anza wiki.

klorokwini

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
8,648
5,139
kuna njemba ilikuwa inamkong'ota na kumdunda waif wake vibaya sana mpaka yule mama akawa anaiogopa hii njemba vibaya sana.
kuna siku hii njemba iliumwa ikaenda hospitali na ikatakiwa kupeleka mkojo, njemba ilirudi home na ikatia mkojo kwenye kichupa na kukiweka pembeni ya kitanda. wakati anatandika kitanda kwa bahati mbaya yule mke wa hii njemba akaumwaga ule mkojo, kwa kuogopa mkong'oto na kipigo cha njemba akaamua atie mkojo wake yeye, halafu auchune kama hakukutokea kitu, bikozi angesema kaumwaga angeng'olewa meno yote kwa kipigo.
siku ya pili njemba ilichukua mkojo na kupeleka hospitali ,madaktari walionekana kuwa na tafrani na mshangao flani na kuja kuoneshana ile njemba ikiwa imekaa pale inasubiri majibu. na hatimae daktari mkuu akaiita hii njemba chumbani na mambo yakawa kama yafuatavyo.

daktari: ndugu,una uhakika huu mkojo ni wa kwako?
njemba:(:ikajibu kwa jeuri na hasira) ushaona mkojo nimeuleta mimi halafu unauliza kama wa kwangu?, wako wewe basi!! aaaargh
daktari::(baada ya kuona njemba ni jeuri na yeye akaamua kuijibu kwa kejeli) hongera ndugu una ujauzito wa miezi miwili!.

njemba ilizimia.
 
Ha ha ha, kuna mpwa 1 huku ni mkali kwa mkewe(jina kapuni) naye anahizi tabia za kibaunsa nahisi ujumbe umefika.
 
youblessed-title1.gif
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom