Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Naona tambo zinaendelea baina ya pande zote mbili..

Anyway, nawatakia maandalizi mema leo wanangu wa The Gunners.

Japo Liverpool wanaamini wao ni favorite, ila wategemee mchezo mzuri na wa ushindani leo.

Hii ni Arsenal nyengine kabisa, mentality mpya, hakuna makosa ya kijinga kwenye back line.

Hivyo lolote linaweza kutokea.. Wasishangae tukawashangaza kama jana Leicester alivyowashangaza City!
 
Tierney vipi? Atakwepo leo!?
Sijamuona kwenye mazoezi na wenzake.. Hopefully updates za baadae wanaweza kumjumuisha.

Ila sina shaka, uwepo wa Rob Holding bado unanipa jeuri.. Hii Arsenal ya sasa hata umuweke beki asieaminika anakamua vyema tu, si yule pale Mustafi!
 
Sasa City ina mashabiki? Nafikiri ni miongoni mwa timu zenye plastic fans duniani. Angalia hata jukwaa lao humu.
 
Mara ya mwisho Liverpool kupoteza mechi ya ligi (PL) Anfield ilikuwa msimu wa 2016/17.

Nawashauri kocha wenu asihangaike kuandaa speech nyingi, moja tu inatosha.
Hesabu na leo hatuna namna nyingine liver mtakaa tu pale pale kwenu.Vijana wana ari na nguvu na kila sababu ya kuwamaliza liver nyumbani.
Tunajua hamtaki kufungwa ila itabidi mfungwe tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo kauli ya kuwashangaza itoe, kwasababu wenyewe wanajua kinachoenda kufanyika pale uwani kwao, tumΓͺmkalisha game mbili mfululizo, una haja gani ya kutuumia neno 'kuwashangaza' hawa tunaenda kuchukua point3 kama tulivyochukuaa kwa Fulham
 
Sasa City ina mashabiki? Nafikiri ni miongoni mwa timu zenye plastic fans duniani. Angalia hata jukwaa lao humu.

Sihesabu kuna fans wa Citeh bongo. Nimeshangaa umeniambia wanajukwaa huku. Kwenda kupitia kidogo nakuta picha za Adebayor na wachangiaji ni fans wa Liverpool na Arsenal 😁😁
 
Ingawa Citeh wako aggressive kwenye kujitanua. City Group nadhani inamiliki au kuwa na hisa nyingi kwenye timu kama 10 au zaidi nchi mbali mbali. Watakuwa wanazitumia hizi kujiongezea mashabiki duniani
 
Sihesabu kuna fans wa Citeh bongo. Nimeshangaa umeniambia wanajukwaa huku. Kwenda kupitia kidogo nakuta picha za Adebayor na wachangiaji ni fans wa Liverpool na Arsenal 😁😁
Hahahaha ni hatari. Baada ya kupigwa tano nikaenda jukwaa lao nikakuta post ya mwisho ni alhamisi wiki iliyopita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…