Are spies made or born?

dah!

mara nyingi kunakuwepo na viashiria ambavyo vinaweza onekana tangu udogoni.
viashiria hivi vinaweza kuwa kutambuliwa na mtu wa familia ambaye tayari yuko kwenye system. ikitokea hivi na huyo mtu wa familia akaona utafaa basi anaweza akawa "anakulea" na kukujenga ili baadae iwe rahisi kukushawishi kuingia huko.

aidha viashiria hivi vinaweza kuonekana katika mfumo wa makuzi na elimu, mfano mwalimu wako, jirani yako, ndugu wa rafiki yako n.k.

pia wapo wataalamu kutoka ofisi kuu ambao nao wanajukumu la kutambua vipaji (potential candidates).

baada ya "kuonekana" unafaa inakuja ushawishi na kukujengea mazingira ya utakapo fuatwa na kuombwa kujiunga usisite kukubali. miaka ya awali chuo kikuu na jkt vilikuwa viwanja vya mawindo kwa watu wa "taaluma". mkufunzi kutoka makao makuu alikuwa na "warsha" ya siku moja na wanafunzi wa mwaka wa kwanza kuwaelezea umuhimu wa usalama hii ilikuwa ni mbinu ya kuwatayarisha wanafunzi kifikra ili wanapofuatwa wasisite kujiunga (ikumbukwe wakati huo chuo kikuu kilikuwa kimoja tu, hivyo hapo ndio palikuwa na jumuiko la wasomi wetu). idm mzumbe pia ulikuwa uwanja wa ajira(ingawa wakati huo haikuwa chuo kikuu)

kwa maneno mengine mtu anazaliwa na viashiria lakini viashiria hivyo lazima viboreshwe. usisahau kila sehemu hawa watu wapo kuanzia walimu, madaktari, wahandisi, wachumi, wahasibu, viongozi wa dini, wanasiasa nk. hata watu wasio na taaluma mahususi pia wapo. japokuwa kama alivyosema mchangiaji moja hapo juu sio kila mwenye viashiria ameajiriwa au ameonwa. wengine wanaviashiria husika lakini mazingira ya malezi/makuzi yao yamefanya wawe na viashiria vingine vyenye nguvu zaidi hivyo kuwa disqualify.

naamini nimekusaidia kidogo
 
nashukuru sana je viashiria hasa ni vipi vinavyotazamwa na hawa jamaa wa usalama naomba kuwasilisha
 
dah!

mara nyingi kunakuwepo na viashiria ambavyo vinaweza onekana tangu udogoni.
viashiria hivi vinaweza kuwa kutambuliwa na mtu wa familia ambaye tayari yuko kwenye system. ikitokea hivi na huyo mtu wa familia akaona utafaa basi anaweza akawa "anakulea" na kukujenga ili baadae iwe rahisi kukushawishi kuingia huko.

aidha viashiria hivi vinaweza kuonekana katika mfumo wa makuzi na elimu, mfano mwalimu wako, jirani yako, ndugu wa rafiki yako n.k.

pia wapo wataalamu kutoka ofisi kuu ambao nao wanajukumu la kutambua vipaji (potential candidates).

baada ya "kuonekana" unafaa inakuja ushawishi na kukujengea mazingira ya utakapo fuatwa na kuombwa kujiunga usisite kukubali. miaka ya awali chuo kikuu na jkt vilikuwa viwanja vya mawindo kwa watu wa "taaluma". mkufunzi kutoka makao makuu alikuwa na "warsha" ya siku moja na wanafunzi wa mwaka wa kwanza kuwaelezea umuhimu wa usalama hii ilikuwa ni mbinu ya kuwatayarisha wanafunzi kifikra ili wanapofuatwa wasisite kujiunga (ikumbukwe wakati huo chuo kikuu kilikuwa kimoja tu, hivyo hapo ndio palikuwa na jumuiko la wasomi wetu). idm mzumbe pia ulikuwa uwanja wa ajira(ingawa wakati huo haikuwa chuo kikuu)

