Arsenal (The Gunners) | Special Thread




Haters wanasema kuna makosa mawili offside na handball.

Madai yote hayana msingi kwani hata kama Koscielyn asingeguswa na mpira bado mpira huo ulikuwa ukienda kimiani baada ya kuguswa na Alex-Oxlade Chamberlain.

Mwamuzi kaona mpira umemgusa Koscielyn na sio Boss kaugusa mpira kwa makusudi.

Mkuu Mwanakijiji ana mada hapa inafafanua hili la mpira kugusa mkono.
 
Alifunga kwa mkono Mkuu, hakuna sababu ya kupindisha ukweli Mkuu.
Leo umekuwa mkweli yaani ungekuwa karibu ningekupa kitu kizuriiiiiiiiii!!!!!...... haya wanasema win is a win
 
Reactions: BAK
Uko moyoni mwangu kwa muda mrefu twende Mombasa tukawaone Kiba,Whizkid na Breezy tafadhali kila kitu juu yangu
kesho nawahi job mapema sana w'end murua.
Hahahhaha kwa goli la mkono
...... baada ya kunichamba ndo wanifariji eehhhh.....haya bana!!!
 
Reactions: BAK
Niko tayari kukifuata popote ulipo hicho kitu kizuri kasoro Syria tu kule mabomu yanavyoanguka kunatisha sana Khe kheeeee kheeeee....lakini hebu kuwa mkweli tulistahili kupata penalty au la? Kandanda tulilocheza hatukustahili kupata ushindi? 😉😉😉

Leo umekuwa mkweli yaani ungekuwa karibu ningekupa kitu kizuriiiiiiiiii!!!!!...... haya wanasema win is a win
 

Mkuu, Syria waingia bila tabu ila usijaribu kwenda mji wa Aleppo mji balaa huu..

😀
 
Reactions: BAK
Mhhhh !!! sema ni makosa tu ya kimechezo kawaida uwanjani hata refa naye ni binadamu lakini siyo kwa sababu hizo.....
 
Hahahahha njooo huku.... mlistahili pia hata Burnely alistahili ila ndo hivyo mwisho wa siku lazima mmoja awe mshindi hongereni kuna vijimakosa tu fulani mkirekebisha mtatisha sana ila tatizo ndo limekuwa kama ugonjwa wenu
 
Reactions: BAK
Pole na kushikwa shati nyumbani mapema leo. Niliacha kuangalia kwenye nikijua mmeshashinda kuja kuangalia matokeo naona 1-1 dah! Kweli kandanda ni dakika 90.

Sawa mimi sisemi
.......
 
Mhhhh !!! sema ni makosa tu ya kimechezo kawaida uwanjani hata refa naye ni binadamu lakini siyo kwa sababu hizo.....

Inaweza kuwa ni handball lakini mwamuzi hakuona kama Boss ameugusa mpira bali kaona mpira umemgusa.

Kuna magazeti mengine tayari wanasema eti Boss "he smuggled it in".

😀😀
 
Huyo Boss alikuwa amelala kabisa kulingana na picha uliyoweka. Si amefunga macho yake hapo ili asiuone mpira!!??. Mpira ndio ulitafuta shari na ugomvi, hapo Boss wako hana hatia. Ilikuwa hakuna namna, lazima ajitetee dhidi ya mpira.

Offside? Haikuwa offside bana. Nilichora msitari na sikuona hiyo offside. LOL. Babu Wenger afurahi tu leo kwa miaka 20 ya kutibu wagonjwa wa moyo na pressure. Ngongo amerudi kwa Babu au amekacha bado?

Tottenham aendelee kuwa pale juu, ndio ligi itanoga kwa Arsenal.
 
Pole na kushikwa shati nyumbani mapema leo. Niliacha kuangalia kwenye nikijua mmeshashinda kuja kuangalia matokeo naona 1-1 dah! Kweli kandanda ni dakika 90.
Acha tu kama vile nyie mlivyonivuruga yaani nilikuwa nishafunga mahesabu nije nifanye fujo humu Mara kitu kimesomeka nilivurugwaaaaaaa!!!
 
Reactions: BAK
Ni kweli aisee tuna timu nzuri sana mwaka huu na majeruhi wakirudi tutatisha sana, ila pia bado tunafanya uzembe mwingi tu ikiwemo kutojiamini na kutojituma haya yanaweza kusababisha tukaishia tena kushika nafasi yetu ya nne au hata ya chini zaidi lakini wakiamua kungangamara basi tutakula sahani moja na MANC, Chelsea na Nyinyi pia mpaka kieleweke.

Hahahahha njooo huku.... mlistahili pia hata Burnely alistahili ila ndo hivyo mwisho wa siku lazima mmoja awe mshindi hongereni kuna vijimakosa tu fulani mkirekebisha mtatisha sana ila tatizo ndo limekuwa kama ugonjwa wenu
 

Ilikuwa ni lazima tuwakaribie Man City na Spurs kwa points leo.

Ila yaliyoandikwa leo kwenye magazeti, ndiyo utafahamu ni jinsi gani Arsenal inachukiwa.
 
Pole sana huwa inaudhi sana hali hiyo ya kujua ushindi na 3 points kapuni halafu kibao kinageuka.

Acha tu kama vile nyie mlivyonivuruga yaani nilikuwa nishafunga mahesabu nije nifanye fujo humu Mara kitu kimesomeka nilivurugwaaaaaaa!!!
 
Siku hizi umekuwa mfuasi wa Wenger?
 
Reactions: BAK
Ilikuwa ni lazima tuwakaribie Man City na Spurs kwa points leo.

Ila yaliyoandikwa leo kwenye magazeti, ndiyo utafahamu ni jinsi gani Arsenal inachukiwa.
Hamna kuchukiwa Hilo ndo soka bana kutambishiana kukejeliana alimradi siku inaenda soka linanoga ,kuna timu ina haters wengi kama Man U ?.......nyie shida yenu tu mmekuwa kivutio kwenye dunia miaka mingi bila kombe la EPL wala UEFA mkizingatia mnafanya vizuri sana..... ila naamini ipo siku yenu tu nanyi mtabarikiwa..
....keeping on trying one day Yes !!!!
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…