Apigwa risasi nje ya Kanisa Ubungo

Apigwa risasi nje ya Kanisa Ubungo

Hauwezi kuficha ukweli. Magaidi wote niliowai kusikia matukio yao ni waislamu. Lililotokea sio tukio la kigaidi, usichanganye mambo mkuu. Haikua sahihi kuleta imaginations za ugaidi kwenye hili swala.

Ni kweli si sawa kuhusianisha ugaidi kwenye hili suala lakini tuko kwenye wakati mbaya kwa mfano huyo mtuhumiwa asingejulikana/ kupatikana tungeweza kuwa tunaongea habari nyingine hapa, tena kwa kuwa tukio limetokea kanisani naamini kabisa ingekuwa habari mbaya sana,tumshukuru MWENYEZI mtuhumiwa amepatikana.


Sasa wewe usichanganye mambo kwanza kamsome CARLOS THE JACKAL ( ILICH RAMIREZ SANCHEZ) hako ni kamfano ili kakuweke sawa tu

Ukijua kabisa maana ya Ugaidi WAZUNGU( wengi wao sana hawakuwa waislamu) WAMEEUA sana katika historia yao kwa ajili ya masilahi yao na ndio MAGAIDI WAKUBWA KULIKO WOTE

Waafrika mamilioni kadhaa waliuliwa na wazungu wakati wa ukoloni
Mifano wabelgiji waliua watu zaidi ya milioni kumi ZAIRE, Waingereza waliua sana MAUMAU na kwenye makoloni yao mengine, Wajerumani pia Tanzania yaani mifano ni mingi sana, na sio Afrika tu wamefanya huo UGAIDI DUNIA NZIMA.

Yaani kwa nielewavyo hata UKOLONI NI UGAIDI TU.

Kutest mabomu ya nuklia kule Australia na kuua watu asili wa kule ni UGAIDI tu.

MAREKANI Wameuua watu wengi sana na kufanya dhuluma nyingi sana duniani huo NI UGAIDI MKUBWA NA NDIO WA MWANZO KWA KARNE HIZI kwa maana ukawasababisha baadhi ya watu waanze kuwashambulia kwa namna hii ambayo sasa ndo tunalazimishwa kuielewa kuwa ndo UGAIDI na ndio maana wewe umejikuta ukisema wote uliowasikia ni waislamu, maana wametaka dunia nzima watu wajue hivyo ili wao wapate pa kujificha,

hawa watu ni hatari sana wamezunguka dunia nzima kufanya dhuluma kwa mabavu yaani kwa UGAIDI ama kwa wizi wa kijanjajanja ili kuendeleza nchi zao tena kwa miaka mingi.

NA HATA WAZEE WETU WAKATI WA UKOLONI WALIPOKUWA WANAWAPINGA WALIITWA MAGAIDI, HUKU WAO WAKIJIONA SIO MAGAIDI KWETU...

Naamini umenielewa ndugu
 
mwenye miwani ndio kaamtia mwenzie mkwaju...nilikuwa natoka makoka ndio nimi nikachukua picha kidogo

20229149_369943693421130_5407867311937929914_n.jpg
MZEE MPANDE...MMBUNGE WA ZAMANI UKO MSOGA KWA MSTAAFU.....inasemekana ni mkwewe hyo
 
hyo mzee hatujui wamefanyana nini ila sidhan kama njaa...labda mambo mengine ya ndani kabsaaa....labda kuna vsa zaidi ya tunavoviona huku nnje
Ishu ya njaa ikibebwa ndani ya tamaa ni mbaya sana. Hujamshangaa mwanamke mumewe ana hela na maisha safi na Bado penzi atapata lkn Bado atatoa nje kwsabb y tabia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ishu ya njaa ikibebwa ndani ya tamaa ni mbaya sana. Hujamshangaa mwanamke mumewe ana hela na maisha safi na Bado penzi atapata lkn Bado atatoa nje kwsabb y tabia?

