikilie hoja ya bora hatupo FA au carabao au europa na city ana games nyingi kwakua kwa determined team kwa pale tulipokua muda tunacheza na sporting ilikua top four tuna uhakika nayo kwa 70% so ingekua logic kukomaa na Europa.

City ana tournaments nyingi ila ana kikosi. Watu wakawa wanatoa hoja mfu, na siyo hivyo tu ana kikosi chenye individual brilliance na yeye na kikosi chake wanaweza kudeal na pressure. Nafikiri pia udogo wa Arteta upo hapa kwenye kudeal na pressure tactically he is good ila huku kwingine ni anahitaji huu msimu na kikosi kipana zaidi.
 
Sahihi,
Kocha kwenye hili anaweza ongeza mchezaji yeyote wa zamani aliyeshinda vitu vingi ili awape uzoefu wachezaji jinsi ya kuwa calm na focused kwenye presha.
Kuna muda determination ni muhimu zaidi ya kipaji.ATTITUDE ya timu kwa kila mechi ni muhimu mno.
 
Unavyosema mchezaji kuwa matured una maana gani? Leicester city ilikua ina mchezaji gani matured?? Matured in terms of umri au uzoefu na ligi??
Uzoefu ukomavu wa akil sio watt.. Unakumbuka vzr kikosi cha Leicester ww kilivokua na watu kaz.. Wanaweza kukufunga 1 tu na goal ilo usirudishe wakadefend kama maisha yao Yana defend on it.. Uwe na watu who can get you over the line when you need it most.. Sio na watt wacheza Ps kama Arsenal.
 
Sisi ni champion bottlers Mzee. Ile season Leicester anachukua ubingwa tulikuwa tunamfukuza tukamkaribia halafu tukapotea tena akatuacha na kama points 10 kama sikosei. Last season tulihitaji sijui points 4 kwenye game nne tuingie top 4 nayo tu tukashindwa.
Sisemi kuwa ni sawa. Nishasema mara nyingi humu kuwa nina standards za juu kidogo kuliko uwezo wa timu yangu. Hivyo ikijitahidi na kuperform juu ya nilivyodhani, napongeza. Ni kama mzazi unategemea mtoto awe na ufaulu wa 90% katika somo fulani. Ila unamuona ana uwezo mdogo, yeye unategemea atapata 40%. Akija na 60% unampongeza then unampa moyo afike hiyo 90% yako

 
Ushabiki ndivyo ulivyo. Ingawa msimu huu kiukweli ubingwa ulikuwa nje nje. Kina Arteta na timu wamezingua sana nao wanajua hilo. Kwa shabiki ni sahihi kabisa kuona ubingwa upo toka October huko na kina Mkorea na Hamis walikuwa sahihi kabisa.

Ila ndio ushabiki huo. Nyie hamjaperform vibaya msimu huu. Shida ni kuwa hamfungi sana na mmepokea vipigo vichache vikubwa na kuwapatia goal difference ya hovyo. Ila kiushabiki Lazima tuwaponde kuwa mna timu mbovu na mpira wa janja janja.

Simba hatujawapita sana msimu huu ila tumekuwa mabingwa na tunawaponda utadhani wamepona kushuka daraja.

Sisi tumesota na kukosa ubingwa kizembe na tutamaliza wa 2. Ila ukiingia humu utadhani tuko chini ya Chelsea
 
Dah nimecheka sana
 
Hizo point 15 za Juventus alirudishiwa ndio maana yupo pale nafasi ya 2
 
Mwamba huyu hapa sasa.
Yaani maisha yakutie stress halafu unajipa moyo wacha nikapunguze stress kwenye burudani ya soka, unaenda zako kuishabikia mi Arsenyau na yenyewe inazidi kukutia simanzi na majonzi tu kila msimu, halafu kuna kima zinakuzuia ubaki tu hapohapo kwenye maumivu yasiyo kwisha.
Hata mke ambae umezaa nae ukiona hamna furaha kwenye ndoa unapiga chini unaenda tafuta mrembo mwingine sembuse huyo Arsenyau?
Maisha yenyewe mafupi haya jamani, nyie kina Forgotten msiwalazimishe watu wabakie sehemu inayowapa mateso na msongo wa mawazo mwisho wa siku wanaishia kujitundika kwenye kamba.
Binafsi mimi nakupongeza sana Labyrinth 84 kwa huo uwamuzi uliochukua, ni uwamuzi wa busara sana na mimi ninakuhakikishia kukuunga mkono na kukusaport kwa kuendelea kuzihamasisha hizi kima nyingine zilizobakia humu zinazoendelea kuteseka kwa misongo ya mawazo kufanya maamuzi ya busara kama uliyofanya wewe.
 
 
Labyrinth 84 hili timu limekutesa kwa miaka mingi sana Aisee, naona msimu huu umeamua rasmi kutoa nyongo zote safi sana Mkuu.
Nnahakika hata hamis77 nae anatamani sana atoe nyongo zake hapa ila kila akikumbuka jinsi alivyokua anaiaminisha hii misukule ya Arteta nafsi yake inamsuta.
 
Siku na mwambi bwana hamis77 kuwa city kikosi chake kimeshiba Cha kwenye bench kuliko Arsenal akaanza kutoa maneno ya kejeri kikowapi Sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…