Anipa onyo baada ya kuhisi natembea na mkewe

Anipa onyo baada ya kuhisi natembea na mkewe

Acha kuchepuka, mke wa mtu sumu....utakatwa madubwasha.
 
Kwanini hukumwambia kuwa mlishaachana na mkewe?Huyo mama atakuwa analiwa kwingine lakini usoni kwake anaweka sura yako.Je, umechukuwa namba ya simu ya mume mwenzio? Itakuwa rahisi kumkamata huyo mke wenu huko anakotangatanga.
 
Assume una mke halafu ukaja kugundua siku moja mke wako ana uhusiano wa kimapenzi na MTU mwingine utajisikiaje? Kama utajisikia vizuri endelea naye,na kama kinyume chake ni sahihi basi ACHANA naye!!!
 
Duh pole sana kijana. Katika hali ya kawaida huyo jamaa ni mstaarabu sana. jambo la msingi unalopaswa kufanya ni kukata kabisa mawasiliano na huyo mwanamke haijalishi ataendelea kukusumbua kiasi gani maana ukirudia tena mwaisho wako utakuwa mbaya sana. Wake za watu wachungu sana.
 
Duh pole sana kijana. Katika hali ya kawaida huyo jamaa ni mstaarabu sana. jambo la msingi unalopaswa kufanya ni kukata kabisa mawasiliano na huyo mwanamke haijalishi ataendelea kukusumbua kiasi gani maana ukirudia tena mwaisho wako utakuwa mbaya sana. Wake za watu wachungu sana.[It is not enough to have a good memory the main thing is to it well]
 
Mambo ya wake za watu onyo ni mara moja tu kama lipo usijemwona ---- au anakuomba. Lengo lake wakati wanakutoa boxer usiseme sikujua
 
Tatizo kubwa ulilonalo wewe ni hili.. Jamaa ataamini vipi kama umeachana na mkewe..! Yaani chochote utakachofanya jamaa bado tu atakuwa na shaka na wewe maana ule msemo wa "muonja asali haonji mara moja" utakuwa unajirudia sana kichwani mwa jamaa..

Ushauri wangu tafuta kitu kama hii ya chini hapa na uwe unavaa.. Maana hujui muda wala saa........

lock.jpg
 
Aisee ukijaribu tu kurudia tena hakyanani unaliwa watsap na lazima ujinyonge...
 
Kwanini hukumwambia kuwa mlishaachana na mkewe?Huyo mama atakuwa analiwa kwingine lakini usoni kwake anaweka sura yako.Je, umechukuwa namba ya simu ya mume mwenzio? Itakuwa rahisi kumkamata huyo mke wenu huko anakotangatanga.

Hahahahaaaa sasa ana kazi ya kumsaidia mume mwenzie kumpata mchepuko. Atafute namba ya mume mwenzie ili awe safe side. Dunia ina vituko!!!
 
Huyo jamaa ni mtu wa hatari sana...kaa mbali na mke wake???
 
Kwa kuwa huyo mwanamke aliweza kutoka nje ya ndoa yake basi inawezekana pia huyo aliyekupa onyo ni mmoja kati ya mabwana zake sema huyo ana nguvu fulani kuliko wengine.Mume ahana haja ya kukupa onyo hata siku moja maana akishajua anaibiwa mali zake suala la onyo halipo,cha msingi angalia maisha yako wanawake wapo wengi na si lazima awe huyo.
 
Kama kweli umeshaachana naye lakini yeye anaendelea kuaga wa mumewe na kuhisiwa anakuja kwako; ongea na mumewe mweleze ukweli ili aendelee kumchunguza mkewe ili kuujua huo mchepuko mpya wa mkewe. Jiondoe hatarini huyo bwana ni mafia wallah atakuua.

Dah mkuu unamtisha mwenzako ujue....,Ila hapo kwenye red nimecheka mpaka basi...!
 
Umeamini kabisa huyo jamaa ni 'mstaarabu' ?nyoka wastaarabu unawajua?
You have been warned.

Mara nyingi watu mpaka washikishwe ukuta ndio wanajifunza.....wanawake wamejaa kibao...shida yote ya nn kuhatarisha maisha.
 
Back
Top Bottom