Ansbert Ngurumo amchana Kikwete live...

Ningeshauri kuwepo na 'political maturity' badala ya usalama kumtafuta Ansbert serikali ijibu hoja/issues alizoandika huyu bwana. Hii itatujengea a new political culture inayokijita zaidi kwenye mgongano wa mawazo au/na hoja badala ya ku-supress imani/mtazamo tofauti kati yetu.

I hope walio karibu na wakubwa wataona umuhimu sasa wa kuchukulia mgongano wa mawazo kama opportunity ya kuboresha mikakati na utendaji. We need the likes of Ansbert to ingnite public debates on important issues. Dont supress him- answer him.
 
He..!
Uchuro huu!
Wewe sasa ndio unashinikiza hii thread ifungwe...ongea vitu vya ukweli bwana weeee!

Ukitaka ukweli juu ya hilo ongea fresh na mods nije na tread yenye data zote tena za kweli!

Anwy tuachane na hayo tukae kwenye maada ya kamanda Ngurumo!!
Mbiu ya mnyonge ikilia katu tajiri hatoizuia!!
 
Hii ni sahihi kabisa inabidi imfikie rasmi JK na chama chake wajue tumeshtukia uozo wao na watumie kama mwongozo kujirekebisha
 
jamani mimi hii kitu nai print kabis a nitairudia mara 10
hivi huyu Ansbert ngurumo ni nani?
Ni moja ya waandishi Mahiri kabisa wa Makala ambao Taifa limebahatika kuwa nao pia ni mmoja wa Wahariri wa Gazeti la Tanzania Daima,Mara nyingi Makala yake inatoka Tanzania daima ya kila Jumapili binafsi nimekuwa nasoma sana Makala zake na ninampongeza kwa kazi nzuri anayoifanya.
 
Ni moja ya waandishi Mahiri kabisa wa Makala ambao Taifa limebahatika kuwa nao pia ni mmoja wa Wahariri wa Gazeti la Tanzania Daima,Mara nyingi Makala yake inatoka Tanzania daima ya kila Jumapili binafsi nimekuwa nasoma sana Makala zake na ninampongeza kwa kazi nzuri anayoifanya.

Tupo pamoja mkuu! Huyu jamaa ni kifaa. Huwezi ukalinganisha na waandishi uchwara ambao bahati mbaya hapa nchini ndiyo wengi.
 
Invisible ukiiondoa hii Mods na wewe tunakufukuza kazi na tabia yako mbovu ya kujipendekeza kwa Mafisadi kikwete na Lowassa
 
Nimekugongea thanks mwandishi wa thread na heshima kwa kusimama (standing ovation) kwa Ansbert Ngurumo.

Tatizo ni zaidi ya kauli mbiu. Ebu fikiria hao mawaziri wameteuliwaje kama siyo kishikaji? Halafu kumbuka birds of same feathers flock togather. Wote wote kabisa wana umbumbu wa kiwango kikubwa tu juu ya uendeshaji wa serikali, baya zaidi uwaziri ni fursa pekee ya kujinufaisha kiwadhifa na kimaslahi.

Nikujuvyeni uzoefu wangu serikalini. Rais anapoingia madarakani na anapounda serikali yake muongozo hapa bongo ni yeye anavyotaka au anavyoshauriwa hata na mkewe, hakuna standing instructions zinazombana kuzingatia maslahi ya taifa kwa sababu hazipo kwa katiba ambayo ndiyo mkataba na wananchi. Mtakumbuka Nyerere aliwahi kusema angetaka angekuwa dikteta, alikuwa anamaanisha hicho. Lakini tuangalie anavyotoa majukumu ya utekelezaji (Mandate) kwa kila wizara.

1. Utayarishaji wake siyo makini kwa sababu hayana mwongozo bayana na yanafanywa kwa kulipua.

2. Mikakati yake pamoja na kutokuzingatia majukumu haifuatiliwi na kukubalika kukidhi mahitaji kwa kutoelewa, kwa ulege lege wa serikali au kwa mapungu wa uwezo wa watendaji (Low capacity).

