Arsenal (The Gunners) | Special Thread

London, England. Kiungo wa Arsenal, Henrikh Mkhitaryan, amemwaga chozi baada ya kuambiwa na daktari kuwa majeruhi aliyoyapata yatamuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Madaktari wamemwambia mchezaji huyo aliyeumia Jumatano iliyopita katika mechi ya Kombe la Ligi ambayo walipoteza kwa kufungwa 2-0 na mahasimu wao Tottenham Hotspur anaweza kukaa nje hadi mwisho wa msimu huu.

Kiungo huyo aliumia mguu sehemu ya misuli mkubwa wa uliopo kati ya dole gumba na kifundo cha mguu ‘ankle’ siku tatu tangu aifungie Arsenal mabao yote ilipofungwa 3-2 na Southampton katika Ligi Kuu England.

Mchezaji huyo kutoka Armenia, aliyetua Arsenal siku ya mwisho ya usajili wa Januari mwaka huu, akitokea Manchester United anaamini benchi litamnyima fursa ya kutoa mchango wake kwenye timu hiyo.

Madktari wamesema kama hatajitonesha atarejea uwanjani katikati ya Februari 2019, hivyo ataikosa michezo dhidi ya Liverpool wa Desemba 29 na ule wa Manchester City Februari 3 mwakani.

Wakati kiungo huyo akikutwa na majanga hayo, Arsenal imetangaza kuwa beki wake wa kulia Nacho Monreal na Shkodran Mustafi wamepata ahueni na wanatarajiwa kuwepo uwanjani katika mchezo wa kesho dhidi ya Brighton & Hove Albion.

Ingawa itaendelea kumkosa Hector Bellerin, kwa wiki mbili zaidi kwani bado hajaruhusiwa kuanza mazoezi na madaktari.
 
Arsenal inataka kuvunja rekodi ya usajili ya Club kwa kupeleka kitita cha £72 millions kwa club ya Lille ili kupata saini ya winger wa club hiyo Nicolas pepe
Source, London evening standard
 
Heri ya krisimass Arsenal Fans, gemu yenu na Burnley mlishinda lakini mlicheza ovyo ovyo sana ..

Next mko na Liverpool ..naomba msituangushe wadogo zetu ..

Liver lazima akae, Come on Arsenal.
 
Hayo mawazo yako unatakiwa uyafute kwanzia sasa..
 
Arsenal inataka kuvunja rekodi ya usajili ya Club kwa kupeleka kitita cha £72 millions kwa club ya Lille ili kupata saini ya winger wa club hiyo Nicolas pepe
Source, London evening standardView attachment 977249
Huyu jamaa ni Dangerous ni zaidi ya hatari ana skills, ana speed, na kizuri zaidi ana jicho la Goli balaa ......... Lakini sidhani kama anaweza kuwa value ya £ 72 ml ni nyingi mno........ mkibahatika kumsajili mtakuwa mmelamba mtu.
 
#Breaking_News Kulingana na taarifa kutoka Espain timu ya Arsenal tayari wamefikia makubalino na Sevilla juu ya kumsajili Ever Banega pamoja na beki wa Real Valliadolid Fernando Calero amabae anapatikana kwa kiasi cha £10m.
Sevila wamewambia Arsenal walipe kiasi cha £18m ili wamnase kiungo iyo ambae anaonekana kuvutiwa kufanya kazi na Unai Emery.
Adi sasa mazungumzo yanaenda vizuri kupitia wakala wa wachezaji.
Pamoja na timu zote mbili dili inaweza ikawa Official pindi dirisha la usajili litakapo funguliwa January.
Tukumbuke huu utakuwa ni usajili mzuri sana endapo tu km utakamilika mapema.
Ila cha msingi ni kusubiri pindi dirisha litakapofunguliwa january na lolote linaweza kutokea.
 
Banega atatukumbusha Santi Carzola akija pale ana udambwi sio kidogo

Mkuu unajipa moyo tuu!!Itapita muda sana kuja kupata kiuongo kama Santi Cazorla


Kiungo anajua kudribble anajua kupiga pass normal na killer ones,anaejua kuhold mpira anajua kufunga akipata chance


Huyo Banega mzuri kama deep lying playmaker lkn kumpata wa kukusahaulisha Cazorla bado Mkuu


Kama ilivotake time kumpata wa kumrithi Vieira atleast for now unaweza ukamake case kwa Torreira ila the same itakua kumpata kiungo wa kuwasahaulisha mambo ya Santi Cazorla mojawapo ya viungo waliokua wamebarikiwa sana
 
Ndio maana nimesema atatukumbusha tu, maana carzola alikuwa anatumia miguu yote miwili kwa ufasaha,

Banega namuona kama mtu atakayesaidia kupandisha timu mbele, na ndicho anachokitaka unai, anahitaj mtu wa hivo,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…