kwa maneno mengine mtu anazaliwa na viashiria lakini viashiria hivyo lazima viboreshwe. usisahau kila sehemu hawa watu wapo kuanzia walimu, madaktari, wahandisi, wachumi, wahasibu, viongozi wa dini, wanasiasa nk. hata watu wasio na taaluma mahususi pia wapo. japokuwa kama alivyosema mchangiaji moja hapo juu sio kila mwenye viashiria ameajiriwa au ameonwa. wengine wanaviashiria husika lakini mazingira ya malezi/makuzi yao yamefanya wawe na viashiria vingine vyenye nguvu zaidi hivyo kuwa disqualify.

naamini nimekusaidia kidogo

Daaah asante sanaa mkuu umenipa zinga la elimu aisee..kumbe jamaa ndio tunakaa nao huku huku mitaani!
 
Kwa hawa wanaoanza mapema kama sekondari, kwa kweli sijui hata ni saa ngapi wanakuwa trained, yaweza kuwa ni watu waliokwishakuuwa trained somewhere halafu wakaingia shule kama wanafunzi, labda!,ila wewe ambaye bado, huwezi kujijua kuwa unafuatiliwa ili uwe hivyo mpaka baada ya muda fulani, hutofuatwa na kuambiwa au kuombwa ufanye kazi hiyo, utafuatiliwa kimya kimya baada ya kuonekana kuwa unaweza kuwafaa, hutojua kuwa unafuatiliwa, kuna mtu atasogezwa close na Wewe, huyo ndiye atakaye kutune mpaka utafika huko, anaweza kuwa mjomba wako ambaye naye yumo huko, mwalimu, jirani au rafiki yako, kuwa na wewe karibu kutamfanya akujue zaidi na kupeleka information, na anakuwa anakulead kwenye njia ya kukufikisha huko bila wewe kujijua, utakuja kujielewa baadae kuwa wewe ni nani, na hapo ndipo utaanza kuwa msiri zaidi na mambo yako, mtu aliyewekwa kuwa close na wewe, atakushauri mambo mengi ambayo ukiyafuata yatakufikisha huko bila wewe kujijua mwanzoni but ni mambo ya manufaa tu kwako, na kwa hao wanaokusubiri wakuingize kwao, kwa mfano, unaweza ukawa unapenda kusomea kitu fulani, lakini huyo mtu akakushauri mara mbili mbili kusomea kitu kingine, akakusisitiza mno, akakupa faida zaidi za kusomea hicho anachokushauri, akakuhaidi au akakuweka katika connection nzuri na ya uhakika ya kuzidi kufanikiwa katika kitu hicho, yaani anakuwa mshauri wako anayekufanikisha kila mara, unamuamini, kila atakapo kueleza jambo unalifuata cause unafanikiwa mwisho unajikuta tayari umeshafika mlango, kwenye hivyo vyuo vyao utafika hivyo, utashauriwa na washauri wako wa siku zote mpaka utafikia huko, unaambiwa jiendeleze kwenye hili, kachukue diploma ya hili, embu kasome chuo fulani kitu fulani, kuna sehemu nitakuunganishia kuna mtu namfahamu etc. unaweza hata ukawa hutumii hela zako sometimes, unaweza akatukoa wa kukufadhili au ukafadhiliwa na ofisi aliyokupeleka, ukasoma kwa raha, unafanyiwa mambo yako faster kuliko wenzako, ukishaingia kwenye vyuo vyao utakuwa tayari umejijua, na utakuwa msiri zaidi, usije ukapata matatizo outside, hawa watu wana raha mambo yao wanafanyiwa faster, mnaweza kujikuta wengine kwenye ofisi, mnasahaulika, hamshughulikiwi haraka mnapoomba kwenda kusoma, lakini yeye ni faster anashughulikiwa, hawatakiwikuwa waropokajiropokaji , lakini unaweza kukuta mtu wa aina hiyo anaropoka kitu fulani mbele yako ili akujue wewe una maoni gani au unakijua vipi, anakuchunguza tu, yuko kazini, nahauoi au kuolewa hovyohovyo, mtu unayetaka kuoana naye anachunguzwa kwanza, akionekana ok kwao wewe kuwa naye, mtaoana, ukikataliwa kuoana naye, hutomuoa, la sivyo uchague ofisi au yeye, nahata ukimchagua yeye ukiacha ofisi utakipatapata, cause you have siri nyingi waweze payuka huko unakoenda, mara nyingi wanaoana wao kwa wao, hii kazi wengine unaweza kusikia kastaafu lakini huwa ni till death, sio kustaafu totally kama kazi nyingine, unaendelea kimya kimya, kama nyie wazazi mko humo mtoto wenu ni rahisi kuingizwa humo, sio mtu yule wa kuchunguzwa saaana, muda mreeefu kwa kuwa nyie tayari mnajulikana ni watu wa aina gani, wasiri, na moja kwa moja mtoto wenu mtakuwa mmemkuza kuwa hivyo, kutokana na mazingira yenu nyumbani au atakuwa amestaadopt kuwa hivyo, atawafaa, watamuongoza/ mtamuongoza tu kuwa anavyotakiwa kuwa, kuwa barabara itakayomfikisha/ itakayomfanya kuwa hivyo
 
