Angalizo: Usitafute mchumba kanisani

Angalizo: Usitafute mchumba kanisani

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,579
Reaction score
161,430
Makanisani ndio sehemu kwenye mafisi wengi wenye ngozi za kondoo.

Watu wengi waliokosa wachumba hukimbilia kanisani kudhani kuwa mke bora au mke mwema hupatikana kanisani, lakini mke mwema hutoka kwa Mungu. Penye watu wawili au watatu Mungu yupo katikati yao.

Makanisani watu ndio sehemu yao ya kutembeza ngoma, huko watu wanapigana mijeledi kinoma.
Waimba kwaya ni wazinzi kinoma.

Vijana ni wazinzi, wapigaji mizinga na matapeli kupindukia. Ukitaka mwenzi mwema, usiende kumtafuta kanisani, muombe Mungu akupe, naye atakupa kutoka kwenye hazina yake.

Huenda mkakutana kwenye daladala, au sehemu yoyote ile, usikate tamaa, Mungu ana jibu kwa wakati wake.

Ombeni bila kukoma.
 
Sehemu yeyote ile yenye mkusanyiko wa watu wengi ina watu wema na wabaya. Kwa hiyo mwandishi ungesema "kuweni makini mnavo tafuta wachumba makanisani"
Wako kinadada wazuri wanapatikana makanisani na wako kina dada wabovu kupindukia wanapatikana makanisani. Na hata wa mitaani ni hvo hivo.
*napenda kina dada wanao sali
 
Sehemu yeyote ile yenye mkusanyiko wa watu wengi ina watu wema na wabaya. Kwa hiyo mwandishi ungesema "kuweni makini mnavo tafuta wachumba makanisani"
Wako kinadada wazuri wanapatikana makanisani na wako kina dada wabovu kupindukia wanapatikana makanisani. Na hata wa mitaani ni hvo hivo.
*napenda kina dada wanao sali
Haswaaa,.palipo na wema,ubaya haukosi pia.
 
Ni kweli kabisa.,,,watu wengi huenda kanisani kutafuta wachumba.,lakini inahitaji umakini unaweza kujuta kuzaliwa.
 
Eeeh! Tena mbaya aliyepo kati ya wema anakuwaga nyoka mkubwa. Ni kuwa makini hoes are everywhere. Eti kwa kuwa mtu ni mnasali naye tuu basi ndio anafaa kuwa mke. Lazma ulie.

Ila mimi mwanamke anaye mpenda Mungu is a big plus kwa kweli.
Wadada wa biblia wapo hawawezi isha ila wanafichwa na hao wenye mingozi yao ya kondoo ndani chui...
 
Back
Top Bottom