Ufisadi unachukua muda kufahamika kwenye Jamii, inaweza kuchukua mwaka mmoja mpaka muongo moja (Miaka 10) au zaidi.
Ukisikia ufisadi mwaka huu jua Dili hiyo ya kifisadi ilichezwa miaka kazaa nyuma. Kwa mfano Ufisadi wa Escwro tumeusikia hivi karibuni ni zao la Dili iliyopigwa miaka mingi ilyopita.
Kwa utangulizi huo naomba kujibu maswali yako kam ifuatavyo
1. Chadema kama ilivyo kwa vyama vingine makini ina interegencia kali kufahamu siri nyingi hasa zinazohusiana na Ufisadi mapema kabla ya wananchi ewngine wakawaida kufahamu.
Wakati wanatoa List of Shame 2007 walikua tayari wanajua Ufisadi wa Richmond japo Ufisadi wenyewe Publicaly ulijulikana 2008.
2. Kuhusu Mwl Nyerere kumkataa Lowassa tayari Kingunge ameshalifafanua nitalielezea kifupi hapa.
2005 wakati wa mchakato wa kumpata mpeperusha bendera wa CCM, majina matano yaliletwa na CC kwa NEC ili yachaguliwe majina matatu, katika majina hayo matano jina la Lowassa halikuwemo wajumbe wa NEC walihoji sana kwaninin jina la Lowassa halikuwepo walihoji sana mpaka kutishia mchakato kutoendelea, ndipo Mwl Nyerere akashituka kua kumbe Lowassa ananguvu kiasi hicho. Ili kutuliza munkari wa wajumbe wa NEC ndipo Kingunge akaleta sababu za Lowassa kukatwa na CC, Nyerere akatumia hoja hizo za Kingunge kuwezesha mchakato uendelee.
Hivyo basi Kingunge na Nyerere walifanya hivyo tu kunusuru mchakato na kurinda Heshima ya Chama, na hatuwezi kuhukumu kua Nyerere alimkataa Lowassa. ilikua KISIASA zaidi.