Nilisoma ile ruling ya mahakama nikaona kuwa wanatambua kuwa kuwazuia wagombea binafsi ni makosa, lakini wakaogopa kutoa hukumu sahihi na kudai jambo hilo liamuliwe na bunge. Hapo ndipo nilipoona kuwa Tanzania hakuna pa kukimbilia kama ukionewa na serikali kwani hata mahakama itakuambia rudi mkajadiliane na serikali hiyo hiyo iliyokuonea.
Kifungu cha katiba kinachopingwa na Mtikila vile vile kinakiuka Article 20(2) ya UNIVERSAL DECLARATION OF HUMAN RIGHTS ya Umoja wa Mataifa inayosema kuwa : "No one may be compelled to belong to an association," na Article 21(1) inayosema "Everyone has the right to take part in the government of his country, directly or through freely chosen representatives."
Mahakama Kuu ilitakiwa iangalie swala la haki za binadamu kwa upana zaidi na kuiambia serikali kuwa mmekosea. Cha kushangaza, ni kuwa mahakama yetu pia imekuwa kama ni sehemu ya utawala au inaogopa majukumu yake. Inawezekana majaji wanaogopa kuvuliwa nyadhifa zao na Rais Kikwete.!!!!