Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,608
Diwani aliyemaliza muda wake wa Mawenzi, Jimbo la Moshi Mjini, Apaikunda Naburi ameongoza kura za maoni katika kata hiyo kwa kupata kura 58 kati ya 94 zilizopigwa.
Akitangaza matokeo hayo, katika uchaguzi huo uliofanyika leo Jumatatu, Agosti 4, 2025, Katibu wa CCM Kata ya Mawenzi, Jolitha John amesema Apaikunda amepata kura 58 akifuatiwa na Said Mndeme (29) na Abdi Mohamed (6) huku kura moja ikiharibika.
Mwenyekiti wa CCM wa Kata hiyo, Mujibu Abeid amesema pamoja na matokeo yaliyotangazwa na msimamizi hayo siyo uamuzi wa mwisho, uamuzi utatoka vikao vya juu.