3. Hakuna rasilimali zinazoambatana na majukumu hayo kwa sababu hazipo ila ni kutegemea bajeti ya makusanyo ya kila siku ambayo yanavuja.

4. Hakuna mrejesho unaofuata uwepo wa mfumo wa uthibiti wa kisayansi (Monitoring and Evaluation System)

Kwa hayo yaliyotajwa hapo kila kitu kinafanyika kiholela yaani utendaji wa serikali ni wa zima moto hawa agenda wala taratibu za utendaji.

Tabia inayozungumzwa hapo kwenye hii thread ya kufokea mawaziri na watendaji ni dhahiri shahiri udikteta wa namna fulani unaokubalika na genge zima za utawala. Kwa hiyo ni kweli kabisa ni anguko lililokwisha tokea. Ubaya ni kwamba hawa jamaa hawataki kuambiwa hivyo wala hawaoni tatizo ni nini kwa sababu ulimwengu wanaoishi ni tofauti na tunaoishi wananchi wote.

Chakufanya

1.Katiba MPYA ni lazima

2. Siasa za kitoto zinazoendeshwa nchini ziachwe, kuwe na umakini kwa wananchi kuelewa wanapoiingiza serikali ni kwa mkataba upi wa utekelezaji na si ahadi. Mkataba wa utekelezaji ni wenye sera, mikakati, na mipango ya utekezaji wenye rasilimali watu, pesa, taaluma na maadili yanayopimika kwa muda mfupi, wa kati na muda mrefu. Haya yote yakiwa yametoka kwa wananchi siyo kwa watawala walio out of touch na reality ya maisha ya watu.

3. Vyombo vya serikali vizingatie taaluma na utendaji huru usio na shinikizo la kisiasa. Limesemwa vizuri na Ansbert Ngurumo, anguko la kauli mbiu, anguko la rais, anguko la serikali yake lakini ni anguko la nchi.

Kweli nimefarijika na hii thread inajenga taswira ya JF inayotakiwa.
 
Hii kweli mistari! Naomba ninukuu huu mmoja:

''Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais "anayeishi kwenye ndege?"

Hili nalo neno!!
 
  • Thanks
Reactions: Bob
Uhuru wetu wa kutoa maoni ulinyongwa bila sababu maalumu enzi za zidumu fikra sahihi za mwenyekiti!! Sasa muda waukombozi umewadia na Ngurumo amefungua njia!!

Naomba wanamageuzi ujumbe huu usambazwe kwa mitandao yote ili walimwengu wajue serikali ya mkweree ilivyo!!
 
Umekuwa mwandishi bora wa wkenda,laiti ningelikuwa nasomea uandishi wa habari ningelikutumia saaana,umehit!

Leo nimebahatika kumwona JK anahitimisha semina pale Dom,nimemwangalia sana usoni,he is so scared and sorrowful (ana ujasiri wa woga),nimejiuliza saana endapo haya aliyoyaagiza hayatatimizwa na kwa jinsi alivyokuwa anaonekana,sijuhi itakuwaje,sielewi atafanya nini JK ukizingatia hapendi kushauriwa katika yaliyo mema/mabaya...asije kuchanganyikiwa
 
Ukitaka ukweli juu ya hilo ongea fresh na mods nije na tread yenye data zote tena za kweli!

Anwy tuachane na hayo tukae kwenye maada ya kamanda Ngurumo!!
Mbiu ya mnyonge ikilia katu tajiri hatoizuia!!

check PM yako mkuu
 
"Rais aneishi katika ndege" hahaha hili nalo neno! Umenena Ansbert ngurumo safi sana!!!!
 
"Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?"
Hana.... hana... hana kabisaaa... Ni kilaza mkubwa...
 
Back
Top Bottom