Mi kinachonishangazaga kuhusu watu wa aina hii, jinsi wanavyojua kufanya kazi yao, ni pale mtu anapojifanya kichaa, ombaomba, shoeshiner, mvuta bhangi n.k ile kupata information fulani, unakuta mtu katokea Mwanza anakuja kujifanya kichaa Dar, hakuna anayemjua, anaifanya kazi yake saaafi, akimaliza anarudi alipokuwa(ofisini Mwanza), kuna mtu alishakwepwa na mtu posta ambaye alishawahi kuwa kama kichaa mtaani kwao kwa muda then akatoweka ghafla, yaani watu walishangaa mtaa ghafla umepata kichaa wasiyemjua, wakawa wanampampa vyakula vyakula,muda mfupi baadae ghafla akatoweka, siku hiyoaliyomuona posta alitaka amfuate amsalimie, akakwepwa, alimshangaa cause alikuwa amepiga nguo smart za ofisi, akajua yule hakuwa kichaa kweli kuna mtu alikuja kumfuatilia mtaani kwao, alipowaambia wenzie mtaani hawakuamini, eti yule kichaa kamkuta that smart mjini wakati alikuwa anavaa nguo chafuchafu na kulala nje mtaani kwao
 
Mi kinachonishangazaga kuhusu watu wa aina hii, jinsi wanavyojua kufanya kazi yao, ni pale mtu anapojifanya kichaa, ombaomba, shoeshiner, mvuta bhangi n.k ile kupata information fulani, unakuta mtu katokea Mwanza anakuja kujifanya kichaa Dar, hakuna anayemjua, anaifanya kazi yake saaafi, akimaliza anarudi alipokuwa(ofisini Mwanza), kuna mtu alishakwepwa na mtu posta ambaye alishawahi kuwa kama kichaa mtaani kwao kwa muda then akatoweka ghafla, yaani watu walishangaa mtaa ghafla umepata kichaa wasiyemjua, wakawa wanampampa vyakula vyakula,muda mfupi baadae ghafla akatoweka, siku hiyoaliyomuona posta alitaka amfuate amsalimie, akakwepwa, alimshangaa cause alikuwa amepiga nguo smart za ofisi, akajua yule hakuwa kichaa kweli kuna mtu alikuja kumfuatilia mtaani kwao, alipowaambia wenzie mtaani hawakuamini, eti yule kichaa kamkuta that smart mjini wakati alikuwa anavaa nguo chafuchafu na kulala nje mtaani kwao

Kweli inahitaji moyo wa ajabu sana na akili nyingi kweli kweli aisee! Kwenda kujifanya kichaa sehemu si kanzi ndogo atii.
 
