Sasa huyu jamaa kwa nini anafanya kazi kwenye magazeti ya vyama (Tanzania Daima na Uhuru), si aende kwenye gazeti la Taifa, MwanaHalisi. Mimi ndo gazeti ninalonunuaga na sikutegemea kukuta taarifa ya Kiataifa huku. Naomba Saed Kubenea either mkodishe au amuajiri kabisa ili makala hizi tuzipate kwenye gazeti la Taifa, MwanaHALISI.
Jielimishe:
1. Ngurumo ameandika
Maswali Magumu tangu mwaka 2002 katika
Mwananchi Jumapili, akamtia kibano Rais Mkapa. Lilipoanza
Tanzania Daima akahamisha makala hiyo kwenye gazeti hilo mwaka 2004 hadi leo. Amemtandika JK tangu alipotangaza nia ya kugombea 2005 hadi leo. Alikuwa mwandishi pekee aliyethubutu kukosoa serikali ya JK wakati wahariri na waandishi wote wakiogopa kumgusa
JK, au
RA au
EL. Hivyo, wanaoanza kumsoma leo, mmekoa mengi. Amekuwa pioneer, wengine wamefuata, na sasa wakosoaji wa JK wameongezeka. Katika wote wanaomkosoa JK, Ngurumo ndiye amekuwa consistent. Kudos!
2. Ngurumo ni mmoja wa walimu (mentors) wa Saed Kubenea, tangu enzi za
RAI miaka ya 2000. Kubenea alipokuwa anasimamia gazeti la upinzani,
Hali Halisi, kabla hajaanzisha
MwanaHALISI, Ngurumo aliendelea na kazi hiyo - mentoring - akiwa anahariri gazeti hilo. Kwa hiyo, kabla ya Ndimara, mwalimu wa Kubenea alikuwa Ngurumo. Sijui kama ameacha kum-mentor sasa, na ndicho kiini cha urafiki kati yao. Ukisoma vema kazi za Kubenea utagundua kuwa yapo maneno na staili ambazo ameziiga kwa Ngurumo. Wote wawili hawa wana sifa moja ya msingi - ni waandishi jasiri.
3. Kubenea alipotaka kuanzisha gazeti la
MwanaHALISI, miongoni mwa waliomsaidia kulianzisha na kulisajili ni Ngurumo na Absalom Kibanda. Nina uhakika watu hawa wawili, Ngurumo na Kibanda, wanaendelea na kuhariri baadhi ya kazi za
MwanaHALISI hata leo.
4.
Tanzania Daima si gazeti la Chadema, bali ni mali ya mtu, familia ya Freeman Mbowe (si unajua kila ampuni lazima iwe na mmiliki?) haliwezi kufananishwa na Uhuru kwa sababu si la chama cha siasa, na ndiyo maana utakuta habari zinazowabeba watu wa CCM au tahariri zinazounga mkono masuala kadhaa ya serikali katika
Tanzania Daima. Mbona kumekuwa na habari na makala nyingi zinazoumiza Mbowe au Chadema? Huwezi kukuta Uhuru ikisifia lolote la Chadema, na ndiyo maana
Uhuru halinunuliwi (linategema ruzuku na subscription ya lazima kwenye wizara na idara za serikali), na
Tanzania Daima linakua kila siku. Ni vema tutofautishe mali za Mbowe na mali za Chadema. Mimi naamini Tanzania Daima limeamua kuwa na
sera ya MABADILIKO, na kwa kuwa Chadema inasimamia mabadiliko hayo, achana na ukweli kwamba inaongozwa na Mbowe, lina kila sababu ya kuendelea kuandika linavyoandika, maana limetusaidia sana kuinua akili, hisia na mioyo wa Watanzania katika mapambano. Siku
Tanzania Daima litakapogeuka la Chadema ndiyo siku litakapoanza safari iliyoliua Uhuru. Unapozungumzia magazeti ya TAIFA, huwezi kuyasahau
Tanzania Daima na
MwanaHALISI.
5. Waliochelewa kumjua Ngurumo ndio wanaomshangaa na kumlinganisha na Kubenea. Ukweli ni kwamba hawalingani, hata kama wanashaabiana katika mambo fulani fulani. Sisi tuliofuatilia maendeleo na ukuaji wa Kubenea katika fani ya uandishi, tunatambua kazi nzuri ya akina Ansbert Ngurumo na Ndimara Tegambwage katika kumtengeneza Kubenea kuwa hivyo alivyo. Anayebisha amuulize Kubenea mwenyewe, maana kwa jinsi asivyo mtofu wa shukurani atawasifu na kuwashukuru waliom-mentor... hawa niliowataja na wengine anaowajua, waliolifanya
MwanaHALISI kwa hivi lilivyo leo. Kubenea unasemaje?
Nawasilisha.