YNNAH
JF-Expert Member
- Dec 6, 2011
- 1,702
- 969
Dada mmoja alikuwa kwenye mishemishe zake,mara akaona kanga inaning'inia dukani ikamvutia na kwenda kuinunua. Bila kuisoma jina akampelekea mama mkwe wake,kisha akaondoka zake. Huku nyuma mama mkwe akaifungua ile kanga na kukuta imeandikwa "GUBU LA MAMA MKWE LIMENICHOSHA". Akampigia simu mwanae na kumueleza amwambie mkewe kwamba ujumbe wake nimeupata,mume akamuuliza mume umemwambia nini mama yangu?,mke akahamaki,akhuuu!! Sijamwambia kitu,kulikoni kwani? Mara akaingia mtu na ile kanga na kumwambia yule mume kwamba ujumbe wenyewe ni huu hapa. Palepale yule mume akampa talaka mkewe. Kadri mke alivyojieleza mume hakumuelewa. Je,hii ni halali?