Mkuu,
Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Levy ameweka zuio kwa Adebayo asiende West Ham kwa sababu Adebayo amekataa kwenda QPR au Crystal Palace. Levy alitaka Adebayo aende kwenye timu hizo ambako Tottenham wangechangiana malipo ya paundi 100,000 ambazo Adebayo analipwa na Tottenham kwa wiki.
Adebayo kuona anaambiwa achague moja ya timu hizo akakataa na Levy akawaambia West Ham kama wanamtaka Ade basi wao wachukue jukumu la kumlipa pesa yote yaani paundi 100,000 kwa wiki wazo ambalo West Ham wamelikataa.
Unafahamu Tottenham wanawaangalia West Ham kwa jicho la husda hasa kwa kuzingatia kwamba wote wapo juu kwenye msimamo wa ligi hivyo West Ham kuonekana ni tishio kwa Tottenham. Ndio maana Tottenham wakaona Adebayo aende kwenye hizo timu za chini ambazo si tishio sana.
Haya mambo ya usajili wakati mwingine yanaleta mtafaruku sana ulojaa pilikapilika nyingi.
Hata hivyo Tottenham ndio watakaokula hasara kwa kuendelea kumlipa Adebayo hicho kiasi cha fedha hadi msimu wa ligi uishe, na mkataba wake baadae mwaka huu.