Lazima uwe na chembe chembe za kijasusi tangia mdogo then baadae zinakuwa developed kwa mafundisho maalumu ya kazi husika. Ila kwa nchi yetu miaka is karibuni imekuwa tofauti na kipindi cha Nyerere. Now days kujuana na pia watoto wa high government officials ndo wanachukuliwa hata kama waredi wa kiintelijensia hawana.
From this point is where maafisa wengi wa serikali wanashiriki katika mambo ya kifisadi, embezzlements na corruption bila kujulikana au hatua stahiki kuchukiliwa na serikali.
 
Sasa yale makeke kama ya kucheza na gadgets, dead drops, planting and clearing surveillance bugs, surveillance detection techniques na tailing a subject hizo ni mpaka uingie huko chuoni kwao au unafuliwa mtaani ambapo ndio kama field zao?
 
Sasa yale makeke kama ya kucheza na gadgets, dead drops, planting and clearing surveillance bugs, surveillance detection techniques na tailing a subject hizo ni mpaka uingie huko chuoni kwao au unafuliwa mtaani ambapo ndio kama field zao?


Mambo kwa hatua (awamu), mtoto hukaa, hutambaa, husimama, hutembea, hukimbia nk. Kwa hatua/awamu muda muafaka ukifika.

Unalidhalilisha jina unalotumia kwa swali unalouliza au kushangaa!

Halafu usipekenyue saana... "Utapata homa ya dengue bure!,"
 
Mambo kwa hatua (awamu), mtoto hukaa, hutambaa, husimama, hutembea, hukimbia nk. Kwa hatua/awamu muda muafaka ukifika.

Unalidhalilisha jina unalotumia kwa swali unalouliza au kushangaa!

Halafu usipekenyue saana... "Utapata homa ya dengue bure!,"

hahahaaa...sawa mkuu tena naogopa homa ya dengue!
 
I think the more the world becomes dynamic and rapidly changes socially, politically and even technologically, ndivyo recruitment techniques zinavyopaswa kuboreshwa na kuimarishwa ili kuhakikisha wanapatikana well-balanced and more intelligent individuals who could cope with those global dynamics!
Hayo ni mawazo yangu tu wakuu!
 
Kweli inahitaji moyo wa ajabu sana na akili nyingi kweli kweli aisee! Kwenda kujifanya kichaa sehemu si kanzi ndogo atii.

Ndio, but wanapoact katika namna tofauti tofauti katika kutafuta ukweli wa kuisaidia jamii, wanaisaidia jamii, sio kutumiwa kudhuru watu wasio na hatia kwa manufaa ya mtu fulani mkubwa(kigogo) for example kukamata drug dealers, wanaisaidia jamii, kukamata majambazi wakubwa n.k
 
Kweli inahitaji moyo wa ajabu sana na akili nyingi kweli kweli aisee! Kwenda kujifanya kichaa sehemu si kanzi ndogo atii.

Sijui kama nchi ikikosa spies, itakuwa salama vya kutosha, wanatusaidia sana wanapofanya mambo ya kuilinda jamii kikweli dhidi ya watu hatari, but wanapofanya tofauti na hapo, kuwadhuru watu wasio na hatia kwa manufaa ya mtu fulani mkubwa(kigogo), ndipo wanapoenekana kuwa ni wabaya na hawafai, but wana umuhimu wanapofanya mambo ya kuisaidia jamii kikweli
 
Kuna sehemu nimesoma wanasema kuwa;
"The only thing you can be certain of is that you are a potential target if you have access to classified, controlled or sensitive proprietary information. That's why it's important to be careful what you say when talking with ANY Stranger!"
 
Zamani enzi za mwl ulikuwa spotted kuanzia primary ila huambiwi kwa umri ule. Wakuu wengi wa shule walikuwa usalama!!! then unaendelea kufuatiliwa hadi sekondari na chuo wanakupasulia jipu!!! kinachoendelea hapo nameza.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom