Kama nilivyokwishasema Jumamosi, mzee Wenger inabidi asajili mshambuliaji makini na DM kijana. Arsenal tunahitaji washambuliaji zaidi ya wanne.
Mikael Arteta anazidi kuchoka kutokana na umri na hali hio inasababisha Arsenal kukaribisha mashambulizi mengi ndani ya eneo lao.
Pia hali hiyo inawafanya Aaron Ramsey na Santi Cazorla wawe wanarudi nyuma kutafuta mipira ambayo ingekuwa inarudishwa na Arteta.
Hali hiyo pia inamchosha sana Jack Wilshere ambae inabidi awe anakwenda mbele kutafuta magoli na kuacha eneo la wazi pale katikati ambalo inabidi aliangalie pia.