Sent using Jamii Forums mobile app
mmmmmh!!! kweli ila mi natzama kwa nnje kwenda kumshoot baba mkwe ni zaidi ya huku nnje tunavoona.....sjui kwa kweli...ila swala mke kutoa nnje na mumewe tajiri ni kesi ingine kabsaaa
 
Sababu za mwandishi kumpiga risasi mkwe




Muumini wa kanisa Katoliki, Adrian Mpande amepigwa risasi mbili akiwa anasubiri kuingia kanisani katika Parokia ya Kibangu wilaya Ubungo jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa George Ng’atigwa ambaye ni shuhuda wa tukio hilo amesema kuwa Mpande alikuwa akisubiri kuingia kanisani majira ya saa tatu asubuhi lakini alikuja mtu mmoja aliyekuwa anatembea kwa miguu na kumpiga risasi ubavuni na mkononi, hali iliyosababisha aanguke na kupoteza fahamu.

Alisema kuwa mtu huyo alikimbia lakini watu waliokuwa maeneo hayo walifanikiwa kumkamata baada ya kuishiwa risasi wakati akijaribu kuwatishia.

Aliongeza kuwa baada ya kumkamata mtu huyo, waliwasiliana na jeshi la polisi ambalo lilifika na kuondoka naye kwa ajili ya taratibu za kisheria na kwamba majeruhi alikimbizwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupatiwa huduma ya kwanza katika zahanati iliyokuwa karibu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni Dar es Salaam, Suzan Kaganda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi wa awali unaonesha kuwa limetokana na ugomvi wa kifamilia.

“Mtuhumiwa tunaye tunaendelea kumhoji na aliyejeruhiwa yuko hospitali anaendelea na matibatu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” Kamanda Kaganda anakaririwa.
 
Kwani silaha zinatengenezwa kwa ajili ya kuulia mbu ?
Hayo ni matumizi halali ya silaha na ndilo kusudio LA kutengenezwa kwake
Tuache porojo wakuu. Motive behind ndiyo big deal

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TE="Interest, post: 22436242, member: 284027"]Mkazi mmoja wa maeneo ya Ubungo Kibangu Jijini Dar mapema leo amepata ajali ya kupigwa risasi na mtu asiyejulikana wakati akiwa anaingia Kanisani Parokia ya Kibangu.

Kwa bahati nzuri, risasi zilimlenga maeneo ya begani na ubavuni hivyo jamaa kwa mshtuko ama kupoteza damu nyingi kulimfanya azimie papo hapo.

Watu waliokuwa maeneo hayo baada ya kumwona mfyatua risasi ambaye hakuwa na usafiri wowote, walianza kumkimbiza na kumpigia kelele za mwizi hadi kumtia mikononi na hatimaye kumkabidhi kwa Polisi.

Hata hivyo inahisiwa kuwa huenda ni ugomvi wa kifamilia.

======
Mkazi wa Ubungo, Kibangu amenusurika kifo baada ya kupigwa risasi wakati akitaka kuingia katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Kibangu, wilayani Ubungo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Akisimulia tukio hilo, mfanyakazi wa kanisa hilo, George Ng’atigwa amesema aliyejeruhiwa ni muumini wa kanisa hilo aliyemtaja kwa jina la Adrian Mpande.

Amesema tukio hilo lilitokea majira ya saa 3 asubuhi wakati muumini huyo alikuwa nje ya kanisa akisubiri muda ufike ili aingie kanisani.

“Mara akatokea mtu mwenye bastora akampiga risasi ubavuni na mkononi akaanguka na kuzimia,” amesema.

Amesema baada ya kutekeleza unyama huo, mtu huyo ambaye alifika kanisani hapo akitembea kwa miguu, alikimbia.

Amesema watu waliokaribu na kanisa hilo walimfukuza huku wakipiga mayowe na baada ya muda mfupi alikamatwa.

“Inaonekana alikamatwa baada ya bastora yake kuishiwa risasi kwa kuwa wakati anakimbia hakuwa akiwatishia waliokuwa wakimfukuza,”amesema.

Amesema baada ya kukamatwa,walifanya mawasiliano na Polisi ambao walifika baada ya muda mfupi na kuondoka naye.

Alisema alijeruhiwa kwa risasi alipata huduma ya kwanza katika zahanati iliyopo jirani na kanisa hilo na baadaye kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akifafanua, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Kaganda alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba huo ni ugomvi wa kifamilia.

“Mtuhumiwa tunaye tunaendelea kumhoji na aliyepigwa risasi anaendelea vizuri na Matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” amesema.

Chanzo: Mwananchi[/QUOTE]
Mbunge wa zamani wa Bagamoyo
Mzee Adrian Mpande amefariki nchini India akipatiwa matibabu
Chanzo Familia.
 
Back
Top Bottom